Siko hapa kuwakebehi wanawake ama dada zetu lakini hii habari ni ya ukweli na iko-based na my own personal experience huko ughaibuni na kwa sasa hapa Dar. Nimejaribu mara kadhaa kutafuta rafiki kwaajili ya dating then kama chemistry ipo na tuna-click basi sitosita kuendelea kumpenda ambaye tutapatana ili eventually tufunge ndoa na nitulizane na mwenza wangu ili tuendelea na safari ya maisha.<br />
Baada ya kuwasaka akina dada wa mitaani/makazini/makanisani na miskitini etc. bila mafanikio nikaona sasa nihamie online dating, ambako nimekutana na wanawake wa aina mbalimbali lakini tatizo wanawake wengi wa mtandaoni sio wakweli. <br />
Utakuta mtu kaweka kwenye profile picha yake nzuri anapendeza na anavutia. Lakini tukikubaliana tuonane nakuwa nabaki mdomo wazi. <br />
1. Unakuta kwanza hiyo picha kumbe ni ya zamani alipokuwa bado umri haujaenda na akitokea unakuta umri umekwenda<br />
2. Mdada ni mnene zaidi transforma wakati alisema kwenye profile yake kuwa maumbile yake ni slim/average. <br />
3. Anadai ktk profile yake kuwa ni mrefu kumbe ni mfupi. n.k.<br />
<br />
Nimeshakutana na wadada 13 (8 ughaibuni 7 hapa hapa Dar) na mara zote nimepoteza muda wangu na pesa zangu kwaajili ya hizi dates na kuambulia kulipia gharama za dinner, wine, taxi etc at expensive restaurants. <br />
Swali: <br />
1.Je wanawake wanaotafuta wapenzi online ni wale ambao hawavutii kimaumbile na wako desperate?<br />
2. Kwa nini akina dada hawako wakweli ktk online profiles zao? mnaweka picha za zamani, mnadai wembamba kumbe wanene?