jjs2017
JF-Expert Member
- May 25, 2019
- 2,025
- 4,276
Bila kupepesa macho, niwaambie hawa wanawake / wamama wenye tabia za kuficha watoto wao wakike baba zao mwache hiyo tabia kwani mnawaathiri sana kisaikolojia.
Hata kama hukumpenda mwanaume ulie zaa nae huyo binti yako, hakuna sababu ya kumnyima haki mwanao ya kumjua baba yake pindi atakapo hitaji, wewe kama ulikosea kutokana na ulimbukeni wenu acheni kumtesa mtoto wa kike.
Mwanaume unajikuta katika harakati za kutongoza tongoza gafla anatokea binti umemuelewa, katika kuchunguza chunguza unanijikuta unamuukiza baba yako yupo wapi anakuambia hajui, unajitahidi kumdadisi anasema mama amekataa kunionyesha na hadi na fikia hapa simjui na hata kama amekufa hajanambia chochote huku mtoto wa kike analia machozi ya huzuni kuu, mnajibebea laana nyie wamama wa hovyo sana..
Sasa binti kama huyu kakosa upendo au malezi ya baba na wewe bado hata kumjua baba yake tuu hutaki amjue unamaana gani, hata kama alimkataa akiwa mdogo au ukiwa na mimba yake sio sababu binti kafika miaka 18+ bado unakataa asimjue baba yake , hiyo laana ni kali sana ole wenu .mwache upumbavu na ulimbukeni wa kipuuzi..
Hata kama baba yake alifariki wewe mwonyeshe tuu hata kaburi lake, hata kama yupo kifungoni wewe mwonyeshe tuu na hata kama mlipotezana mwambie tuu binti ukweli sio unamtesa kiakili , mnatupa wakati mgumu sana tunapo uliza mwaswali kama haya tukikutana na mabinti wa aina hii
Nb. Sometime tunauliza tuu kujua chimbuko la binti pale tunapo dhamiria kumuoa
Hata kama hukumpenda mwanaume ulie zaa nae huyo binti yako, hakuna sababu ya kumnyima haki mwanao ya kumjua baba yake pindi atakapo hitaji, wewe kama ulikosea kutokana na ulimbukeni wenu acheni kumtesa mtoto wa kike.
Mwanaume unajikuta katika harakati za kutongoza tongoza gafla anatokea binti umemuelewa, katika kuchunguza chunguza unanijikuta unamuukiza baba yako yupo wapi anakuambia hajui, unajitahidi kumdadisi anasema mama amekataa kunionyesha na hadi na fikia hapa simjui na hata kama amekufa hajanambia chochote huku mtoto wa kike analia machozi ya huzuni kuu, mnajibebea laana nyie wamama wa hovyo sana..
Sasa binti kama huyu kakosa upendo au malezi ya baba na wewe bado hata kumjua baba yake tuu hutaki amjue unamaana gani, hata kama alimkataa akiwa mdogo au ukiwa na mimba yake sio sababu binti kafika miaka 18+ bado unakataa asimjue baba yake , hiyo laana ni kali sana ole wenu .mwache upumbavu na ulimbukeni wa kipuuzi..
Hata kama baba yake alifariki wewe mwonyeshe tuu hata kaburi lake, hata kama yupo kifungoni wewe mwonyeshe tuu na hata kama mlipotezana mwambie tuu binti ukweli sio unamtesa kiakili , mnatupa wakati mgumu sana tunapo uliza mwaswali kama haya tukikutana na mabinti wa aina hii
Nb. Sometime tunauliza tuu kujua chimbuko la binti pale tunapo dhamiria kumuoa