Elections 2010 Wanawake watatuangusha uchaguzi huu wabadilike

MTWA

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2009
Posts
1,166
Reaction score
168
Mara nyingi sana napata mawazo ya watu wengi sana kuhusu uchaguzi wa mwaka huu,
nikikutana na akina mama karibia wote, wanalaumu sana JK kwa mambo alivyoyaendesha, lakini wanasema Upinzania hauwezi kushinda, eti CCM itashinda,

lakini linaloniuma sana ni kwamba wanasema kura yao hawataki kuipoteza kumpa mtu ambaye hatashinda. Najaribu kuwaelekeza kuwa hiyo ndo msg kwa kiongozi wao, lakini hawataki.

kwa hili naona kuwa watatupoteza sana maana wanataarifa juu ya utendaji mbovu wa JK lakini hawataki kumtosa kwa kura zao, Jamani tuwaelimishe popote tunapokuwa, kwa hizi siku za majeruhi!
 
Tatizo kubwa zaidi ni kwenye vyombo vya DOLA. Hasa wakubwa wao. Wanadhani na wanataka sisi tuamini kuwa bila CCM, Tanzania haipo.
 


Habari ndio hiyo,its nbetter you have learned it
 
Na zile msg za vitisho bado wanatuma, kumbe kuna mdada mmoja hapa, ametumiwa na bosi wake, kuwa
"Usiache kupiigakura, Mchague kikwete, usipoteze kura yako kwa waeneza fujo, udini na ukabila" wakati yeye kwenye ile msg ndo kaweka na udini ndani yake.

Tuwaelimisheje waoga katika nchi hii?
Maana wao wanakiri kabisa kuwa Kikwete anawakera sana kwa mambo yake!
 
Ni kweli wanawake wamepumbazwa sana,wamepewa kanga ndani yake kuna buku 2,alafu anaambiwa katafute wenzako kumi,hawa si wengine bali ni wakina mama wa uswazi hapa tegeta,harafu kawaangalie wanavyo lazwa kwenye sakafu pale m'nyamala wakiwa wanajifungua.
 
Do not ignore the power of women ! Hawadanganyiki mwaka huu kura zao kwa Dr Slaa
 
Do not ignore the power of women ! Hawadanganyiki mwaka huu kura zao kwa Dr Slaa

Hawa watu wanasikitisha sana kwa sababu wanadanganyka kwa vitu vidogo, wakati wa kwanza kuteseka kwa uongozi mbaya ndio wao kwanza.
Maji, shule, hospital, utawakuta wao ndo wengi.. Cha ajabu wanayosema ni tofauti kabisa
 
Wapiga kura waliowengi wanataka umewashawishi kiasi gani sio unajua kiasi gani,hivyo akina mama wakishawishika watampigia kura.
 
Unyonge wao ndiyo unasababisha yote haya, wanapewa tuvimikopo vya laki laki huku wakitakiwa kurejesha kila wiki kwa riba iliyo juu,wanaungua na moto kutwa kwa faida ya sh alfu 3, wanatembeza bidhaa za promosheni kutwa kwa ujira wa alfu jero, Je akitokea mtu akawapa chips mayai, valuu ili wamwage radhi vizuri na spika kubwa za mzee yusuf, kanga na buku mbilimbili ndani unategemea nini?
 
Kwa wale ambao wana wasiwasi kuhusu upigaji kura wa wake zao, siku hiyo ya Jumapili waanzishe ka-zogo kadogo nyumbani ili wasiende vituoni!! Tehe, tehe tehe!!!!! Mikweza kuwazuia nusu ya wanawake kwenda vituoni, nafikiri CCM ni bye bye for real!!!!!!!
 
WANAPENDA TABASAM LA JK SIYO SERA ZA CCM na kuwabadili ipo kazi.

Sio kweli wakina mama wengi sana wamemstukia Kiwete kuwa anawadanganya na safari hii watamtosa; wanasema kwani watoto wao watakula hilo tabasamu lake? Karo za shule zinawaumiza na DR. amewaahidi shule bure kwahiyo wamama wengi mpaka vijijini siku hizi hawadanganyiki kwa khanga, watampa Slaa kura zao!!
 
mimi mke wangu hapana hayumo katika ujinga huo. Anajua sukari tu imepanda toka tshs.400(2005) hadi Tshs1800(2010). Na hataki ujinga wa kanga za Tshs.500.

CHAGUA CHADEMA
 

hao wakiwezeshwa ndo wanaweza TUWAWEZESHE JAMANi
 
Naona lugha za mashabiki wa Chadema JF zinachukuwa sura mpya kadri uchaguzi unavyokaribia, naona wanaanza kukubali uhalisia wa matokeo ya uchaguzi ujao. Kama ni dhahiri wanawake waitaipigia kura CCM, kama ni dhahiri kwamba Chadema haijasimamisha wagombea katika majimbo kadhaa, kama ni dhahiri kwamba baadhi ya wanachama wachedema wanasikitishwa na kampeni za matusi, matumaini ya Chadema kushinda yanashikiriwa na nguzo gani? Nielimisheni.
 
mimi mke wangu hapana hayumo katika ujinga huo. Anajua sukari tu imepanda toka tshs.400(2005) hadi Tshs1800(2010). Na hataki ujinga wa kanga za Tshs.500.

CHAGUA CHADEMA

Maisha si mchezo ni vita usiendekeze uzembe wa kumwachia mwanamke afanye jambo utakalolijutia kwa miaka 5, mwelimishe, mshauri ikibidi msaidie kupiga kura. VITENGE/KANGA, TSHIRT, KOFIA, VILEMBA NA MABANGO YASITULETEE ADHABU YA MIAKA 5 KURA YENYE TIJA PIGIA CHADEMA VEMAAAA Pipooos Pawaaaaaa.
 
Wapiga kura waliowengi wanataka umewashawishi kiasi gani sio unajua kiasi gani,hivyo akina mama wakishawishika watampigia kura.
Du, ndugu mimi sidhani kuwa ni sahihi, kwa sababu hii ni suala la kuangalia haki yako, maendeleo yako. Mbaya zaid ni hao wakina mama wanaoteseka na wao wanasema, sasa kwanini upate shida, au usubiri ushawishiwe ndo uchague haki yako?
Wao wameshateseka vyakutosha mahospitalini, usafiri masokoni, watoto, bado wanataka kuambiwa nini
 

Bado sana ila kuna mambo ambayo yanatokea pia kwa rafu za hao hao mafisadi.
Maana wamewahonga na kuwatisha, na bado wataiba
 
hao wakiwezeshwa ndo wanaweza TUWAWEZESHE JAMANi

Kwa hili Jamani sasa haki sawa iko wapi?
wanatakiwa kuwa waelewa nini wanahitaji. haya mambo ya sitaki nataka hadi wasomeshwe sana yatatupeleka Jehanum mapemaaaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…