Wanigeria na Wahindi wamefanikiwa sana kutambulisha utaifa wao kupitia mavazi

Wanigeria na Wahindi wamefanikiwa sana kutambulisha utaifa wao kupitia mavazi

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
1694247176510.png
Indian Prime Minister Narendra Modi shakes hands with Nigeria President Bola Ahmed Tinubu upon his arrival

Sisi tunakwama wapi? Wahindi wanaona fahari sana kutumia mavazi kama njia ya kutambulisha utaifa wao, hali kadhalika wa-nigeria. Waarabu pia wako vizuri katika hili.

Hivi imeshindikana kabisa wabunifu wetu wa mavazi wakabuni vazi kama utambulisho wa Taifa letu? Cha maana liwe ni vazi lenye staha tu.
 
Hizi ni Petty issues,
Lakini pia hakuna vazi la utamaduni mmoja Tanzania, huwezi kumuambia mtu wa pwani aliyezoea kuvaa vijora au kanzu avae Rubega au shuka za Wamasai.
 
Hizi ni Petty issues,
Lakini pia hakuna vazi la utamaduni mmoja Tanzania, huwezi kumuambia mtu wa pwani aliyezoea kuvaa vijora au kanzu avae Rubega au shuka za Wamasai.
Hujanielewa! Kuwa na vazi rasmi la Taifa haina maana uondoe mavazi rasmi ya makabila mbali mbali!! Inatakiwa kubuni vazi rasmi la kitaifa mbali na mavazi mengine ya kiutamaduni wa mikoa mbali mbali!!

Halafu utambulisho wa kitaifa SIYO PETTY ISSUE!! That is a very big misconception!! Kwa mfano lugha ya kiswahili ni utambulisho wa Taifa letu, japo kuna nchi zingine pia kiswahili hutumika lakini inatambulika kuwa Tanzania ndiyo kitovu cha kiswahili. Kama ambavyo Kiingereza huzungumzwa na mataifa mbalimbali lakini inajulikana kitovu chake ni UINGEREZA. Kwa bahati mbaya sana watanzania hawajivunii kiswahili chao, na wakiongea kiingereza huonekana kujisikia vizuri zaidi., hiyo ni mentality ya kitumwa!!
 
Hujanielewa! Kuwa na vazi rasmi la Taifa haina maana uondoe mavazi rasmi ya makabila mbali mbali!! Inatakiwa kubuni vazi rasmi la kitaifa mbali na mavazi mengine ya kiutamaduni wa mikoa mbali mbali!!

Halafu utambulisho wa kitaifa SIYO PETTY ISSUE!! That is a very big misconception!! Kwa mfano lugha ya kiswahili ni utambulisho wa Taifa letu, japo kuna nchi zingine pia kiswahili hutumika lakini inatambulika kuwa Tanzania ndiyo kitovu cha kiswahili. Kama ambavyo Kiingereza huzungumzwa na mataifa mbalimbali lakini inajulikana kitovu chake ni UINGEREZA. Kwa bahati mbaya sana watanzania hawajivunii kiswahili chao, na wakiongea kiingereza huonekana kujisikia vizuri zaidi., hiyo ni mentality ya kitumwa!!
Hakuna taifa walilokaa chini wakabuni vazi la kitaifa, pia hata hao wenyewe hayatambulishi hayo mavazi kama ya kitaifa kwao.
 
Hakuna taifa walilokaa chini wakabuni vazi la kitaifa, pia hata hao wenyewe hayatambulishi hayo mavazi kama ya kitaifa kwao.
Hawakuwa na haja ya kukaa kwa kuwa tayari kuna vazi lililokuwa linawatambulisha!! Wasiokuwa na vazi ndio wanatakiwa kukaa na kuamua vazi lipi walipendekeze kuwa vazi la utambulisho wa utaifa wao!!
 
View attachment 2743858
Indian Prime Minister Narendra Modi shakes hands with Nigeria President Bola Ahmed Tinubu upon his arrival [Evan Vucci/Pool via Reuters]

Sisi tunakwama wapi? Wahindi wanaona fahari sana kutumia mavazi kama njia ya kutambulisha utaifa wao, hali kadhalika wa-nigeria. Waarabu pia wako vizuri katika hili. Hivi imeshindikana kabisa wabunifu wetu wa mavazi wakabuni vazi kama utambulisho wa Taifa letu? Cha maana liwe ni vazi lenye staha tu!!
Hii nayo iwe agenda au? Pambana na njaa, umaskini, elimu duni, miundombinu, nk.
 
Hayo mavazo sio wahindi tu, wapakistani na jamii nyingine wanavaa hivyo.
Kuhusu nigeria, naona waafrika magharibi wengi wanavaa hivyo.
 
Wewe tengeneza Vazi zuri tu (likiwa Cool kila mtu atalipenda na kulivaa) Sio huku tu bali Ulimwengu mzima...

Hivi unajua asili ya Batiki (utashangaa wala sio Africa); Kanzu inatokana na mazingira pia kwenye joto ni more comfortable..., Hence with fashion sio lazima watu wakae wewe tu leo unaweza ukaja na mtindo wa mashati Middle Sleeves (yaani sio short wala long) kila mtu akafuata..., Au zile Kaunda suti (sio Kaunda alizianzisha ila alizifanya mainstream) Mashati ya Mandela halikadhalika (nothing to do with SA)

Je OPP (bila Naughty by Nature huenda yangeendelea kuishia huku huko kwenye baridi) na Pull Necks je (ni fashion au vazi la kujikinga na baridi) ? Premier- League sababu ya baridi watu kuvaa scarf kulifanya iende mainstream hadi Dar kwenye Joto la Jehanum watu walivaa Scarf (moral of the Story; jambo zuri / promoted litachukuliwa na jamii)

Huku kwetu kuna kipindi watu walivaa sana mavitenge na Khanga na Samia angekuwa anaupiga mwingi kweli huenda Ushungi ungekuwa vazi la Taifa.... (kumbe wengine ni wavivu tu wakuchana nywele na wanaficha kipilipili)
 
Wewe tengeneza Vazi zuri tu (likiwa Cool kila mtu atalipenda na kulivaa) Sio huku tu bali Ulimwengu mzima...

Hivi unajua asili ya Batiki (utashangaa wala sio Africa); Kanzu inatokana na mazingira pia kwenye joto ni more comfortable..., Hence with fashion sio lazima watu wakae wewe tu leo unaweza ukaja na mtindo wa mashati Middle Sleeves (yaani sio short wala long) kila mtu akafuata..., Au zile Kaunda suti (sio Kaunda alizianzisha ila alizifanya mainstream) Mashati ya Mandela halikadhalika (nothing to do with SA)

Je OPP (bila Naughty by Nature huenda yangeendelea kuishia huku huko kwenye baridi) na Pull Necks je (ni fashion au vazi la kujikinga na baridi) ? Premier- League sababu ya baridi watu kuvaa scarf kulifanya iende mainstream hadi Dar kwenye Joto la Jehanum watu walivaa Scarf (moral of the Story; jambo zuri / promoted litachukuliwa na jamii)

Huku kwetu kuna kipindi watu walivaa sana mavitenge na Khanga na Samia angekuwa anaupiga mwingi kweli huenda Ushungi ungekuwa vazi la Taifa.... (kumbe wengine ni wavivu tu wakuchana nywele na wanaficha kipilipili)
Is minor issue. What is mavazi in this globalized world?
People are discussing about economic, social welfare services then you talk about vazi la taifa? So what?
 
Is minor issue. What is mavazi in this globalized world?
Moja ya basic needs za mwanadamu; A feel good factor; A consumable ambayo inamfanya mtu afanye kazi ili aweze kupata hii need/ want
People are discussing about economic,
As one of the basic need its directly proportional to the economy of an individual and state as a whole - (sitashangaa kuona kwamba mavazi ni moja ya consumption kubwa ya individual - people want to look good)
social welfare services then you talk about vazi la taifa? So what?
Am not talking about vazi la taifa nimemwambia mleta uzi akitengeneza vazi unique likapendwa na taifa / jamii ya sehemu fulani basi vazi hilo lita-identify sehemu husika hakuna haja ya kukaa na kuchagua / kupangiana vitu vya kuvaa unless ni matambiko au utamaduni
 
View attachment 2743858
Indian Prime Minister Narendra Modi shakes hands with Nigeria President Bola Ahmed Tinubu upon his arrival [Evan Vucci/Pool via Reuters]

Sisi tunakwama wapi? Wahindi wanaona fahari sana kutumia mavazi kama njia ya kutambulisha utaifa wao, hali kadhalika wa-nigeria. Waarabu pia wako vizuri katika hili. Hivi imeshindikana kabisa wabunifu wetu wa mavazi wakabuni vazi kama utambulisho wa Taifa letu? Cha maana liwe ni vazi lenye staha tu!!
Wabunifu wenyewe wahindi
 
Hujanielewa! Kuwa na vazi rasmi la Taifa haina maana uondoe mavazi rasmi ya makabila mbali mbali!! Inatakiwa kubuni vazi rasmi la kitaifa mbali na mavazi mengine ya kiutamaduni wa mikoa mbali mbali!!

Halafu utambulisho wa kitaifa SIYO PETTY ISSUE!! That is a very big misconception!! Kwa mfano lugha ya kiswahili ni utambulisho wa Taifa letu, japo kuna nchi zingine pia kiswahili hutumika lakini inatambulika kuwa Tanzania ndiyo kitovu cha kiswahili. Kama ambavyo Kiingereza huzungumzwa na mataifa mbalimbali lakini inajulikana kitovu chake ni UINGEREZA. Kwa bahati mbaya sana watanzania hawajivunii kiswahili chao, na wakiongea kiingereza huonekana kujisikia vizuri zaidi., hiyo ni mentality ya kitumwa!!
Mentallity tuliyonayo ni kwamba ukivaa suti na tai unaonekana una elimu kubwa na una pesa mingi !!
Hata kwenye joto kali la Dar tunapigaga three pieces suits !! Acha mchezo kabisa 😅😅🙏🙏
 
Vazi la mtanzania linajulikana mfano wakina mama angali kweny shehere zao za kitaifa utaona wanavaa sana mbona ...Marehemu Amina chifupa ndo alikuwa anapenda kuvaa vazi la mtanzania mda wowote .
Wanaume nao kawaida sana unavyopenda ila sio vipesi kama watu wa Dar.
 
Hujanielewa! Kuwa na vazi rasmi la Taifa haina maana uondoe mavazi rasmi ya makabila mbali mbali!! Inatakiwa kubuni vazi rasmi la kitaifa mbali na mavazi mengine ya kiutamaduni wa mikoa mbali mbali!!

Halafu utambulisho wa kitaifa SIYO PETTY ISSUE!! That is a very big misconception!! Kwa mfano lugha ya kiswahili ni utambulisho wa Taifa letu, japo kuna nchi zingine pia kiswahili hutumika lakini inatambulika kuwa Tanzania ndiyo kitovu cha kiswahili. Kama ambavyo Kiingereza huzungumzwa na mataifa mbalimbali lakini inajulikana kitovu chake ni UINGEREZA. Kwa bahati mbaya sana watanzania hawajivunii kiswahili chao, na wakiongea kiingereza huonekana kujisikia vizuri zaidi., hiyo ni mentality ya kitumwa!!
Mawazo yangu, kama taifa tuachane na mambo ambayo hayana mchango wowote ktk maendeleo. Mambo ya lugha, tamaduni, matambiko and the like tuwaachie makabila kila mtu na kabila lake na utamaduni wake. Tutafute elimu na maarifa yatakayotusaidia kutatua changamoto zetu za umaskini, afya na elimu. Mambo ya mavazi yatatusaidia nini? Ndio hivi tumeng'ang'ania kiswahili matokeo yake tumageuka mabubu mbele ya watu wa mataifa mengine, tunashindwa kufaidi fursa za ajira na elimu zilizopo duniani. Hawa "wakoloni" wanaotutawala watoto wao wanawasomesha ulaya, America, afrika kusini nk; halafu sisi wanatuambia watoto wetu tuwapeleke elimu bure huko kwenye kata, wakimaliza wanaambiwa wajiajiri wakati watoto wao wanapewa ajira kwenye idara za serikali na majeshi.
 
Hawakuwa na haja ya kukaa kwa kuwa tayari kuna vazi lililokuwa linawatambulisha!! Wasiokuwa na vazi ndio wanatakiwa kukaa na kuamua vazi lipi walipendekeze kuwa vazi la utambulisho wa utaifa wao!!
Kupitia vazi hilo unaloita la kitaifa wameongeza nini?
 
Kupitia vazi hilo unaloita la kitaifa wameongeza nini?
Swali lenye mantiki hili. Kama kuvaa mavazi ya aina fulani kungekuwa kunaongeza kitu katika maendeleo kiuchumi,basi ingetulazimu kuvaa mavazi ya watu wa maeneo fulani ili twende nao sambamba kimaendeleo.
Miaka ya sitini,sabini na themanini mwanzoni, wachina walitambulika zaidi kwa kuvaa suti zao zisizo na collar,zilizovaliwa na kutambulishwa zaidi na viongozi wao...kiasi cha kufikia suti ya aina hiyo kuitwa jina la Chou En Lai huku kwetu..,jina la waziri mkuu wa China miaka hiyo aliyependa sana kuvaa suuti muundo huo.
Leo viongozi wa China wanavaa suti za kimagharibi zaidi.
Leo China ni taifa namba 2 kwa uchumi mkubwa duniani...,wamefikia hatua hiyo siyo kwa sababu ya mavazi ya kwao au ya kimagharibi. Wamepiga hatua basda ya kufanya mikakati mahsusi katika sera zao za kiuchumi na kuweka bidii katika kazi.
Waarabu wa Yemen na wa Qatar wote wanavaa mavazi ya asili ya maeneo yao,..kanzu, lakini hawafanani kiuchumi.
 
Wamasai wanatutambulisha vema.

Napendekeza wathibitishwe kama tunu ya taifa. Pia wapewe maeneo yao ya asili kule Ngorongoro.
 
View attachment 2743858
Indian Prime Minister Narendra Modi shakes hands with Nigeria President Bola Ahmed Tinubu upon his arrival [Evan Vucci/Pool via Reuters]

Sisi tunakwama wapi? Wahindi wanaona fahari sana kutumia mavazi kama njia ya kutambulisha utaifa wao, hali kadhalika wa-nigeria. Waarabu pia wako vizuri katika hili. Hivi imeshindikana kabisa wabunifu wetu wa mavazi wakabuni vazi kama utambulisho wa Taifa letu? Cha maana liwe ni vazi lenye staha tu!!
Tuwaulize ninyi UVCCM; si kila awamu mnapewaga tenda ya kutafuta vazi la taifa mnaishia kupiga ufisadi na hakuna kinachoendelea?

Kwamba hujui tumekwama wapi au kikwazo ni nini huo ni unafiki.
 
Back
Top Bottom