Wankyo Nyigesa, RPC Kagera: Natamani kuwa IGP, aliyepo hajafanya makosa lakini mimi nitafanya mazuri zaidi

Tunaposena JESHI LIUNDWE UPYA ndo tunamaanisha hivi, hata nidhamu naona kama imeshuka jamani!! Unawezaje kuitamani nafasi ya boss wako alieko madarakani?

Jeshi sio chama cha siasa! Huku ni sawa na kumwambia mkuu wa nchi kuwa mteule wake hatoshi!! Kwamba atafanya mazuri zaidi ya mkuu wake!!!?
 


Huyo hafai katika kazi hiyo, atakuwa hovyoo.
 
Mnajaribu sana kurudisha hizo Siasa za udini udini ila kila Mkiingiza hizo 'single' studio zinakataliwa

Kikundi kinachokula Mema ya Nchi kina watu wa dini zote, makabila yote kutoka maeneo yote na kinachowaunganisha ni michongo tu…nyie mmekaa kijiweni mnahesabu majina ya kidini ya walioteuliwa

Wankyo kama ni Mktistu imekula kwake
 
Ni vyema mwanadamu kutazama mbali, tena ni nimependa zaidi aliposema apewe miaka mitatu tu then amwambie mama kazi uliyonikabidhi imetosha.

Huyu anaonekana ameshajua anachotaka kwenda kufanya, ana mipango kichwani, ameshaona mapungufu ya IGP aliyepo hivyo anataka kwenda kuyafanyia kazi.

Tatizo lililopo kwake naona litakuwa ni uhuru wa kutimiza majukumu yake, kama akiteuliwa na Rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM lazima atasikiliza na kufuata mapendekezo yake, na hili litampunguzia nguvu ya kutimiza majukumu yake.
 
Ni wale wale tuu. Kwani Azori akichukukiwa wapi? Viroba vya maiti viliokotwa wapi kama sio mkoa wa Pwani??
Wankyo ni wa kanda gani??

Hii labda Sirro ndie kapendekeza jina la home boy ili walindane.. Pole sana mzee
 
Anatamani kuinuliwa kama yule askari Magereza enzi za Mwendazake, basi asuburi maombi yake yajibiwe
 
Hapo ndipo tulipofika ndani ya jeshi la Polisi, ni mwendo wa kusaka vyeo kwa mgongo wa kujipendekeza kwa wanasiasa. Walianza kwa kulogana, wakahamia kwenye kufitiana na mwisho wa siku matamalizia kwa kuuana.
 
Hakuna ubaya ila sio busara kuongea ndoto zako kwenye mazingira kama hayo. Huyo kamanda angekua ni afisa wa cheo cha chini kisha akajiwekea hayo malengo na akayazungumza wala isingekua na tafsiri hii ambayo nimeifikiria.

Ila unapokua na cheo kikubwa kinachokaribia na nafasi unayoitamani kisha ukaizungumza hadharani hiyo ni dhahiri unatamani cheo cha boss wako kabla ya wakati au unamwona boss wako hatoshi kwenye hiyo nafasi.

Lakini pia ingekua hiyo nafasi anayoitamani ni nafasi ya kusoma na kupanda cheo isingekua na shida maana jitihada zake zingemfikisha uko ila kwavile nafasi yenyewe ni moja na ni ya kuteuliwa kuongea hadharani hiyo ndoto nikumkosea nidhamu aliyepo kwenye hiyo nafasi. Huu ni mtazamo wangu lakini.
 
LUMUMBA by products hizo pwani ndio kuliokotwa viroba vya kutosha kuwapeleka jiwe na sirro the Hague, huyu ana hasira na uhamisho huo
 
Wewe unaamini hizo porojo za miaka mitatu au kua na vision. Hata hivyo Uzoefu wa kiafrika unaonyesha watu wanaojipigia debe mara nyingi wakipata hiyo nafasi wanakuaga wabovu kupindukia.

Mimi naamini kwenye uwezo wa mtu. Ukiwa na uwezo au mawazo makubwa utaonekana tu. Maana unatakiwa uanze kuonyesha uwezo na mawazo yako kuanzia pale ulipo. Kisha uwezo wako ndio ukupandishe sio kujipigia debe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…