Uchaguzi 2020 Wanufaika na wanufaika watarajiwa wa bodi ya mikopo mnayo kila sababu ya kuikataa CCM na kumchagua Lissu

Uchaguzi 2020 Wanufaika na wanufaika watarajiwa wa bodi ya mikopo mnayo kila sababu ya kuikataa CCM na kumchagua Lissu

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Miongoni mwa mambo ya kustaajabisha ya awamu ya tano ni sheria mpya zilizotungwa pamoja na marekebisho ya sheria za zamani waliyoyafanya.

Kuna muda ukikaa utafakari unashindwa hata kuelewa hawa watu wanafanya haya kwa lengo la kumkomoa nani? Kuna baadhi ya sheria ni za ajabu kwelikweli hadi wao wenyewe wakalazimika kuzifanyia marekebisho tena au kabla hata ya mwaka mmoja kuisha.

Tukiigusia kwa ufupi hii sheria ya bodi ya mikopo, kwa sasa mkopo huu umefanywa kama mkopo wa biashara, kwanza marejesho yake ni 15%, kwenye ripoti za CAG mara kadhaa alieleza jinsi makato hayo yalivyo kuwa mzigo mzito kwa wafanyakazi ambao wanazigo la makato mengine mengi kwenye mishahara yao.

Pili kuna kitu kinaitwa 'value 'retention fee' ambayo ni 6% ya deni lililobakia kwa kila mwaka. 'riba' hii imeongeza mzigo mzito kwa walipaji na kuna baadhi wako hatarini kutomaliza madeni yao hadi wanastaafu.

Sasa serikali inayotunga sheria za aina hii haistahili kura yako kwakua ni wazi kuwa hawajali sheria hizo zinakuumiza kiasi gani

Kwa wale mlio sekondari na mmefikia umri wa kupiga kura, ninyi ndio kabisaa msithubutu kuwapigia hawa CCM, waulizeni dada na kaka zenu waliosoma shule binafsi ni wangapi wamepata mkopo?

CCM watataka kuwalaghai kuwa 'idadi ya wanufaika imeongezeka', huu ni upotoshaji wa maksudi kabisa, ukweli ni kwamba idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa imeongezeka sana, ndio maana idadi ya wanufaika inaonekana kama imeongezeka. Lakini ukiangalia kwa asilimia, waombaji wengi zaidi wanakosa mikopo ukilinganisha na hali ilivyokua 2015 kurudi nyuma.

Bodi inawanyima mikopo wanafunzi karibia wote waliosoma shule binafsi, pia wanakomaa kuangalia makosa madogo madogo ya ujazaji form na kuyatumia kunyima watu mikopo.

Sasa hali hii hairidhishi, na ili ibadilike ni lazima ukapige kura na kumpigia mtu sahihi, Lissu ameahidi kwa dhati kuifanyia marekebisho sheria ya bodi ya mikopo pamoja na sheria nyingine nyingi za kikandamizaji za CCM.
 
Huwa nashangaa sana kuona bado kuna watanzania wanaendelea kufikiria kuwachagua wabunge kutoka CCM wakati ndio wanaopitisha hizi sheria.
Tukiwapa mitano tena ndio itakua balaa, unajua Magufuli hajali sana kuhusu CCM au serikali zitakazo fuata baada yake, kutokana na nature yake ya ubinafsi anachojali ni legacy yake tu, ndio maana haoni tabu kukopa matrilioni kwa ajili ya white elephant projects alimradi yeye ataacha structure zimesimama akiamini kuwa watu watazitizama na kumkumbuka.
 
Huwa nawaangalia wale wanafunzi wa vyuo wanaoshabikia ccm najiuliza hivi wanajua wanachokishabikia?

siku watakapomaliza vyuo na kuanza kuzurura mitaani huku bodi ikiwatolea macho ndio akili zitawakaa sawa.
 
Huwa nawaangalia wale wanafunzi wa vyuo wanaoshabikia ccm najiuliza hivi wanajua wanachokishabikia?

siku watakapomaliza vyuo na kuanza kuzurura mitaani huku bodi ikiwatolea macho ndio akili zitawakaa sawa.
Watajuta kwa kweli, kuna penalti ya 10% kila mwaka na hiyo retention fee ya 6%. Siku ukienda kuomba statement ya deni unaweza kuzimia palepale.
 
Huwa nashangaa sana kuona bado kuna watanzania wanaendelea kufikiria kuwachagua wabunge kutoka CCM wakati ndio wanaopitisha hizi sheria.
CCM kama maji, usipoyaoga utayanywa. Wabunge wa Chadema kina nani? Hawa wanaogoma, kususa,kutukana Serikali yao kila uchao huku posho, mishahara wanachukua na majimboni kwao hakuna walichofanya.Ukawa uliwapa wabunge 70,ila safari hii mkipata 10 Mungu ashukuriwe,maana wananchi wamechoshwa na ulaghai, ubabaishaji wenu. Rais wa CCM, wabunge wa CCM, madiwani wa ccm ndivyo itakavyokuwa.
 
Jana nilifanikiwa kusoma mchanganuo wa marejesho ya hizo pesa za bodi ! Kweli inasikitisha sana! Nikagundua vitu viwili Mosi Ni heri mzazi akope pesa mwanae asome kuliko ajiweke kwenye huu mtego , Pili walioshiriki kutunga hizo sarakasi watoto wao hawasomi huko nchini na kama wanasoma basi wamekatazwa kujiandikisha kwenye huo umasikini wa kudumu!
 
Back
Top Bottom