Wanufaika wa Katiba Iliyopo hawahitaji elimu

Wanufaika wa Katiba Iliyopo hawahitaji elimu

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Katiba Iliyopo ina mapungufu mengi yasiyoweza kuvumilika zaidi.

Ni wazi kuwa anayebeza jitihada zozote za kuanzishwa tena kwa mchakato wa kupata katiba mpya kiporo uliobakia, ni kwa sababu tu ya kuwa na uelewa mdogo au ni mnufaika wa moja kwa moja wa katiba mbovu hii iliyopo.

Wanaobeza jitihada hizi wamo katika makundi haya mawili tu wala si vinginevyo.

IMG_20210701_164655_928.jpg

Kwa wale wasioelewa ni jukumu letu kuwaelimisha wakapate kujua kwa nini katiba mpya ni muhimu sana kwao. Labda pia kwa nini ni muhimu zaidi sasa kuliko wakati mwingine baadaye.

Hatuna haja ya kupoteza muda na wanufaika wa mfumo. Hao wanatumia mbinu na sababu zozote zikiwamo za kijinga kuona kuwa mchakato huo hautapata kurejelewa kwa kadri iwezekanavyo.

Kwa hao ilikuwa ni muda muafaka sasa kuwasusia, zikiwamo shughuli zao, na hata "nyuzi na mabandiko yao yote." Hatuna haja ya kupoteza na muda wala kuwa na marumbano yoyote ya maneno na watu hawa kwa sasa.

Kama mbwai na wajue kabisa imeshakuwa mbwai!

Wanadhani tutasusa tu uchaguzi au hatutaweza kukabiliana nao sawia kuhakikisha katiba mpya inapatikana. Kwa mawili haya, ni wajibu wetu kuona kuwa hayawi faida kwao.

Tupambane kivyetu nao wapambane na hali zao.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Si kwa maneno bali kwa vitendo:


Au siyo bwana Extrovert @bukililo Mulokozijr12 na wazalendo wenzangu?
Unajua hamna tuzo ya kuwa raia mwema laiti ingekuwapo ningeshabikia katiba.

Mie sinufaiki na lolote katika hio katiba maana ni kwa vile sifanyi uhalifu wala sijishughulishi na siasa! Siwezi kushabikia wala kupinga mchakato wa katiba mpya ila tu mtu asinishurutishe maana binafsi hainiathiri kwa namna moja ama nyengine maisha yangu ya kawaida tu! Mnaopambania ipambanieni tu.

Wenye maslahi ni wanasiasa na wahalifu maana ndio ina vipengele vya kuwatetea na kuwaneemesha kwahio lazma wawe na moto nayo! Sasa jiulize makundi haya mawili ni watanzania wote million 60?
 
Unajua hamna tuzo ya kuwa raia mwema laiti ingekuwapo ningeshabikia katiba.

Mie sinufaiki na lolote katika hio katiba maana ni kwa vile sifanyi uhalifu wala sijishughulishi na siasa! Siwezi kushabikia wala kupinga mchakato wa katiba mpya ila tu mtu asinishurutishe maana binafsi hainiathiri kwa namna moja ama nyengine maisha yangu ya kawaida tu! Mnaopambania ipambanieni tu.

Wenye maslahi ni wanasiasa na wahalifu maana ndio ina vipengele vya kuwatetea na kuwaneemesha kwahio lazma wawe na moto nayo! Sasa jiulize makundi haya mawili ni watanzania wote million 60?

Katiba Iliyopo ina mwathiri sana mtanzania na hasa yule wa kawaida. Baadhi ya maeneo husika ni haya hapa:
-------
1. Katiba iliyopo haiwawajibishi baadhi ya watendaji wakuu kwa kuikiuka, na hii ni kwa mujibu wa katiba yenyewe.
2. kwa katiba iliyopo pana watu hata kama wakiiba, wakipora, wakiuwa, wakidhulumu nk hiyo ni halali kwa mujibu wa katiba yenyewe.
3. katiba iliyopo inawapa baadhi ya watu mamlaka ya kujifanyia lolote bila kuhojiwa au hata kuwajibishwa tu.
4. Katiba iliyopo haitoi haki sawa kwa watu wote ndani ya nchi.
5. Kuna mianya mingi katika katiba hii ambayo inaweza kuifanya mihimili mingine hata kupoteza uhuru wake wa kiutendaji kwa mujibu wa katiba yenyewe.
6. Kuna utitiri wa nafasi za uongozi wasio na tija wala ridhaa ya wananchi ambao pia ni mzigo mkubwa kwa mlipa kodi.
7. Kuna utitiri wa vigogo wenye mapato yasiyoakisi tija, wala kuwa na ridhaa ya wananchi na wasiolipa kodi wanaopata uhalali kwenye katiba hii.
8. Kwa katiba hii polisi wanaweza mshikilia mtu kwa kumbambikizia kesi hata kwa miaka kadhaa. Mhanga akaja kuachiliwa bila ya wahusika kuwajibika kwa lolote. Hili likihalalishwa na katiba hii.
9. Nk, nk.
-----------

Mkuu,

(a) wewe hulipi kodi?
(b) Wewe hubambikiziwi kesi au hujabambikiziwa kesi hata barabarani?
(c) Kama hauko sawa na wengine mbele za sheria wewe haikupi taabu?
(d) Kama walinzi wako wakuu wa haki zako hawawajibishwi na katiba, kuona haki zako ziko salama, wewe haikuhusu?
(e) unapokuwa na viongozi waovu usio na ridhaa nao wewe haikuhusu?
(f) unapokuwa na viongozi wasio na tija wewe haikuhusu?
(g) ukiibiwa au ukadhulumiwa, wewe haikuhusu?
(h) mihimili ya utawala inapokuwa haiko huru, wewe haikuhusu?
(I) nk, nk

Wewe hunufaiki na katiba mpya ila wasiasa na wahalifu? Seriously?!

Lakini labda tuanzie hapo mkuu?

NB:

(i) hakuna anayetafuta tuzo kwenye hili.
(ii) hakuna anayekulazimisha wewe au mtu yeyote kuwa sehemu ya jitihada hizi usizoona wewe umuhimu wa kuziunga mkono au kutoziunga mkono.
(iii) Japo inafahamika pana opportunists pia ambao hupenda kukaa mkao wa mafanikio tu. Yaani upande wa mlo tu. Wao huwa ni marafiki wa Mungu na Shetani at the same time.

Aghalabu kwenye mpambano huwa neutral kuchagua upande wa ushindi baada ya vita.

Au nasema uongo ndugu zangu akina joka kuu Yoda BAK johnthebaptist na wazalendo wenzangu?
 
Mnaacha kujenga chama chenu kilicho poteza uaminifu kwa wananchi mnaanza kuhangaika na katiba na mnajua kabisa kwa hii miaka 4 iliyobaki hilo jambo la katiba mpya haliwezekani

Kwa lugha nyepesi isipopatika katiba mpya katika hii miaka 4 iliyobaki na CHADEMA ndio imekufa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnaacha kujenga chama chenu kilicho poteza uaminifu kwa wananchi mnaanza kuhangaika na katiba na mnajua kabisa kwa hii miaka 4 iliyobaki hilo jambo la katiba mpya haliwezekani

Kwa lugha nyepesi isipopatika katiba mpya katika hii miaka 4 iliyobaki na CHADEMA ndio imekufa

Sent using Jamii Forums mobile app

Chama kipi unaongelea mkuu? Vyama vyote kasoro CCM vinahitaji katiba mpya? Wananchi wote kasoro ya wasiojitambua wanahitaji katiba mpya? Mwananchi wa kawaida? Comment #9 hapo juu haikuhusu?

IMG_20210702_105324_920.jpg


Penye nia ipo njia. Njia ya kuelekea mafanikio haijawahi kuwa rahisi.

Wewe uko kundi lipi lisilohitaji katiba mpya mkuu?
 
Katiba ya sasa ni mbovu na bado haiheshimiwi, hofu kubwa ya CCM ni kuweka mazangira sawa ya kisiasa ambayo yanaweza kuwatoa madarakani

CCM hawana incentive yoyote kuridhia katiba mpya. Wana kila kitu cha kupoteza kwa kuwapo kwa katiba mpya.

Bila kuwalazimisha kikamilifu katu hawatauridhia mchakato huu.
 
Tujikite na wenye issue ya uelewa acha akina Magonjwa Mtambuka wabakie na m@vi yao:

Kabisa asee
 
Mnaacha kujenga chama chenu kilicho poteza uaminifu kwa wananchi mnaanza kuhangaika na katiba na mnajua kabisa kwa hii miaka 4 iliyobaki hilo jambo la katiba mpya haliwezekani

Kwa lugha nyepesi isipopatika katiba mpya katika hii miaka 4 iliyobaki na CHADEMA ndio imekufa

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu ajenda anayo zungumzia Chadema ni ya watu:

"Katiba ni yetu sisi wananchi. Hatutaki kuendelea kubambikiziwa kesi, hatutaki dhuluma, hatutaki kubebeshwa mizigo ya kodi ya wengine, tunataka mihimili ya utawala iliyo na huru kamili, tunataka usawa, tunataka uwajibikaji, tunataka mawazo yetu kusikilizwa nk."

Wewe hudhani hayo kuwa ni muhimu bila kujali nani anaongoza jitihada za kuyapigania?
 
Katiba Mbovu iliyopo imewadumaza akili, watu kutoa maoni yao wanasingiziwa wametukana kwasababu wanajua mtu anaweza wekwa ndani bila kosa lolote.
 
Wanufaika wa katiba hii mbovu (CCM) ndiyo hawataki kabisa kusikia habari ya katiba mpya.
 
Back
Top Bottom