Wanufaika wa Katiba Iliyopo hawahitaji elimu

Wanufaika wa Katiba Iliyopo hawahitaji elimu

Mnaacha kujenga chama chenu kilicho poteza uaminifu kwa wananchi mnaanza kuhangaika na katiba na mnajua kabisa kwa hii miaka 4 iliyobaki hilo jambo la katiba mpya haliwezekani

Kwa lugha nyepesi isipopatika katiba mpya katika hii miaka 4 iliyobaki na CHADEMA ndio imekufa

Sent using Jamii Forums mobile app
Mmoja wa wanufaika.
Watu wakiongelea katiba nawe ukakimbilia vyama, unatuhakikishia kuwa ni mmoja wa wanufaika.

Tunakupotezea ,, pambana kivyako.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Katiba Iliyopo ina mapungufu mengi yasiyoweza kuvumilika zaidi.

Ni wazi kuwa anayebeza jitihada zozote za kuanzishwa tena kwa mchakato wa kupata katiba mpya kiporo uliobakia, ni kwa sababu tu ya kuwa na uelewa mdogo au ni mnufaika wa moja kwa moja wa katiba mbovu hii iliyopo.

Wanaobeza jitihada hizi wamo katika makundi haya mawili tu wala si vinginevyo.


Kwa wale wasioelewa ni jukumu letu kuwaelimisha wakapate kujua kwa nini katiba mpya ni muhimu sana kwao. Labda pia kwa nini ni muhimu zaidi sasa kuliko wakati mwingine baadaye.

Hatuna haja ya kupoteza muda na wanufaika wa mfumo. Hao wanatumia mbinu na sababu zozote zikiwamo za kijinga kuona kuwa mchakato huo hautapata kurejelewa kwa kadri iwezekanavyo.

Kwa hao ilikuwa ni muda muafaka sasa kuwasusia, zikiwamo shughuli zao, na hata "nyuzi na mabandiko yao yote." Hatuna haja ya kupoteza na muda wala kuwa na marumbano yoyote ya maneno na watu hawa kwa sasa.

Kama mbwai na wajue kabisa imeshakuwa mbwai!

Wanadhani tutasusa tu uchaguzi au hatutaweza kukabiliana nao sawia kuhakikisha katiba mpya inapatikana. Kwa mawili haya, ni wajibu wetu kuona kuwa hayawi faida kwao.

Tupambane kivyetu nao wapambane na hali zao.

Au nasema uongo ndugu zangu?
Imeeandikwa vizuri sana. Leo hii naanza kupanda mbegu kwa watu wanahohitaji elimu ya katiba mpya.
 
Katiba Iliyopo ina mwathiri sana mtanzania na hasa yule wa kawaida. Baadhi ya maeneo husika ni haya hapa:
-------
1. Katiba iliyopo haiwawajibishi baadhi ya watendaji wakuu kwa kuikiuka, na hii ni kwa mujibu wa katiba yenyewe.
2. kwa katiba iliyopo pana watu hata kama wakiiba, wakipora, wakiuwa, wakidhulumu nk hiyo ni halali kwa mujibu wa katiba yenyewe.
3. katiba iliyopo inawapa baadhi ya watu mamlaka ya kujifanyia lolote bila kuhojiwa au hata kuwajibishwa tu.
4. Katiba iliyopo haitoi haki sawa kwa watu wote ndani ya nchi.
5. Kuna mianya mingi katika katiba hii ambayo inaweza kuifanya mihimili mingine hata kupoteza uhuru wake wa kiutendaji kwa mujibu wa katiba yenyewe.
6. Kuna utitiri wa nafasi za uongozi wasio na tija wala ridhaa ya wananchi ambao pia ni mzigo mkubwa kwa mlipa kodi.
7. Kuna utitiri wa vigogo wenye mapato yasiyoakisi tija, wala kuwa na ridhaa ya wananchi na wasiolipa kodi wanaopata uhalali kwenye katiba hii.
8. Kwa katiba hii polisi wanaweza mshikilia mtu kwa kumbambikizia kesi hata kwa miaka kadhaa. Mhanga akaja kuachiliwa bila ya wahusika kuwajibika kwa lolote. Hili likihalalishwa na katiba hii.
9. Nk, nk.
-----------

Mkuu,

(a) wewe hulipi kodi?
(b) Wewe hubambikiziwi kesi au hujabambikiziwa kesi hata barabarani?
(c) Kama hauko sawa na wengine mbele za sheria wewe haikupi taabu?
(d) Kama walinzi wako wakuu wa haki zako hawawajibishwi na katiba, kuona haki zako ziko salama, wewe haikuhusu?
(e) unapokuwa na viongozi waovu usio na ridhaa nao wewe haikuhusu?
(f) unapokuwa na viongozi wasio na tija wewe haikuhusu?
(g) ukiibiwa au ukadhulumiwa, wewe haikuhusu?
(h) mihimili ya utawala inapokuwa haiko huru, wewe haikuhusu?
(I) nk, nk

Wewe hunufaiki na katiba mpya ila wasiasa na wahalifu? Seriously?!

Lakini labda tuanzie hapo mkuu?

NB:

(i) hakuna anayetafuta tuzo kwenye hili.
(ii) hakuna anayekulazimisha wewe au mtu yeyote kuwa sehemu ya jitihada hizi usizoona wewe umuhimu wa kuziunga mkono au kutoziunga mkono.
(iii) Japo inafahamika pana opportunists pia ambao hupenda kukaa mkao wa mafanikio tu. Yaani upande wa mlo tu. Wao huwa ni marafiki wa Mungu na Shetani at the same time.

Aghalabu kwenye mpambano huwa neutral kuchagua upande wa ushindi baada ya vita.

Au nasema uongo ndugu zangu akina joka kuu Yoda BAK johnthebaptist na wazalendo wenzangu?
Achana naye huyo hao Ni katika watu wenye uelewa na anafaidika na mfumo uliopo in one way or another. How come a university graduate even from jalalani doesn't know the part that a good law plays in individuals and communities?
 
Achana naye huyo hao Ni katika watu wenye uelewa na anafaidika na mfumo uliopo in one way or another. How come a university graduate even from jalalani doesn't know the part that a good law plays in individuals and communities?

Hatimaye tulielewana hadi nikaandika uzi juu yake:

IMG_20210703_151942_647.jpg


Tuzikate tamaa kuwaelimisha wenye matatizo ya uelewa wa dhati.

Angalia ushuhuda huu:

 
Back
Top Bottom