Wanyakyusa hawawezi kutamka herufi "L"?

Benokolongokonongose

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2012
Posts
213
Reaction score
52
Za jioni wakuu. Tumetoka kuangalia video ya Bahati Bukuku na tumeangalia pia ya Bon Mwaitege. Nilichojifunza kwao na kwa wanyakyusa wote hawawezi kutamka vema heru L ambapo kila wakitaka kutamka herufi hii lazima watasema R. Mfano LEO watasema REO. MBELE-MBERE. Sasa naomba kuuliza mbona herufi L wanaishindwa?Wenu, Benokolongokonongose.
 
Daah inawezekana kukawa na ukweli coz me mnyakyusa na izo herufi izo mbili zinanisumbua kweli bt nimezaliwa dar na nimekulia dar
 
Hii nayo ni thread?put it in dustbin mods
 
mbona na wewe huwezi kuandika vizuri; ref, heading yako
 
Sio r wanasema l kuna mtu nafanya nae kazi ni mnyakusa rim anasema lim
 
Mhhh! hakuna ukweli wanyakyusa hatuna r kabisa. Hao wanapamba tu sisi kwenye r tunaweka l na kweny l inabaki l
 
mari3mari upo sahihi wanyakyusa hawana R kama wachaga na wakurya vile hawana L.
mleta maada kachanganya madawa ,wanyakyusa kwenye R mara nyingi wanaweka L ndio maana na jina la KYELA linaukweli wa kukosa R, Arusha imekosa L.
 
Nyie hamjawasikia vema. Wasikilizeni kwa makini mtagundua. L ni R ni L. Bukuku katika ajabu shangaza BWANA anaimba AtakubaLIki Reo.
 

labda wamasai
 
Unadanganyaa
 

Usirudie kuongopa,
httpp://nyakyusa.com/nod/nya_striveregler.php
 

Heru!!!!!!ni kitu gani hicho!!!!!!!!!!
 
Wanyakyusa wanatumia L hawana R, hutaikuta popote katika maandishi au majina ya asili ya wanyakusa. sina hakika katika kutamka ila nijuavyo mimi wanyakyusa hawaezi matumizi ya R. Rehema wanatamka lehema n.k
 
Uko sahihi kabisa.
Katika kila kabila kuna herufi ambayo inakua shida kwao.
Mfano; Wanyakyusa R inatumika badala ya L (waliketi-wariketi)
Wachaga S inatumika badala ya Z (Maziwa-Masiwa)
Wamakonde wana N badala ya M (Mjomba-njomba)
Wamasai S badala ya Z
So ni makabila mengi na hii utapata kufahamu zaidi ukikutana na mtu aliyeishi huko kwa muda mrefu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…