Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja

Hahahhahaha inaonyehs una uelewa mdogo sana wa Katina ya JMT ya mwaka 1977 na katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.kazisome upya hizo katiba na utaona jinsi gani ulivyovurunda na kuizikanganya katiba kwa lengo la kupotosha watu.
Hivi Nauliza kwani wa ZNZ pekee yao ndiyo wasiopenda Muungano?
 
Pasco bana,yaani huyuhuyu aliyesimamia uchaguzi na kuamua alivyotaka ndo asimamie hiyo kura?hata wakikataa atasema wamekubali.
 
Tunaongea sana ila katika duania hakuna taifa linalojitambua linaruhusu kataifa kadogo kujiuendesha karibu na mipaka yake. Ndo yaliyopo Macao, Taiwan, Hong Kong, Gilblatar, hata visiwa vingi vidogo vinavyo zunguka Marekani, UK, Uholanzi, Ufaransa, Uturuki, Urusi, n.k.

Kwa maana moja hata nyingine, huwa watawala hawako radhi kuachia maeneo kama haya. Sisi tunalalamika ila itabaki hivyo.

 
Acha kumshambulia bwana Pasco.ameeleza ukweli tukitaka kuliamua hili suala iitishwe kura ya maoni mbona ni simple tu.tena kura yenyewe ipigwe nchi nzima si Zanzibar pekeyake.
 
Mkuu Baraghash naomba kukuunga mkono, wakati wote mimi huamini kuwa adui wa wazanzibari ni CCM tu. Mambo yote na maamuzi yote ya kisiasa ndani ya Zanzibar hufanyika Dodoma, kwa hiyo hakuna haja ya wazanzibari kuwachukia wala kuwakasirikia wamrima. Adui yenu CCM, siku mkiweza kuwaondoa na maninja wao basi mtakuwa mmeshinda.
 
Acha kumshambulia bwana Pasco.ameeleza ukweli tukitaka kuliamua hili suala iitishwe kura ya maoni mbona ni simple tu.tena kura yenyewe ipigwe nchi nzima si Zanzibar pekeyake.
Usiwafanye wenzenu wajinga, Kura tupige sote mkoloni na mkoloniwa, umeoana wapi? Mbona mulipopiga kura ya kujitawala Tanganyika mlipiga peke yenu na mkoloni akawa msimamiaji tu
 
Hivyo visiwa kwa ridhaa yao vingi vinajitawala, na vingine kwa mapenzi yake vimeamua kuwa chini ya tawala hizo, siyo kwa hila, vitisho, mauaji na ukandamizaji kama huu wa akina Jecha na CCM yenu
 
Hiyo Zanzibar unayoongelea ni Muunganiko wa Pemba na Unguja, nao wanahitaji kura ya maoni kubaki kuwa Zanzibar au kila kisiwa kijiamulie mambo yake
Zanzibar tafsiri yake ni Unguja, Pemba,Mombasa, Mafia na kisiwa cha Latham.
Mombasa tumeiuza kwa Kenya. Mafia na Latham vimeporwa kwa mabavu na bara. Ikiwa jina la Zanzibar linakutia kichechefu, basi kura ya maoni hiyo iishie Mafia,sio unguja na Pemba tu
 
Unalijua Taifa linalojitambua au kutambulika Hivi wewe umo?Zanzibar ilianza kujitambua na kutambulika duniani kabla ya Tanganyika. Nchi ya kwanza kuwa na uhusiano wa kibalozi na USA barani Afrika ni Zanzibar.Tanganyika wakati huo inaitwa MRIMA
 
Mkuu Pasco hilo ni wazo zuri tu na lenye manufaa zaidi kwa upande wa Zanzibar.

Hapa kuna mambo mawili ya msingi, kwanza Uingereza kama tunavyofahamu ni muungano wa England, Wales, Northern Ireland na Scotland.

Pili, alie na mamlaka ya kuamua iwepo kura ya maoni ni waziri mkuu wa Uingereza ambae ni David Cameron.

Aliekuwa waziri wa nchi wa Scotland (first minister) katika serikali ya UK na anaeiwakilisha Scotland kwenye bunge la UK (house of Commons bwana Alex Salmond ndie alieitisha kura ya maoni ya Scotland kujitenga kutoka UK mwaka 2014, na hiyo ni baada ya kuomba ruhusa kutoka kwa David Cameron ambae ni waziri mkuu wa UK.

Alex Salmond akiwa kiongozi wa chana cha SNP alikuwa na "ambition" ya kuona Scotland inakuwa nchi huru bila kufuata nyuma na kuitikia kila kitu kutoka serikali ya UK.

Hali kadhalika David Cameron nae akiwa waziri mkuu wa Uingereza akatoa ahadi iliyokuwepo kwenye manifesto ya kampeni ya uchaguzi wa mwaka 2015 kwamba angeitisha kura ya maoni mwaka 2016.

Lakini kiufundi ni kwamba ni David Cameron ambae amefanikisha kura za maoni ile ya Scotland na hii ya UK kujitoa kwenye umoja wa Ulaya EU ndie mwenye mamlaka ya kuitisha au kuidhinisha hizi kura za maoni akiwa waziri mkuu wa UK.

Na hata sasa waziri wa nchi wa Scotland mama Nicola Sturgeon anaandaa utaratibu wa kuomba ruhusa kutoka kwa David Cameron ili awezeshe Sctoland kupiga kura ingine ya maoni ya kutaka kujitoa kutoka Uk maana wa-scotish wanaamini kwamba wameamuliwa maamuzi ya kutoka kwenye EU bila ya wao kupenda na wangependa kuendelea kuwa wanachama wa EU wakiwa nchi huru.

Hivyo basi tukiangalia hali hiyo ya wazungu hawa na utaratibu wao waliojipangia, mimi naona itakuwa ni vigumu sana kwa Zanzibar kupiga kura ya maoni ya kutaka kujitoa kwenye Muungano na Tanzania Bara.

Hiyo ni kwasababu kuu mbili.

Kwanza, ni lazima uamuzi huo ufanywe kwa makubaliano ya raisi wa Zanzibar na raisi wa JMT na baada ya hapo suala hilo lijadiliwe na Bunge la JMT kukubalina na wazo hilo.

Hii ni tofauti na kura za maoni kama ile ya ZUK ambayo ilihusu masuala mengine kabisa.

Pili, bado katiba ya sasa haijaweka mazingira mazuri kwa Zanzibar kuweza kujiamulia kufanya kura ya maoni.

Na hata kama katiba itabadilishwa, bado haitaboresha hicho kipengele cha kuipa nafasi Zanzibar kujiamulia mambo yake yenyewe.

Hitimisho langu ni kwamba suala la Zanzibar ni gumu sana na kama hakuna tume huru ya uchaguzi kama wenzetu wa Uingereza ambao wana uhakika wa matokeo tusitegemee jipya.

Tume za uchaguzi za kiafrika zinaendeshwa kwa mtindo wa kiafrika na demokrasia ya kiafrika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…