#COVID19 Waoga wa Sindano: Mikakati gani tutumie kuchanjwa?

#COVID19 Waoga wa Sindano: Mikakati gani tutumie kuchanjwa?

TheChoji

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2009
Posts
5,771
Reaction score
17,849
Niseme tu mimi binafsi sina tatizo lolote na chanjo. Yaani kama ingekua sio huu uoga uliopitiliza wa sindano, mimi ningekua kati ya watu wa mwanzo kabisa kuchanjwa! Lakini mpaka leo bado nambwelambwela kwenda kuchanjwa kisa tu naogopa ile sindano. Kama mliona ile video ya mwanajeshi aliepelekwa kuchanjwa na kundi la wenzake kama 9 wamemshikilia na bado akawaponyoka na kukimbia, basi huyo ni mimi kabisaa..!!🤣

Sasa naomba kuuliza kwa wale ambao mmeshachanjwa hebu tupeni uzoefu hapa, je inauma? Au ni chwaaa... Imeisha iyo! Hapa nilipo sijawahi kuchoma chanjo yoyote pamoja na kuletewa chanjo izo bure kabisa kisa ni uoga.

Najua tupo wengi kwenye hili kundi japo mwenzetu mmoja ambae ni mkuu wa wilaya yeye tayari. Hebu tupeane akili hapa jinsi ya kuovercome huu uoga au mbinu gani tutumie?

Mwisho naiomba serikali iangalie uwezekano wa kutuletea chanjo za vidonge ione jinsi watu watakavyofurika kuchanja. Zikipatikana za kupaka pia itasaidia sana. Ieleweke uoga wa sindano ni "phobia" kama ilivyo uoga wa nyoka, tandu, vinyonga, nge, heights nk.
 
Mkibanwa sana woga mtauweka kando.
Opportunity Cost
Ukijiona huwezi kusafiri, kujumuika na kupata huduma za kijamii utachagua Moja, kufa mapema kwa sononi au kuchanjwa
 
Inauma wakati wa kuingia ila sio kiviilee..baada ya hapo akisha press dawa mambo mukide! Ni kitendo cha dakika tu mkuu..!
 
Sindano sijawah izoea kabisa!
Ila kwenye chanjo inabidi kujikaza hivyo hivyo, na sidhan kama itachukua zaidi ya dk 2
 
Inauma wakati wa kuingia ila sio kiviilee..baada ya hapo akisha press dawa mambo mukide! Ni kitendo cha dakika tu mkuu..!
Waachaa..! Kumbe tunaogopa bure tuu? 😁
 
Sindano sijawah izoea kabisa!
Ila kwenye chanjo inabidi kujikaza hivyo hivyo, na sidhan kama itachukua zaidi ya dk 2

Ishu ni pale mwanzo unapomuona daktari anakuja na kale ka chupa, anatikisa tikisa, anakufuta na pamba...! Yaani hicho kitendo utaona kama ni saa nzima imepita 😀 mpaka hapo unakua umeshasali sala zote ndani ya hizo sekunde chache..
 
Nasubiri za vidonge kwa kwel maana sindano daa

Yani mpaka nawaza siku nikienda kuchanja niombe wanichome sindano ya ganzi kwanza ndio wanichanje 🙄 ila sasa hata iyo sindano ya ganzi nayo sijui watanichomaje. Akili matope kabisa hizi!
 
Niseme tu mimi binafsi sina tatizo lolote na chanjo. Yaani kama ingekua sio huu uoga uliopitiliza wa sindano, mimi ningekua kati ya watu wa mwanzo kabisa kuchanjwa! Lakini mpaka leo bado nambwelambwela kwenda kuchanjwa kisa tu naogopa ile sindano. Kama mliona ile video ya mwanajeshi aliepelekwa kuchanjwa na kundi la wenzake kama 9 wamemshikilia na bado akawaponyoka na kukimbia, basi huyo ni mimi kabisaa..!!🤣

Sasa naomba kuuliza kwa wale ambao mmeshachanjwa hebu tupeni uzoefu hapa, je inauma? Au ni chwaaa... Imeisha iyo! Hapa nilipo sijawahi kuchoma chanjo yoyote pamoja na kuletewa chanjo izo bure kabisa kisa ni uoga. Najua tupo wengi kwenye hili kundi japo mwenzetu mmoja ambae ni mkuu wa wilaya yeye tayari. Hebu tupeane akili hapa jinsi ya kuovercome huu uoga au mbinu gani tutumie?

Mwisho naiomba serikali iangalie uwezekano wa kutuletea chanjo za vidonge ione jinsi watu watakavyofurika kuchanja. Zikipatikana za kupaka pia itasaidia sana. Ieleweke uoga wa sindano ni "phobia" kama ilivyo uoga wa nyoka, tandu, vinyonga, nge, heights nk.

Kuna bwana mmoja hatunaye aliwahi kusema: "bakini na m@vi yenu." Nadhani alikuwa na hoja.
 
Yani mpaka nawaza siku nikienda kuchanja niombe wanichome sindano ya ganzi kwanza ndio wanichanje 🙄 ila sasa hata iyo sindano ya ganzi nayo sijui watanichomaje. Akili matope kabisa hizi!
Hatari, kwel mimi pia natamani chanjo lkn ya vidonge nilisikia israel wameshaitengeneza
 
Yani mpaka nawaza siku nikienda kuchanja niombe wanichome sindano ya ganzi kwanza ndio wanichanje 🙄 ila sasa hata iyo sindano ya ganzi nayo sijui watanichomaje. Akili matope kabisa hizi!
🤣🤣🤣 Acha tu yaani, sijui kwanini hawajatengeneza ganzi ya kunywa hao nao
 
Inasemekana hata yule muhishimiwa anayejifanya kuipinga shida ni uoga wa sindano tu!
 
Nilishawahi pata ajari mbaya sana. Jeraha ilitaliwa lishonwe na nichomwe sindani ya ganzi.......hahaaaa nilisema nipeni vidonge vya maumivu vinatosha.

Nilipona na sasa niko sawa kabisa. Sindano mara yangu ya mwisho kuchomwa ilikua 1999
 
Back
Top Bottom