Mjasiri na Mali
JF-Expert Member
- Jun 24, 2017
- 5,366
- 14,167
Habari za wakati huu,
Sijui wapi pa kuanzia Ila tangia mwaka 2018 niliamua kuacha kazi na kuanza maisha ya kujiajiri.
Kazi niliacha baada ya kuona biashara zangu zingine ndogo ndogo zinalipa Ila changamoto ilikuwa ni kukosa usimamizi nzuri.
Pia sababu nyingine ilikuwa kutoelewana na supervisor wangu kutokana na roho ya kijicho kuona maendeleo niliyokuwa nayo hayaendani na mshahara ninaopata.ingawaje sikuwahi kuwa na loss yoyote au kujibizana naye Ila alichokuwa anafanya kunipiga Vita ya chinichini.kwanza mmiliki wa kampuni alikuwa ni mwenyeji wa Kanda ya ziwa hivyo kufanya asilimia kubwa ya wafanyakazi kuwa watu wa Kanda ya ziwa.
Pili kwenye vitengo vyote waliweka watu wa Kanda ya ziwa. Mimi peke yangu ndio nilikuwa mtu wa kaskazini.hii ilipelekea supervisor wangu kutengeneza na kueneza sumu ya chuki kwa urahisi kuwa watu wa kaskazini ni wezi .turudi kwenye mada
Baada ya kuacha kazi mambo yalinyooka kuliko mwanzoni.niliwaza muda wote nilikuwa wapi kwanini sikuingia mapema kwenye biashara.Ndani ya miaka mitatu nilifanikiwa kupata sehemu ya kujihifadhi na kausafiri kutokana na wakati mwingine Mishe zangu zilikuwa za udalali.
Mwishoni wa mwaka 2022 mambo yalianza kwenda mrama baada ya kuhamia kwenye kibanda changu.Mama yangu mzazi alikuwa akiumwa kifundo Cha mguu na pilingili mbili za mgongo zilikatika pia na sukari ilikuwa ikimsumbua.Hivyo ilibidi aje dar as salaam kwa ajili ya tiba
Tulipambana naye kwa wakorea pale mbezi kwa msuguri ikashindikana tukahamia mhimbili huko nako hakukuwa na nafuu ya kudumu.wakati huo nilikuwa na mtoto mdogo ambaye alikuwa Hali chakula Wala usiku halali.Lakini changamoto haikushia hapo kwenye maisha ya nyumbani.usiku kulikuwa hakuna kulala Mara watu wanagonga mlango wengine wanafagia nje .ukichungulia nje huoni mtu yoyote .hili nilimaliza kwa njia maombi
Changamoto hizi hazikuishia nyumbani tu Bali hata sehemu zangu za kutafuta ridhki.nilikuwa na ofisi mbili moja ya uwakala nyingine ya duka la vinywaji vya jumla na rejareja.Pesa nyingine nilikuwa nazungushia kwenye udalali.
Siku isiyokuwa na jina naenda kufunga hesabu kwenye ofisi ya uwakala mambo hayakuwa mazuri.Wakala hakuwa na cash yoyote wa float.pesa iliyokuwepo ilikuwa ni kamisheni jumla yake Kama laki tatu na machenchi.kuulizia pesa nyingine nikaambiwa iko kwa wakala mwenzake.basi pale tukagawana faida nikaondoka.kufupisha stori Yule wakala alikuja akasema pesa ametapeliwa hivyo atanilipa mdogo mdogo.
Wakati huo nimeshauza gari la kutembelea ili ninunue guta.kumbe guta limeuzwa Mara mbili na Mimi ndiye mtu wa pili .kufupisha guta sikupata niliishia kulipwa mdogo mdogo.
Duka la vinywaji Mambo hayakuwa mazuri nilichezea vitasa Sana kwa TRA kutokana na mambo ya risiti .mbaya zaidi madeni yalikuwa mengi kwenye mabar na mapub .kuna meneja alifukuzwa kazi ,Kuna miliki alishindwa kulipa Kodi ya mwaka mzima Kama mwenye nyumba anavyotaka.
Kifupi ndani ya mwezi wa 11 mwaka 2022 maji yalifika shingoni ikabidi niende nyumbani Kilimanjaro kupumzisha akili.huku nikiwa siamini ni nini kilichonitokea.hatimaye Kodi ya duka iliisha duka nikarudisha kwa mwenye nalo.nikauza vitu vyote vya dukani pia asilimia kubwa niliuzia members wa if.
Tokea hapo maisha yakawa ni kuunga unga mjini kwa kutumia uzoefu .Naishi kwa kulipwa madeni na kuongeza madeni mapya .nikajaribu kutafuta kazi mtaani na humu jf Lakini sikufanikiwa mpaka Sasa bado mambo yamekuwa magumu.
Kusudi la kuandika haya yote wakuu kwa Sasa nimekosa rafiki au hata mtu wa karibu wa kuzungumza naye magumu ninayopitia.mke amerudi kwao amechoka kukaa na mtu anayeishi maisha ya kubahatisha .Nimeamini wakati wa magumu hata wapendwa wako wa karibu wanajitenga na wewe
Wakuu najiona kama nafika mwisho na siku zangu zinahesabika kwa sababu nimebaki na mama yangu na mtoto wangu mdogo.wote wananitazama Mimi Lakini kiukweli jaribu limekuwa kubwa kuliko uwezo wangu.madukani madeni yamefika mwisho.
Wakati mwingine huwa napiga saidia fundi ikipatikana maisha yanaenda japo nakuwa slow kutokana sio mzoefu na hizo Kazi.Pia Nina diploma ya mechanical engineering na leseni class d ,e na c1,c2 na c3 Ila leseni kwa Sasa leseni ni ya kurenew
Napatikana kibaha kwa Mathias wakuu .mwenye ajira yoyote ya halali naomba anishike mkono
Sijui wapi pa kuanzia Ila tangia mwaka 2018 niliamua kuacha kazi na kuanza maisha ya kujiajiri.
Kazi niliacha baada ya kuona biashara zangu zingine ndogo ndogo zinalipa Ila changamoto ilikuwa ni kukosa usimamizi nzuri.
Pia sababu nyingine ilikuwa kutoelewana na supervisor wangu kutokana na roho ya kijicho kuona maendeleo niliyokuwa nayo hayaendani na mshahara ninaopata.ingawaje sikuwahi kuwa na loss yoyote au kujibizana naye Ila alichokuwa anafanya kunipiga Vita ya chinichini.kwanza mmiliki wa kampuni alikuwa ni mwenyeji wa Kanda ya ziwa hivyo kufanya asilimia kubwa ya wafanyakazi kuwa watu wa Kanda ya ziwa.
Pili kwenye vitengo vyote waliweka watu wa Kanda ya ziwa. Mimi peke yangu ndio nilikuwa mtu wa kaskazini.hii ilipelekea supervisor wangu kutengeneza na kueneza sumu ya chuki kwa urahisi kuwa watu wa kaskazini ni wezi .turudi kwenye mada
Baada ya kuacha kazi mambo yalinyooka kuliko mwanzoni.niliwaza muda wote nilikuwa wapi kwanini sikuingia mapema kwenye biashara.Ndani ya miaka mitatu nilifanikiwa kupata sehemu ya kujihifadhi na kausafiri kutokana na wakati mwingine Mishe zangu zilikuwa za udalali.
Mwishoni wa mwaka 2022 mambo yalianza kwenda mrama baada ya kuhamia kwenye kibanda changu.Mama yangu mzazi alikuwa akiumwa kifundo Cha mguu na pilingili mbili za mgongo zilikatika pia na sukari ilikuwa ikimsumbua.Hivyo ilibidi aje dar as salaam kwa ajili ya tiba
Tulipambana naye kwa wakorea pale mbezi kwa msuguri ikashindikana tukahamia mhimbili huko nako hakukuwa na nafuu ya kudumu.wakati huo nilikuwa na mtoto mdogo ambaye alikuwa Hali chakula Wala usiku halali.Lakini changamoto haikushia hapo kwenye maisha ya nyumbani.usiku kulikuwa hakuna kulala Mara watu wanagonga mlango wengine wanafagia nje .ukichungulia nje huoni mtu yoyote .hili nilimaliza kwa njia maombi
Changamoto hizi hazikuishia nyumbani tu Bali hata sehemu zangu za kutafuta ridhki.nilikuwa na ofisi mbili moja ya uwakala nyingine ya duka la vinywaji vya jumla na rejareja.Pesa nyingine nilikuwa nazungushia kwenye udalali.
Siku isiyokuwa na jina naenda kufunga hesabu kwenye ofisi ya uwakala mambo hayakuwa mazuri.Wakala hakuwa na cash yoyote wa float.pesa iliyokuwepo ilikuwa ni kamisheni jumla yake Kama laki tatu na machenchi.kuulizia pesa nyingine nikaambiwa iko kwa wakala mwenzake.basi pale tukagawana faida nikaondoka.kufupisha stori Yule wakala alikuja akasema pesa ametapeliwa hivyo atanilipa mdogo mdogo.
Wakati huo nimeshauza gari la kutembelea ili ninunue guta.kumbe guta limeuzwa Mara mbili na Mimi ndiye mtu wa pili .kufupisha guta sikupata niliishia kulipwa mdogo mdogo.
Duka la vinywaji Mambo hayakuwa mazuri nilichezea vitasa Sana kwa TRA kutokana na mambo ya risiti .mbaya zaidi madeni yalikuwa mengi kwenye mabar na mapub .kuna meneja alifukuzwa kazi ,Kuna miliki alishindwa kulipa Kodi ya mwaka mzima Kama mwenye nyumba anavyotaka.
Kifupi ndani ya mwezi wa 11 mwaka 2022 maji yalifika shingoni ikabidi niende nyumbani Kilimanjaro kupumzisha akili.huku nikiwa siamini ni nini kilichonitokea.hatimaye Kodi ya duka iliisha duka nikarudisha kwa mwenye nalo.nikauza vitu vyote vya dukani pia asilimia kubwa niliuzia members wa if.
Tokea hapo maisha yakawa ni kuunga unga mjini kwa kutumia uzoefu .Naishi kwa kulipwa madeni na kuongeza madeni mapya .nikajaribu kutafuta kazi mtaani na humu jf Lakini sikufanikiwa mpaka Sasa bado mambo yamekuwa magumu.
Kusudi la kuandika haya yote wakuu kwa Sasa nimekosa rafiki au hata mtu wa karibu wa kuzungumza naye magumu ninayopitia.mke amerudi kwao amechoka kukaa na mtu anayeishi maisha ya kubahatisha .Nimeamini wakati wa magumu hata wapendwa wako wa karibu wanajitenga na wewe
Wakuu najiona kama nafika mwisho na siku zangu zinahesabika kwa sababu nimebaki na mama yangu na mtoto wangu mdogo.wote wananitazama Mimi Lakini kiukweli jaribu limekuwa kubwa kuliko uwezo wangu.madukani madeni yamefika mwisho.
Wakati mwingine huwa napiga saidia fundi ikipatikana maisha yanaenda japo nakuwa slow kutokana sio mzoefu na hizo Kazi.Pia Nina diploma ya mechanical engineering na leseni class d ,e na c1,c2 na c3 Ila leseni kwa Sasa leseni ni ya kurenew
Napatikana kibaha kwa Mathias wakuu .mwenye ajira yoyote ya halali naomba anishike mkono