Wapendwa nimfanyaje huyu X husband

Wapendwa nimfanyaje huyu X husband

unajua kaka mi siamini kama kweli huyu mama ndiye mwenye watoto wakubwa hivi alafu anajicontradict kama mtoto. Sasa ukawachukua kwa kujitia unaweza kuwa somesha alafu ukaandika namba za baba ili nini? Wewe huna simu? Au bado unajigonga kwake ile hali umeshabwagwa? Nonsense

Labda mama alimpeleka mtoto kwenye shule expensive akaweka namba ya ex wake kwenye form akitegemea kuwa kwa vile ana uwezo atalipa karo ya mtoto? Labda baba alivyopigiwa simu na kuambiwa anatakiwa alipe karo kiasi fulani akaamua kuifutilia na hiyo nafasi kabisa kwa vile hakushirikishwa tokea mwanzo? Just speculation maana mama hataki kutoa info.

Lakini bado haijaniingia akilini baba awaambie watoto kuwa mama yao ni marehemu halafu bado mama aendelee kumwi entertain baba watoto. What for? Hivi huyo baba watoto angekuwa hana uwezo kifedha bado angeandika namba yake kwenye form? Of course, from the outset alichofanya baba watoto sio kizuri lakini asingeweza kufanya alivyofanya for the sake of it. Lazima kutakuwa na sababu ya kufanya vile.
 
kwanini uliweka namba ya simu ya baba yake, why?????????????????
inaonyesha bado unampenda mumeo
but mumeo hakupendi wewe wala watoto
mwanamke unapoamua kukaa na watoto jiamini, be strong dada
mimi nakushauri simama kivyako na watoto wako.
tafuta shule nyingine sahau hayo.
 
  • Thanks
Reactions: ram
Mtu mmeachana miaka sita sasa. Baba hajui mtoto anakula nini wala anaishije. Afu shuleni unaweka contacts zake ukitegemea nini?

Hivi wanawake mtajiamini lini?

Khaa!
 
Wapendwa, Salaam poleni na majukumu, tatizo langu ni kwamba nimeachana na mume wangu takribani miaka sita sasa, mtoto wangu wa kawnza ndio alimaliza darasa la saba mwaka huu, katika kuhangaika kumtafutia shule ili ajiunge na kidato cha kwanza nilimchukulia fomu Marian Boys ya Bagamoyo.

Kwenye fomu niliandika jina la baba na namba ya simu kwa kutambua kwamba ni baba wa mtoto, alifanya mtihani na akafaulu, tatizo illilonisikitisha sana ni kitendo cha huyu baba mtu pindi alipopigiwa simu ili atambue hilo aliwajibu kwamba, huyo mtoto yupo kwa mama yake mimi hanihusu hiyo nafasi itoelewe kwa mtu mwingine.

Nilipata maelezo hayo baada ya kupiga simu shuleni ili nijue utaratibu unakuaje na kuambiwa nafasi yake ilishatolewa baada ya baba mtu kuwajibu vile. Je baba kama huyu nimfanyaje kwa hili, mtoto amejua na amekosa amani, naombeni ushauri wenu sijawahi kuumia kama nilivyoumia kwa hili.

Asanteni nakaribisha ushauri wenu


Pole mwaya, nilidhani niko peke yangu ila mwenzio siku hizi nina moyo mkuu nilishaacha kuumia sababu ya baba wa mtoto, chochote ninachfanya kwa ajili ya mwanangu naandika details zangu, nilishamuambia asubiri mtoto akikua akafanikiwa amtafute amwambie unajua mimi ni baba yako unatakiwa unijali. so chukulia poa maadamu una uwezo wa kumlea mwanao.
 
pole rafiki wala usifikirie la kumfanya huyo mwanaume cha muhimu angaika dogo aende shule alafu nenda TAMWA waeleze shida yako na pia huyo bwana atafutwe kama hamtaki mtoto aandike kwa maandishi au la sivyo awajibishwe kumsomesha mtoto kwa kumkata fedha kwenye mshahara moja kwa moja na kuingiza kwenye account ya mtoto, kisheria inawezekana fanya hivyo
 
Kwanini uliweka namba yasim bila muktaarifu muhusika?
Na inawezekana kuna walakini katiyako wewe na baba huyo kwa huyo Mtoto na ndo maana ame kana
 
Kweli kila familia inakuwa na matatizo yake. Huyu mwanaume ana mawazo mgando. Kama nimekusoma vizuri ni kuwa limjulisha yote hayo. Umbumbumbu wake ndo unamfanya alipize kisasi kwa mtoto! Angetakiwa angalao ashukuru mungu kwa kupata mtu wa kumsomeshea mwanae. Mimi yalinikuta kama ya kwako angalia hapa https://www.jamiiforums.com/habari-...29-haki-nisaidieni-hapa-huyu-binti-yangu.html Ninachokushauri kwa sasa mtafutie mtoto shule ende. hakikisha kuwa sasa unabeba jukumu la baba na mama. Huna haja tena ya kuandika namba za huyo mumeo wa zamani. Labda anaogopa kulipa ada ya mtoto! Mengine utajipanga. Uhayawani wa mtu mmoja usimkoseshe mtoto haki yake ya msingi ya kupata elimu.
 
pole sana dada ila tafadhali sana kama baba watoto katekeleza watoto usiwahusishe watoto katka malumbano yenu muhimu wewe kuhakikisha watoto wanaendelea na masomo na usiwaambie watoto chochote kibaya ili wamchukie baba yao hayo mengine mwachie mungu,kuhusu kutoa contacts zenu nafikiri hapo sio kweli kidogo kama wewe uliweka contact zako na za baba ya mtoto najua utaratibu wa shule ni kuwasiliana na wazazi wote wawili kabla ya kutchukua maamuzi ya kuiuza nafasi ya mwanao labda kuna kitu kingine beside that ,,,,,
 
pole sana dada ila tafadhali sana kama baba watoto katekeleza watoto usiwahusishe watoto katka malumbano yenu muhimu wewe kuhakikisha watoto wanaendelea na masomo na usiwaambie watoto chochote kibaya ili wamchukie baba yao hayo mengine mwachie mungu,kuhusu kutoa contacts zenu nafikiri hapo sio kweli kidogo kama wewe uliweka contact zako na za baba ya mtoto najua utaratibu wa shule ni kuwasiliana na wazazi wote wawili kabla ya kuchukua maamuzi ya kuiuza nafasi ya mwanao labda kuna kitu kingine beside that ,,,,,
 
ulitakiwa uwasiliane na baba yake kabla hujachukua form kwahiyo kitendo cha kutomshirikisha ndicho kilichomuudhi jaribu kukaa nae namuongee kuhusu mtoto
 
Mwanamke Mpumbavu, huibomoa nyumba yake kwa mikono yake yeye mwenyewe: simaanishi kuwa wewe ni mpumbavu ila wakati mwingine nivizuri kurudi kwenye maadili ya kidini kutatua mambo yetu.

Miaka ya nyuma kidogo kuna lecturer mmoja alimfelisha mtoto wake pale SUA ingawa yule kijana alikuwa na uwezo mzuri tu, kisa wazazi wametengana na wanapendelea kuwa na mama kuliko yeye. Kwa hiyo dada yangu usishangae hayo mambo yapo: remember that mwanaume anaoa ili apate mke, ingawa mwanamke anaolewa ili apate mtoto .....(please don't quote me).
 
Duh hatari kubwa yaani nimejikuta nikikasirika kidogo nivunje keyboard yangu.
 
Back
Top Bottom