Wapi kuna mashamba ya sh 150,000/= mkoani Njombe

Lupembe huko huko kabla haujafika barazani Kata Kona ingia ndani Kuna maeneo mazuri sana bei ni poa kinachonikera mda wote ni baridi na vumbi pia maeneo ya huko karibu mwakani naanza kuvuna parachichi
Lupembe! Nashukuru sana mkuu. Ndilo "jina" nililokuwa nalitafuta. Lilikuwa limenitoka. LUPEMBE!

Nauli ni shilingi ngapi kutokea mjini hadi Lupembe?
 
Mahali yalipo mashamba nayayajua ni kama km 15 toka barabara kuu Njombe to songea..kijiji cha Ngalanga. Ekari sh 500,000 zipo 100. Kuna mto karibu hivyo mwekezaji anaweza tumia mda wote
 
Ukipata mkuu nishtue
 
Acha kukatisha watu tamaa
Mkoa wa pwani tu jirani kabisa na d as salaam hapa ukiwa na laki tano unapata shamba tena heka nzima
Huko unaposema inawezekana kuna maeneo unajifekea tu pori unaendelea na maisha
Miaka ya 2016 huko kisarawe pwani vijijini walikuwa wanataka 10,000 tu unakatiwa heka50 zako za pori unafyeka mwenyew
 
Acha kukatisha watu tamaa
Mkoa wa pwani tu jirani kabisa na d as salaam hapa ukiwa na laki tano unapata shamba tena heka nzima
Huko unaposema inawezekana kuna maeneo unajifekea tu pori unaendelea na maisha
Ninalosema nalielewa atauziwa mashamba ambayo ni mbuga yana udongo mweupe na mfinyanzi ilo shamba inatakiwa ulifanyie rehabilitation si chini ya miaka 3 ili mazao yaanze kukubali na tunavyozungumza ninatoka uko nitaweka picha hapa kama kesho watu waone utofauti wa mashamba ya kilimo na mbuga
 
Asante kwa elimu mkuu, usisahau kutuwekea mapicha
 
Acha kukatisha watu tamaa
Mkoa wa pwani tu jirani kabisa na d as salaam hapa ukiwa na laki tano unapata shamba tena heka nzima
Huko unaposema inawezekana kuna maeneo unajifekea tu pori unaendelea na maisha
Truth is ugly, people what to hear what they what to hear. So goodluck with that.
 
Ndugu ukifanikiwa nakuomba sana unijulishe na mimi tafadhali, huko mbali ndio kuzuri sasa.
Mashamba Lupembe vijiji vya Nyave, Mfiriga, Ikang`asi, Itambo na Madeke yapo kwa bei hizo za 150,000/ mpaka chini ya hapo. Wastani ni 100km toka mjini Njombe mpaka maeneo hayo niliyokutajia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…