Wapi kuna mashamba ya sh 150,000/= mkoani Njombe

Wapi kuna mashamba ya sh 150,000/= mkoani Njombe

Usiseme hivyo mkuu! Penye nia pana njia. Muhimu ni uvumilivu na kuwa na muda wa kutosha "kupeleleza"

Niliambiwa na zaidi ya watu wawili wa Njombe kuwa kuna "mapori" yanayouzwa shilingi laki moja na hamsini vijiji vya mbali. Walioniambia ni watu wa kuaminika, mmoja wao ni "bilionea" wa maparachichi.
Katika kijiji nilipo kule Lupembe, kuna eka zaidi ya 2000 zinauzwa na watu tofauti, mashamba haya nilishiriki kuyapima na kuyanunua, project yetu ya awali ilikuwa miti ya mbao, janga la moto lilikatisha watu tamaa sana wamekimbia na sasa wanauza ardhi kwa wengine.
 
Acha kukatisha watu tamaa
Mkoa wa pwani tu jirani kabisa na d as salaam hapa ukiwa na laki tano unapata shamba tena heka nzima
Huko unaposema inawezekana kuna maeneo unajifekea tu pori unaendelea na maisha
Ukienda vijiji kama Vikumbulu, hadi buku 50 unakatiwa pori, changamoto ya Vikumbulu au Chore au Mloka/Mkamba ni maji, na sasa wamekuja wafugaji holela. Maji ni kikwazo.
 
Lupembe! Nashukuru sana mkuu. Ndilo "jina" nililokuwa nalitafuta. Lilikuwa limenitoka. LUPEMBE!

Nauli ni shilingi ngapi kutokea mjini hadi Lupembe?
Tsh 10,000/ ila ukienda mpaka Ukalawa au Madeke au Ikondo andaa 13,000/
 
Mahali yalipo mashamba nayayajua ni kama km 15 toka barabara kuu Njombe to songea..kijiji cha Ngalanga. Ekari sh 500,000 zipo 100. Kuna mto karibu hivyo mwekezaji anaweza tumia mda wote
Ngalanga sawa, bei imechangamka sana, hata Igawisenga bei iko juu au Mgala bei iko juu sababu ni barabarani
 
Usiseme hivyo mkuu! Penye nia pana njia. Muhimu ni uvumilivu na kuwa na muda wa kutosha "kupeleleza"

Niliambiwa na zaidi ya watu wawili wa Njombe kuwa kuna "mapori" yanayouzwa shilingi laki moja na hamsini vijiji vya mbali. Walioniambia ni watu wa kuaminika, mmoja wao ni "bilionea" wa maparachichi.
Kaka njombe mzima hakuna iyo bei uyo nemes asikudanganye
 
Kaka njombe mzima hakuna iyo bei uyo nemes asikudanganye
Kwasasa Maeneo mengi ya Niombe wilayani huko hata ndani ndani bei ni ghali kutokana na ardhi nyingi kuwa na rutuba nzuri na ya asili, pia potential sana kwa kilimo cha mazao yanayoshika soko kama parachichi, viazi na uwekezaji ktk miti. Kama muhitaji kweli changamkieni maeneo yanayouzwa kwasasa huenda miaka michache ijayo bei zitazidi kupanda. Hukawii kusikia maeneo yana chuma!!!
 
N
Usiseme hivyo mkuu! Penye nia pana njia. Muhimu ni uvumilivu na kuwa na muda wa kutosha "kupeleleza"

Niliambiwa na zaidi ya watu wawili wa Njombe kuwa kuna "mapori" yanayouzwa shilingi laki moja na hamsini vijiji vya mbali. Walioniambia ni watu wa kuaminika, mmoja wao ni "bilionea" wa maparachichi.
Nadhani maeneo ya madeke kama unaenda ifakara kilometa 40 kutoka Njombe
 
Back
Top Bottom