Wapi naweza kupata mkopo niboreshe biashara yangu?

Wapi naweza kupata mkopo niboreshe biashara yangu?

Scaboma

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2018
Posts
335
Reaction score
212
Habari za majukumu wadau,

Mie ni mjasiriamali mdogo wa nafaka, natoa mikoani nazileta mjini nauza kwa jumla, Sina fremu ya kufikishia biashara yangu hivyo nikifika madalali hunidaka na kunidalalia kwa wanaouza kwa jumla nami nageuza zangu shamba. Hii hali nimejikuta kama nawatajirisha madalali waliokaa mjini na kunisubiria wanipangie bei, hivyo nimeona ni bora niwe na fremu zangu za kufikishia mzigo ili niwe nauza taratibu kwa bei nzuri, tatizo linakuja mtaji wangu bado mdogo, nikiziipia fremu nitapunguza mtaji.

Naomba mwenye kujua sehemu nayoweza kupata mkopo wa masharti nafuu, nimejaribu kwenye mabenki na baadhi ya microfinance wanahitaji niwe na fremu ya kuuzia biashara yangu pamoja na mlolongo wa business documents, kitu ambacho kwa Sasa Sina ila nikipangasha fremu lazima nikatie documents zote.

Nina shida ya 10M ili niweze kuboresha biashara yangu iendane na wakati, dhamana yangu ni nyumba ipo Mbezi Beach ina hati ya serikali ya mtaa, naomba mwenye kufahamu sehemu nayoweza kupata mkopo wa masharti nafuu tofauti na bank tujuzane tafadhali.
 
Kama hauna documents ni ngumu kidogo kupata kwenye taasisi za kifedha, mi naona aanza taratibu kuweka akiba, kwani si unataka fremu maana yake hela ya kodi? fremu ya miezi 6 au mwaka kwa biashara yako ina gharimu hicho kiasi 10m?
Nahitaji fremu 2 ili kila moja iwe mbali na mwenzake ili mzigo uondoke kwa Kasi, na pia unapofungua frame kumbuka hapo Kuna leseni ya biashara na Tax clearance, na frame unapoichukua lazima uikarabati kwa kuweka sawa kutokana na biashara utakayoifanya ili iwe mvuto kwa wateja, notahitaji na mizani mikubwa miwili kwa ajili ya kupimia nafaka.
 
Habari za majukumu wadau,

Mie ni mjasiriamali mdogo wa nafaka, natoa mikoani nazileta mjini nauza kwa jumla, Sina fremu ya kufikishia biashara yangu hivyo nikifika madalali hunidaka na kunidalalia kwa wanaouza kwa jumla nami nageuza zangu shamba. Hii hali nimejikuta kama nawatajirisha madalali waliokaa mjini na kunisubiria wanipangie bei, hivyo nimeona ni bora niwe na fremu zangu za kufikishia mzigo ili niwe nauza taratibu kwa bei nzuri, tatizo linakuja mtaji wangu bado mdogo, nikiziipia fremu nitapunguza mtaji.

Naomba mwenye kujua sehemu nayoweza kupata mkopo wa masharti nafuu, nimejaribu kwenye mabenki na baadhi ya microfinance wanahitaji niwe na fremu ya kuuzia biashara yangu pamoja na mlolongo wa business documents, kitu ambacho kwa Sasa Sina ila nikipangasha fremu lazima nikatie documents zote.

Nina shida ya 10M ili niweze kuboresha biashara yangu iendane na wakati, dhamana yangu ni nyumba ipo Mbezi Beach ina hati ya serikali ya mtaa, naomba mwenye kufahamu sehemu nayoweza kupata mkopo wa masharti nafuu tofauti na bank tujuzane tafadhali.
Bank
 
Njoo nikupe fremu bure huku kuna mzunguko mkubwa wa biashara ya nafaka lakini sharti uingize mzigo wa kuanzia tani 10 na nitakuwa muuzaji wako lakni kila kilo nakata sh100. Kinachobaki chako mwenyewe..
 
Mpk unataka mkopo wa 10 million mtaji wako ww bei gani?
 
Back
Top Bottom