Wapi Simba na Yanga walipo achana?

Wapi Simba na Yanga walipo achana?

Nawasalimu wale wote wapenda ukweli na uwazi

Pia napenda kuwakumbusha kila mnapopitia makala hizi basi mfanye ulinganifu na yanayotekea huko kwenye timu zenu.

Siku kadhaa niligusia namna ambavyo SIMBA imekuwa ikiulaghai umma wa mashabiki wake kwa kutumia nguvu ya mitandao, vyombo vya habari, wachambuzi na wadau wengine katika kuwalisha matangopori juu ya uwekezaji hewa uliofanyika, na ninadiriki kusema kuwa hili ni jipu kama majibu mengine.

Leo ni Machi 15, 2021 Gazeti la Championi - Jumatatu limekuja na habari kubwa kwenye ukurasa wa mbele tena kwa maandishi makubwa wakisifu namna ambavyo klabu ya Simba imepiga hatua mbele kwenye mafanikio huku wakiitupa Yanga mbali kwa mujibu wa taarifa zao za kuungaunga.

Tuelewane kuwa hakuna mwanamichezo au mpenda maendeleo aliyetayari kubeza juhudi na jitihada za kuelekea kwenye mafanikio, ila hoja inakuja namna gani maendeleo hayo yatafikiwa.

Sasa kwa pamoja tuanze kupata maelezo na kujiuliza yafuatayo[emoji779][emoji779]

Nakumbuka mara baada ya Mo kuchukua asilimia 49 za uwekezaji kwenye Klabu ya Simba imepita zaidi ya miaka miwili, sasa tuanze kwa kujiuliza tangu amechukua nafasi ya mwekezaji mkubwa kutoka kwa wanachama.

Swali la kujiuliza tangu ameichukua timu hiyo ukitoa udhamini ambao anaufanya kupitia bidhaa zake, Simba wamenufaika vipi kiuchumi?

Atakuja mtu atakuambia Simba wamefungua Mo Arena kule Bunju kitu ambacho ni upotoshaji mkubwa kwa maana uwanja wa Bunju ulikuwepo muda mrefu kabla Mo hajaingia Simba kama mwekezaji tangu enzi ya akina Aveva, Ezekiel Kamwaga ambaye aliwaamasisha wanasimba kwenda kufyeka Uwanja ulikuwepo na nyasi bandia ziliagizwa, alichofanya Mo ni kudandia gari kwa mbele na kuwafikisha standi na yeye kuwa mshindi kwa kazi ya wengine ambao leo hata majina yao hayatajwi.

Ataibuka mwingine atakuambia Simba imeingia hatua ya makundi na kucheza robo fainali katika michuano ya Klabu Bingwa chini ya Mo, ila kabla hajameza mate mwambie Simba sio mara ya kwanza kuingia makundi au kucheza robo fainali, miaka ya 1990 Simba ilicheza fainali ya Kombe la washindi; mwanzoni mwa miaka ya 2000 Simba ilitinga robo ikiwa na wakina Kaseja hivyo hakuna jipya6 ambalo Mo ameongeza zaidi ya ujanjaujanga.

Hoja ya usajili bora ambayo inasemeka ni usanii mtupu juzi tu hapa imetumia zaidi ya Sh. milioni 600 kusajili wachezaji ambao hata mazoezini hawatumiki. Halafu mtu anasema usajili bora...ni ajabu sana.[emoji2377][emoji2377]

]Ishu ya kuchukua ubingwa mara tatu hili sio geni tena hao Yanga ambao ndio wanasemwa kuwa wameachwa na Simba wametoka kuchukua ubingwa huo mara tatu huku Simba wakiteswa na hilo.

Pia takwimu zipo wazi kuwa Yanga ameifunga Simba mara nyingi zaidi, imetwa ubingwa mara nyingi zaidi sasa kusema leo Simba wanapepea ni ulimbukeni wa kiwango cha lami.

Tujiulize ile ahadi aliyoitoa Mo kuwa ataongeza idadi ya wanachama wa Simba imefikia wapi?[emoji3480]

Tuliambiwa Simba imeingia mkataba na Benki ya Equity ili kutoa kadi za uanachama sasa atoke kiongozi yeyote aseme tangu wameingia makubaliano hayo wamepata wanachama wangapi? Nina uhakika hata 10,000 hakuna.

Kusema kuwa Simba wamefanikiwa chini ya Mo ni uwongo wa wazi:

Simba hawajafanikiwa kuongeza vyanzo vya mapato wala kuboresha vile walivyo navyo.

Wameshindwa kuongeza idadi ya wanachama zaidi wameendelea kumnufaisha Mo kwenye bidhaa zake.

Wameshindwa kuweka wazi gawio wanalopata kwa mwaka kutoka kwa Mo kama faida.

Hatima ya Sh. bilioni 20 kama kifungua uchumba cha ushirika wao haijulikani.

Zimezaliwa Simba 5 ndani ya timu moja na kuweka rehani asili ya klabu husika.

Wamepoteza nembo ya asili na kuwa na simba mpya chini ya mdhamini bila wenyewe kujua.

NB Kifupi timu inapoteza uhasili wake na taratibu itakuwa mali ya familia hapo ndipo mabadiliko yatatokea kwa mujibu wa matakwa ya familia..

***** *Tukutane mtoni...
Wewe utakuwa ni kigwangwala wa mabwepande. Wewe ulitaka simba ndani ya miaka miwili iwe sawa na Al ahal? au Tp mazembe? Maendeleo. ni mchakato na kwa simba gari ndiyo imewaka hivyo. Nyie endeleeni kutimua makocha maana hayo ndiyo mnayoyaweza
 
Huu uzi umeandikwa na mtu mkubwa tu huko Yanga. Uzuri mambo ya Simba yapo hadharani. ndani na nje ya uwanja. Yanga ilijaribu kuwalaghai watu wake kuwa wapo vizuri,kilichowapata kiko waaaazi
 
Ni aibu zama hizi kuwa na mtu mwenye fikra hasi na mfu za kuhisi alipoamkia Yanga jana ndo ilipo Simba. Mpira ni mchezo wa wazi sio ule wa chumbani na kila mpenda soka wa kweli akiangalia kinachofanyika uwanjani upande wa Simba na Yanga kuna utofauti mkubwa kama mbingu na ardhi.

Tumeshuhudia kwa miaka kadhaa hapa katikati kabla ya ujio wa Mo simba ilivyokuwa na ilivyo kwa sasa kila kitu kiko dhahiri kuwa Simba ya sasa ilipofika itaihitaji Yanga miaka 20 kupafikia kama wataendelea na utaratibu walionao kwa sasa wa kuendesha timu.

Endeleeni kujilisha upepo ukidhani mko sawa na Simba ya zama hizi wakati mwenzio anajimilikisha uchumi wa soka la Tanganyika ili awe kama Bayern munich Ujeruman; Gormahia Kenya, Al ahyl Misiri, Juventus Italy n.k.

Mwisho japo si kwa umhimu, suala la nani anaimiliki Simba halina mashiko kwa mpenzi wa Simba kikubwa ushundi na mataji vipatikane. Timu zote dunia zinazofanya vizuri zinamilikiwa na mtu mmoja au wachache, na hao ndo wanaonufaika na timu kifedha wengine tuliobaki tunafurahia ushindi basi. Kama Mo anaimiliki Simba wewe mshabiki wa Mtwara, Vyawa, Kasulu n.k unapata hasara gani kama timu inafanya vizuri?

Hebu jitahidi uwe na mawazo mtambuka.
Umemjibu vizuri huyo [emoji196][emoji196] wa kidimbwi.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Katika soka la kisiasa, timu humilikiwa na mtu mmoja mwenye hisa nyingi. Ndiye anayefaidika zaidi na mapata. Wengine wanabaki kufurahia burudani ya mpira!
 
Hakuna shabiki yoyote anaelipwa mshahara na team yake dunian ,mi nashabikia Barcelona na Simba


Malipo ya shabiki ni Furaha na mtakaso wa moyo ambao tunapata pale team inapopata matokeo chanya uwanjan ,,ko nyie yanga endeleen kujivuruga na kutuombea mabaya ila sisi team yetu inajua kutulipa mpaka mnatafuta pa kupumulia
 
Eti wachezaji hawafikii thamani ya millioni 600




Kaangalie makundi kwanza afu mtafute shabiki wa al ahly muulize akukadirie thamani ya wachezaji wa simba yeye kama yeye......

Thamani y mchezaji haina pointi saana ila inategemea na kiwango anachoonyesha katika mechi iliyopo kwa wakati huo

Hata akiwa wa bure lakini mechi ikaisha ana hattrick hakuna atakaeuliza sanasana watamsifia .....
Wee kaa hapo na hilo kopo unaloliita kichwa ukispeculate thamani za wachezaji wakati watu wanaperform vizuri


Utopolo bwana
Uwanja ulikuepo eti yeye kaumalizia....
Sasa ulitaka mo ili aonekane amefanya kitu chake mwnyw ajenge mwingine mpya na wakati kuna wa kuendeleza na kuukarabati umaliziwe tu haraka???

Mtupe basi kiwanja jangwani hapo tulete simba queens muwe mnacheza nao

Umeongea pumb sana hadi nmewaza vibaya huku
 
Hii unaijua mtoa maada
Screenshot_2021-03-16-19-30-12-88_73617a28b0d3e7e6a04848a88f233e6b.jpg
 
Back
Top Bottom