Wapi tunakwama Watanzania mpaka soka letu haliendelei kama wenzetu?


Message sent and derived
 
Mipango! Kila kitu ni mipango.

Nikisema mipango namaanisha kuanzia kwenye malengo ya kimkakati yaani dira, mipango yenyewe ya kufanya hayo malengo yatafsiriwe kuwa uhalisia (mikakati, mipangokazi, sera, falsafa, nk), na utekelezaji na ufuatiliaji wa hiyo mipango.

Je, tunayo malengo mahsusi au tunaenda tu? Jibu ni rahisi sana. Duniani hapajawahi kuwa na mafanikio pasipo mipango. Bahati mbaya sana miongoni mwa vitu wabongo huwa tunakwepa kufanya au tunaona kuwa complications ni "mipango".
 
umemaliza mada na nakuunga mkono.
Wabongo huwa wanapenda kitu kitokee chenyewe bila mipango endelevu.
Utakuta wanamuajiri kocha wanataka mechi yake ya kwanza tu ushindi upatikane,usipopatikana ushindi kocha anaonekana hafai na ajira yake inaota nyasi
 
umemaliza mada na nakuunga mkono.
Wabongo huwa wanapenda kitu kitokee chenyewe bila mipango endelevu.
Utakuta wanamuajiri kocha wanataka mechi yake ya kwanza tu ushindi upatikane,usipopatikana ushindi kocha anaonekana hafai na ajira yake inaota nyasi
Very well said. Vituko ni vingi aisee. Unaajiri kocha, unampa malengo (yasiyo thabiti), unaanza kumpangia wachezaji, kisha asipofikia hayo malengo unamtimua. Noma sana.
 
Ni matatizo sana.
Unamuajiri kocha kutoka nchi za mbali kwa pesa nyingi,anapewa nyumba na gari.
Halafu badala ya kumpa nafasi afanye kazi wanataka kocha afuate ushauri wa washabiki na wafanyakazi wa TFF ambao wao walishindwa kuifanya hiyo kazi.
Very well said. Vituko ni vingi aisee. Unaajiri kocha, unampa malengo (yasiyo thabiti), unaanza kumpangia wachezaji, kisha asipofikia hayo malengo unamtimua. Noma sana.
 
Ni matatizo sana.
Unamuajiri kocha kutoka nchi za mbali kwa pesa nyingi,anapewa nyumba na gari.
Halafu badala ya kumpa nafasi afanye kazi wanataka kocha afuate ushauri wa washabiki na wafanyakazi wa TFF ambao wao walishindwa kuifanya hiyo kazi.
Yap. Hili suala limekuwa donda ndugu sasa. Timu yangu ya Simba kwa mfano, walikosana na Uchebe kwa kuanza kumlazimisha wachezaji flani kucheza. Ulipokuja usajili kapewa mchezaji mmoja tu Kahata miongoni mwa aliowataka. Wengine wote utashi wa "bodi". Kafanya vibaya wakamtimua.

Kaja kocha mwingine naye analazimishwa kucheza na straiker wawili ilimradi tu kipenzi cha mashabiki apate namba. Soon utasikia kafungashiwa virago.
 
Kwa mpira mipango inaanzia kwa mkurugenzi wa ufundi.
Aliyepo sasa hivi kateuliwa wakati taratibu zinataka hiyo nafasi itangazwe.
Mbaya zaidi aliteuliwa baada ya kutoka kufanya vibaya akiwa kocha wa timu ya vijana.
 
Mimi nahis bado serikali yetu haijaweka kipaumbele katika michezo kama inavyoweka kweny masuala mengine, na kama kungekua kuna kipaumbele sana katika michezo Tunisia ilikua ni ya kuifunga 2 kwa 0.

Raisi wa TFF na safu yake CCM
Kocha msaidizi CCM
Makocha wa kipa CCM
Wachezaji wanamrengo wa CCM
Viwanja vya mpira CCM
Benchi la ufundi nanuhamasishaji CCM

Kwa mantiki hiii usitegemee nchi kuendelea kisoka.
 
Ni mambo gani serikali imeweka kipao mbele?

Siku makonda alivyo jiingiza kwenye timu ya taifa nikajua hatupo serious kwenye mambo ya msingi! Kwa kifupi mpira wetu unaendeshwa kisiasa!
Tukifungwa tunaanza kuunda kamati za ushindi🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kwa mpira mipango inaanzia kwa mkurugenzi wa ufundi.
Aliyepo sasa hivi kateuliwa wakati taratibu zinataka hiyo nafasi itangazwe.
Mbaya zaidi aliteuliwa baada ya kutoka kufanya vibaya akiwa kocha wa timu ya vijana.
Hiyo ni tosha kuonyesha kuwa hatupo serious kabisaaaaa
 
Kwani TANZANIA imewahi kuendelea kwenye nini ?

Teknolojia ya kisasa ? Ubunifu wa teknolojia ?
Viwanda ? Uvuvi wa kisasa? Mawasiliano ? Ulinzi wa kisasa ?

Huduma za afya ? Maji ?
 
Ni kwl kbsa hata shule mm niliyo soma haina vipaumbele sana kweny michezo wao wanajali tu masomo
Na hapa ndio tatizo lilipoanzia.
Serikali ilitakkwa kukazia sana umuhimu wa michezo mashuleni na shule zote lazima ziwe na viwanja vya michezo yote na pia wapatikane walimu wa michezo husika wenye vigezo.

Tukiweza hapo tatafanikiwa. Lakini sio hii story ya mtu kufuta michezo na wabunge wote wanakubali hapo we took a step 50 years back. Lilikuwa kosa kubwa sana.
 
Tatizo vilevile kuwa tunapenda kutumia njia za mkato, na tunawaamini watu ambao siyo, tunashiriki kwenye ndumba katika kila sekta. Tuache kufanyiana rostoki, akiwa mtu kajaaliwa kipaji zaidi yako basi mkubali siyo unamuendea kwa babu ili apate ngwengwe au goti kujaa maji. Kitu cha mwanzo tuacheni ushirikina, halafu tuwekeze kwenye kabumbu na kuwaandaa vijana, "Perfection is not an accident."
 
Mkuu umenena ukweli mtupu...bt swala la kumeweka mfungaji bora wa ligi tena Mara mbili mfululizo kwenye benchi ni kurisk ajira yako kama kocha.....na hii ni ulimwengu mzima....ukifanya hivyo hakikisha unashinda ukifungwa hakuna atakaye kusamehe...yaani umuweke Messi benchi halafu timu ifungwe useme wasikupangie
 
Mimi nahis bado serikali yetu haijaweka kipaumbele katika michezo kama inavyoweka kweny masuala mengine, na kama kungekua kuna kipaumbele sana katika michezo Tunisia ilikua ni ya kuifunga 2 kwa 0.
Mpaka tuwe na demokrasia ya kweli.
 
Km Yanga kapewa penalty na shabiki wa Yanga anakataa kbsa kwamba faulo ilifanyika nje ya box badala yake ilkua ndani ya box sasa hapo unategemea soka letu likue?
Laizimeni akikosea akaifaidisha Simba sikuhiyo wanasimba wanaona laizimeni hakukosea ila kesho laizimeni huyohuyo akakosea akaibeba yanga wanasimba wote wanalalamika yanga kabebwa. Sisi kusonga mbele sahau. Hadi comoro tuliyekuwa tunajipigia tu sahivi anamvimbia mwarabu(misri)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…