Wapi wanapofanya upasuaji wa kutoa kidole tumbo (appendectomy) kwa bei rahisi?

pharao

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2017
Posts
397
Reaction score
690
Habari wanajamvi,

Nilipatwa na maumivu ya tumbo na wiki iliyopita nilienda moja ya hospitali zilizopo hapa Dar. Baada ya vipimo nikagundulika nina appendicitis.

Baada ya kugundulika, daktari akapendekeza upasuaji ila bei zao ndizo zikanishinda. Nilitakiwa kutoa Shilingi milioni 1 ili kukamilisha operation hiyo.

Na kwa mfuko wangu hiyo pesa ni kubwa hapa nina kiasi cha Shilingi 400,000 tu. Naomba anayejua hospitali Inayoweza kunisaidia kwa kiasi hicho na huduma zao zikawa bora.

Ahsante
 
Maumivu yake huwa ni makuu, Hasa pale ukichelewa huduma
 
Angalia usije kwenda hospital za ajabu wakaona file tofauti wakakukata dushelele
 
Nenda hospitali ya serikali ya wilaya au mkoa wanakata bima kwa sh 10000 hadi 30000 kwa mwaka ambayo itakusaidia wewe kupata matibabu bila gharama za ziada. Pia jubilee insurance wanatoa bima ya familia kwa sh 170000 ambayo ina cover cost mpaka za sh m1 kwa mwaka.
 
Uko wapi?
Nenda kwenye hospitali za Mkoa kwa mfano Mwananyamala, Amana au Temeke utafanyiwa kwa kiasi hicho au chini yake.
Vinginevyo Tandika kuna hospitali inayofanya upasuaji, jina limenitoka.
 
Pole sana mkuu .Ninachokusihi jitahidi sana ujitutumue uende hospitali za uhakika yaan hapo usiangalie sana bei angalia huduma bora na mara nyingi hospitali za uhakika na gharama zinakua juu kidogo.

Mwaka jana nilishuhudia shida alizopata shemeji yangu ,alikua anaumwa ugonjwa huo huo wa kidole tumbo yaani mwez wa 3 ndo alianza kuhisi maumivu ya tumbo marakwamara alipo pata vipimo ikaonekana ana huo ugonjwa ,akafanyiwa upasuaji ila baada ya siku moja kupita kile kidonda kikaanza kuvujisha uchafu mithili ya choo laini.

Tulipo toa taarfa wakamfanyia tena upasuaji kwa mara ya pili huku wakituficha sababu ya kurudia ule upasuaji.Baada ya kama siku 4 tena bdo hali ya kuvujisha ilijirudia ndipo waka akapata kupelekwa hospitali kubwa na uongozi wa ile hospitali .

Majibu tuliyoyapata pale kutoka ile hosptali kubwa tulipagawa sana maana yule daktar wa mara ya kwnza alikua hashon vzur kile kidonda.sitak kukutsha ndugu ila kuwa makini nashkur mungu shemej yang amepona kabsa baada ya kuhudumiwa kweny hosptal kubwa.
 
Naona ugonjwa wako haujachacha wala usingetafuta hiyo hospitali ya bei nafuu.
 
Nenda mbweni hospital haitazidi laki ishirini usisahau kuleta mrejesho
 
Naona ugonjwa wako haujachacha wala usingetafuta hiyo hospitali ya bei nafuu.
Appendicitis ikikaza hutafikiria gharama-unakua kama unachungulia upande wa pili ambae hakuna anaefahamu kukoje huko. Aiwahi kabla haija chacha.
 
Uko wapi?
Nenda kwenye hospitali za Mkoa kwa mfano Mwananyamala, Amana au Temeke utafanyiwa kwa kiasi hicho au chini yake.
Vinginevyo Tandika kuna hospitali inayofanya upasuaji, jina limenitoka.

Mwamanyamala si ndo huko watu wakienda hawarudi? Aende kwingine tu[emoji22]
 
1M duuu, nenda hospitali za serikali mkuu usisikie maneno ya watu kuwa serikalini huduma mbovu, kama unaogopa madaktari wapiga dili wa Dar, nenda hospitali za serikari za mikoani/hospitali nyingi za wilaya wanafanya huo upasuaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…