Wapiga Makachu Forodhani waruhisiwa, Watasaini Mkataba

Wapiga Makachu Forodhani waruhisiwa, Watasaini Mkataba

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Mamlaka ya Uhifadhi na uendeshaji wa Mji Mkongwe Zanzibar kwa kushirikiana na taasisi nyingine za serikali zimekubaliana kuwaruhusu vijana wa wapiga makachu katika eneo la Forodhani kuendelea na Shughuli zao kwa kuzingatia taratibu zilizoanishwa katika mikataba itakayosainiwa na vijana hao

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Mhandisi Ali Said Bakari ameeleza hayo ikiwa ni takribani wiki moja kwa vijana hao kuwekewa katazo la kupiga makachu katika eneo la Forodhani baada ya kuikukwa taratibu ikiwemo suala la maadili na uharibifu wa mali za serikali katika eneo hilo

Amesema shughuli za makachu zitaendelea kwa vijana watakaokua tayari kusaini mkataba na kuridhia masharti yaliyowekwa ili kufanya shughuli hizo bila ya kuvunja sheria na taratibu za nchi

Shughuli za upigaji makachu zitaanza rasmi Desemba 31, 2024 ikiwa ni sehemu pia ya kuukaribisha Mwaka mpya wa 2025 ambapo shughuli hizo zimekua ni sehemu kubwa ya ajira kwa vijana hao ambao waliathirika na katazo hilo kwa takriban wiki moja

PIA SOMA
- Zanzibar yapiga marufuku upigaji wa makachu Forodhani hadi serikali itakapoandaa utaratibu maalum wa shughuli hiyo
 
Kupiga makachu ni mchezo fulani hivi unahusisha vijana kubeba picha na kukimbia kuruka juu na kuingia ndani ya maji kwa mchupio. Michezo hii ni common sana eneo la forodhani Unguja
Kumbe ni aina ya mchezo!
Asante kutufahamisha.
 
Kwa hio kuruka namna hio huko Zanzibar ni kosa la kimaadi na kuharibu miundombinu?
wewe unaishi shimoni? Hilo eneo hao vijana wanatumia kutangaza utalii zanzibar, wanaita watu maarufu waje zanzibar, so watalii nao huja hapo kuruka na kupiga picha. Kuna baadhi ya watalii wanakuja hapo kuruka na nguo ambazo sio maadili ya Zanzibar, video zinasambaa mitandaoni, hao wanaoruka na chupi ndio wameleta shida.
 
wewe unaishi shimoni? Hilo eneo hao vijana wanatumia kutangaza utalii zanzibar, wanaita watu maarufu waje zanzibar, so watalii nao huja hapo kuruka na kupiga picha. Kuna baadhi ya watalii wanakuja hapo kuruka na nguo ambazo sio maadili ya Zanzibar, video zinasambaa mitandaoni, hao wanaoruka na chupi ndio wameleta shida.
Asante kunielewesha ndugu , nchi kubwa hii na ina mambo mengi sana yanayo tokea ila ndio hatuwezi kuyajua yote.
 
wameona wawe wapole maana vijana wa zenji walianza taratibu za kuhamia bara kupiga makachu

zanzibar wangepoteza fursa ya kutangazwa, ila wabongo nao wachukue hii waanze hapo dar watapata watu sana maana maadili kwetu si inshu sana
 
Back
Top Bottom