Wapigwe Vita Polisi kunyang'anya madereva leseni

Wapigwe Vita Polisi kunyang'anya madereva leseni

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Ajabu na kweli tunaposhuhudia utendaji mbovu kabisa wa jeshi la polisi kupata kutokea, kumbe wao pia wamejipa mamlaka zaidi na kujipongeza juu, kwa kupora haki za watu kuishi!

Eti kumbe Jan - Sep 2021 wamepokonya madereva 537 leseni za udereva? Jambo la hovyo kabisa kusikika kwa wapenda haki na usawa wote.

Kwa hakika hii haitokei kokote duniani. Tutakuwa tumerogwa!

IMG_20211123_150507_895.jpg


Ikumbukwe walengwa hapo watakuwa zaidi ni wale ambao udereva kwao ndiyo kazi yao rasmi inayowapatia kula.

Hivi mtu kama kazi yake pekee anayoendeshea maisha yake na familia yake ndiyo hiyo unamzuia vipi kuifanya milele? Hii si sawa na kumfukuza mtu kazi bila kumlipa stahiki zake? Ili akale wapi?

Kufikuzwa mtu kazi si jambo dogo. Mtu hafukuzwi kazi kirahisi rahisi hivi.

Kwamba kuna kada ambayo haihitaji katiba mpya?

Watu wenye kubagazwa, kuonewa, kunyanyaswa nk hawa, ni wadau wa kuaminika katika harakati thabiti za kudai katiba mpya:

Katiba Mpya ni muhimu kwa Sekta Zote

Taratibu zote za hovyo kama hizi majibu yake ya kueleweka yanaweza kupatiwa suluhu kwenye katiba mpya peke yake. Vinginevyo utakuwa mchezo wa maji na umeme au Ruvu na mchina.

Polisi hawa hawa? Si ndiyo hawa wa kwenye ajali hizi?

IMG_20211123_143522_497.jpg


Kwa utakatifu wao upi walionao kujipa umungu mtu upi kumbukumbu nani kifo?

Hivi hatua gani zilichukuliwa dhidi ya hao waliosababisha ajali hizo?

--------
Ajali iliyohusisha Magari Nane, maelezo ya Polisi yanatia shaka

Madereva 537 wafutiwa lesseni
 
Back
Top Bottom