Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
USULI: Suala la katiba lilitolewa tahadhari nyingi kabla ya kuanza. Tulionya nia mbaya iliyokuwepo tukizingatia CCM haikuwa tayari kwa mabadiliko. Tukaonya hoja kutekwa nyara na serikali, wapinzani kuridhia kwenda Ikulu na miswada bungeni. Taratibu za kuandika katiba hazikufuatwa na hilo lilipaswa kuwa 'wake up call''. Wapinzani hawakuzingatia.
Sasa wameungana kuzuia mswada usisainiwe na rais baada ya kufanyiwa vitimbwi bungeni.
Pengine ushirika ulipaswa kuanza mapema ili kukabiliana na nia mbaya.
Pamoja na kuchelewa au kukosa maono bado wanaendelea na makosa waliyoyafanya mwazoni,kuimba nyimbo za CCM!
NYIMBO ZA CCM
Tume ya katiba imeshatoa rasimu ya muelekeo wa katiba mpya. Suala la serikali 2, mkataba na mengine hayamo.Kinachojadiliwa ni maboresho ya rasimu inayoongelea serikali 3 au basi kuvunja muungano kama haliwezekani.
CCM wanarudisha hoja ya serikali 2 makusudi kabisa wakivuta muda. (Tutaangalia mbele)
KUSUSIA BUNGE NA MSWADA.
Marekebisho ya sheria ya mchakato wa katiba yameletwa na serikali ya CCM kwa hofu ya kushindwa hoja
1. Mswada unasema kura katika bunge la katiba zipigwe kwa 'simple majority' na siyo 2/3 kwa kuelewa hoja za CCM haziwezi kupata 2/3 kutoka pande zote. Kinachotakiwa ni kupata kura hata moja tu zaidi ili kushinda.
Kwamba mustakabali wa nchi utaamuliwa na kura mbili au tatu na si wingi wa wananchi.
Hii itafanyika kwa kutumia mbinu, tuangalie hoja ya pili.
2. Kumpa rais uwezo wa kuchagua wajumbe 166 watiifu na kufanya idadi ya kura kufikia' simple majority'.
Kama bunge lina wajumbe 604, wajumbe 300 wakakataa au kukubaliana na rasimu kwa namna yoyote tofauti na CCM, wale 304 wa CCM watiifu ambao 166 ni kutoka kwa rais watafanya 304 na kushinda(watu 4 tu).
Ili kuchakachua matokeo kwa urahisi kitafanyika nini? Tuangalie sehemu ya 3
3. Tume ya Warioba imeambiwa ikome shughuli zake kabla ya bunge la katiba kinyume na sheria ya sasa.
Kwamba atakayetetea rasimu atatoka kule CCM wanakotaka. Ni wapi hapo? Jibu ni hili
a) Wajumbe wengi wa CCM wakiwemo 166 wa rais ambao ni watiifu kwake.
b) Watachagua Spika kutokana na majority ya CCM na kusukumiza hoja kwa kutumia Spika na wabunge wao.
Nini kitafuta?
Uchakachuaji wa aina mbili.
1. Kwamba rasimu itakayokuwa imetengenezwa na Warioba inaweza kupigwa chini au kufanyiwa mabadiliko makubwa kulingana na matakwa ya CCM ambao watakuwa wengi wakiwemo wajumbe binafsi wa rais 166.
2. CCM itakuwa na njia ya kushinikiza hoja ya serikali 2 ambayo wanaibembeleza iendelee endelee kutajwa ili wakati ukifika wasema majority wanataka serikali 2.
Kwa kutumia wajumbe wengi na Spika wao uchakachuaji utakuwa umetimia.
Rasimu ya CCM kwa jina la wananchi itapatikana!.
MAKOSA YA WAPINZANI
1. Hawaelezi kwa kina kwanini wamekataa mswada na kwanini kuna marekebisho wasiokubalina nayo na madhara yake ni nini kwao. Wao wamejikita katika idadi ya wajumbe 166. Hata kama watapewa idadi hiyo kwa jinsi wanavyotaka bado wanavikwazo kama nilivyosema 1,2 na 3 hapo juu.
Wanasimamia hoja ya znz kutoshirikishwa hoja ambayo wznz wenyewe wamegawanyika,wengine wakisema wameshirikishwa na wengine la.
2. Akina Tundu Lisu,Mbowe, Lipumba, Mbatia n.k. wameng'ang'ania wajumbe sawa kutoka Zanzibar, znz huru na hoja zingine zisizolingana na suala la mswada wanaougomea. Wengine wamezidi kujikita katika wimbo wa serikali 2 wa CCM kitu wasichopaswa kukiongela maana hakipo katika rasimu.
WAFANYE NINI?
Kwanza lazima wajue nini CCM imekusudia kabla ya kuanza kupambana nao majukwaani.
Pili, waeleze hoja kwa njia rahisi ili mwananchi wa kawaida aelewe na si kutumia vifungu na maneno yanayowachanganya.
Tatu, Wakati wanajipanga lazima wajue wanagomea nini na wanataka iweje.
Hadi sasa kusema wajumbe 166 au znz kutoshitrikishwa ndilo tatizo na kuacha hoja nyingine za msingi ni kupunguza nguvu ya hoja zao na kushindwa
Ndio maana tunasema kwa mwendo walio nao wanapaswa kujipanga na kuetete hoja zao kwa mantiki tena zikieleweka na average Tanzanian. Vinginevyo naona kama wanatwanga maji kwenye kinu.
Natumaini kuna maono tofati juu ya hili. Wanajamvi karibuni tujadili, tukosoane, tuelekezane kwa mustakabali wa taifa.
Mchambuzi JokaKuu Jasusi AshaDii gfsonwin Ngongo Bongolander Kimbunga Remote Zitto JJ Mnyika Nape Nnauye Mwita Maranya Mzee Mwanakijiji EMT Mag3 Zinedine The Big show Ritz Yericko Nyerere@Masopyakindi Fundi Mchundo Ngambo Ngali Mchambuzi
Sasa wameungana kuzuia mswada usisainiwe na rais baada ya kufanyiwa vitimbwi bungeni.
Pengine ushirika ulipaswa kuanza mapema ili kukabiliana na nia mbaya.
Pamoja na kuchelewa au kukosa maono bado wanaendelea na makosa waliyoyafanya mwazoni,kuimba nyimbo za CCM!
NYIMBO ZA CCM
Tume ya katiba imeshatoa rasimu ya muelekeo wa katiba mpya. Suala la serikali 2, mkataba na mengine hayamo.Kinachojadiliwa ni maboresho ya rasimu inayoongelea serikali 3 au basi kuvunja muungano kama haliwezekani.
CCM wanarudisha hoja ya serikali 2 makusudi kabisa wakivuta muda. (Tutaangalia mbele)
KUSUSIA BUNGE NA MSWADA.
Marekebisho ya sheria ya mchakato wa katiba yameletwa na serikali ya CCM kwa hofu ya kushindwa hoja
1. Mswada unasema kura katika bunge la katiba zipigwe kwa 'simple majority' na siyo 2/3 kwa kuelewa hoja za CCM haziwezi kupata 2/3 kutoka pande zote. Kinachotakiwa ni kupata kura hata moja tu zaidi ili kushinda.
Kwamba mustakabali wa nchi utaamuliwa na kura mbili au tatu na si wingi wa wananchi.
Hii itafanyika kwa kutumia mbinu, tuangalie hoja ya pili.
2. Kumpa rais uwezo wa kuchagua wajumbe 166 watiifu na kufanya idadi ya kura kufikia' simple majority'.
Kama bunge lina wajumbe 604, wajumbe 300 wakakataa au kukubaliana na rasimu kwa namna yoyote tofauti na CCM, wale 304 wa CCM watiifu ambao 166 ni kutoka kwa rais watafanya 304 na kushinda(watu 4 tu).
Ili kuchakachua matokeo kwa urahisi kitafanyika nini? Tuangalie sehemu ya 3
3. Tume ya Warioba imeambiwa ikome shughuli zake kabla ya bunge la katiba kinyume na sheria ya sasa.
Kwamba atakayetetea rasimu atatoka kule CCM wanakotaka. Ni wapi hapo? Jibu ni hili
a) Wajumbe wengi wa CCM wakiwemo 166 wa rais ambao ni watiifu kwake.
b) Watachagua Spika kutokana na majority ya CCM na kusukumiza hoja kwa kutumia Spika na wabunge wao.
Nini kitafuta?
Uchakachuaji wa aina mbili.
1. Kwamba rasimu itakayokuwa imetengenezwa na Warioba inaweza kupigwa chini au kufanyiwa mabadiliko makubwa kulingana na matakwa ya CCM ambao watakuwa wengi wakiwemo wajumbe binafsi wa rais 166.
2. CCM itakuwa na njia ya kushinikiza hoja ya serikali 2 ambayo wanaibembeleza iendelee endelee kutajwa ili wakati ukifika wasema majority wanataka serikali 2.
Kwa kutumia wajumbe wengi na Spika wao uchakachuaji utakuwa umetimia.
Rasimu ya CCM kwa jina la wananchi itapatikana!.
MAKOSA YA WAPINZANI
1. Hawaelezi kwa kina kwanini wamekataa mswada na kwanini kuna marekebisho wasiokubalina nayo na madhara yake ni nini kwao. Wao wamejikita katika idadi ya wajumbe 166. Hata kama watapewa idadi hiyo kwa jinsi wanavyotaka bado wanavikwazo kama nilivyosema 1,2 na 3 hapo juu.
Wanasimamia hoja ya znz kutoshirikishwa hoja ambayo wznz wenyewe wamegawanyika,wengine wakisema wameshirikishwa na wengine la.
2. Akina Tundu Lisu,Mbowe, Lipumba, Mbatia n.k. wameng'ang'ania wajumbe sawa kutoka Zanzibar, znz huru na hoja zingine zisizolingana na suala la mswada wanaougomea. Wengine wamezidi kujikita katika wimbo wa serikali 2 wa CCM kitu wasichopaswa kukiongela maana hakipo katika rasimu.
WAFANYE NINI?
Kwanza lazima wajue nini CCM imekusudia kabla ya kuanza kupambana nao majukwaani.
Pili, waeleze hoja kwa njia rahisi ili mwananchi wa kawaida aelewe na si kutumia vifungu na maneno yanayowachanganya.
Tatu, Wakati wanajipanga lazima wajue wanagomea nini na wanataka iweje.
Hadi sasa kusema wajumbe 166 au znz kutoshitrikishwa ndilo tatizo na kuacha hoja nyingine za msingi ni kupunguza nguvu ya hoja zao na kushindwa
Ndio maana tunasema kwa mwendo walio nao wanapaswa kujipanga na kuetete hoja zao kwa mantiki tena zikieleweka na average Tanzanian. Vinginevyo naona kama wanatwanga maji kwenye kinu.
Natumaini kuna maono tofati juu ya hili. Wanajamvi karibuni tujadili, tukosoane, tuelekezane kwa mustakabali wa taifa.
Mchambuzi JokaKuu Jasusi AshaDii gfsonwin Ngongo Bongolander Kimbunga Remote Zitto JJ Mnyika Nape Nnauye Mwita Maranya Mzee Mwanakijiji EMT Mag3 Zinedine The Big show Ritz Yericko Nyerere@Masopyakindi Fundi Mchundo Ngambo Ngali Mchambuzi
Last edited by a moderator: