Wapinzani na Rasimu ya Katiba: Jipangeni kutetea hoja kwa mantiki

Wapinzani na Rasimu ya Katiba: Jipangeni kutetea hoja kwa mantiki

Nimeupenda huu Uchambuzi makini na wa kina wa bwana Nguruvi3.Ni kweli kwamba wanachofanya CHADEMA na Wapinzani wengine sijui kama kitaleta matokeo yanayotarajiwa.Kosa lilifanyika tangu awali pale walipokubali kwenda Ikulu kujadiliana na Rais kuhusu ile rasimu ya kwanza ambayo ilisainiwa kuwa sheria.Ni lazima tukiri kuwa hapa Kambi ya Upinzani ilionyesha uchanga wao katika siasa za Nchi hii.Kwa CHADEMA kukubali mwaliko wa Rais na Mwenyekiti wa Chama ambacho mwanzoni hakikuwa tayari kabisa kukubaliana na hoja ya Katiba mpya kwenda kujadiliana na kudhani kuwa angewafanyia yale wayatakayo!!?CCM walijua walichokuwa wanakifanya na kwa bahati mbaya sana kwamba CHADEMA hawakung'amua mtego huu wa CCM japo tuliokuwa huku mitaani tulijuwa nini hasa kitakachowapata CHADEMA mbeleni ambacho ni kugeukwa.Chanzo cha CHADEMA kuyumba katika hoja nyingi walizozianzisha ni kwasababu wamekosa Kiongozi makini.Natamani kama Dr Slaa angekuwa Bungeni na kuongoza Kambi ya Upinzani nadhani Bunge lingependeza kwa vita vya hoja nzito.
 
Maoni yaliyomo kwenye rasimu ni maoni ya wananchi hasa hili serikali tatu, lazima ya heshimiwe.
Ndivyo ilipaswa iwe, kwa bahati mbaya haitakuwa hivyo.
Tume ya Warioba iliyosheheni wasomi nayo haiwezi kukwepa lawama. Tuliwaeleza tume kuwa mchakato wa katiba lazima ufuate taratibu zinzohusiana na suala hilo. Kwamba, wao wanatakiwa waongoze mchakato na si kuongozwa katika mchakato.

Tunakumbuka Rais wa JMT aliwahi kutoa ratiba ya mchakato. Tukauliza nani mwenye mamlaka ya kufanya hivyo? Serikali au tume ambayo ilisemwa ipo huru. Tukamwambia Wariona na wenzake kuna harufu ya kuingiliwa kwa shughuli zao.

Moja ya wajumbe wa tume Profesa Mwesigwa Baregu akatoka na kauli 'nchi kwanza chama baadaye'
Hatukuwa tunapinga uzalendo kinyume chake kuimarisha kwa bahati mbaya nao kama Watanzania wengine njaa ikakamata hatamu. Pengine wangetueleza matumbo kwanza nchi baadaye na chama mwisho tungewaelewa kwa urahisi.

Juzi wajumbe wote wanalalamika kuingiliwa. CCM wamepeleka mswada unaowataka kumaliza kazi yao kabla ya kumalizika.Kwamba, bunge la katiba likianza wao watakoma katika shughuli.

Hii maana yake ni kuwa bunge la katiba litaongozwa na mCCM awe Spika au mwenyekiti.
Hila za kuchaguana kuchangia na kuchakachua maoni na kura zitafanyika akina Warioba wakiwa pembeni. Rasimu ya katiba itatetewa na akina Lukuvu, Nape, Wasira n.k.

Anayeweza kutoa ufafanuzi wa rasimu ni yule aliye ratibu na kukusanya maoni ya wananchi. Sasa utumishi wa tume ukikoma wakati wa bunge la katiba nani ataitetea rasimu? Hapa si kuchezeana shere kweli!!!

Hapo ni sawa na ''kumkabidhi fisi bucha ya nyama, sijui tutegemee nini''
 
Wapinzani wanaposhindwa kukabiliana na hoja dhaifu za wapotoshaji.

Hivi karibuni waziri wa sheria na mh Wassira wamemtaka rais wa JMT asaini mkataba kwasababu kinyume cha hivyo rais ataingia katika mgogoro wa kikatiba kati ya mihimili miwili, bunge na serikali.

Nilitegemea wapinzani waulize na kukumbushia machache:
Ni mara ngapi rais amepewa maagizo ya kutekeleza na bunge na kuyafumbia macho? Kwanini nchi haikuingia katika mgogoro wa na mhimili wa bunge. Tunakumbuka suala la katibu mkuu kiongozi aliyeondoka Luhanjo, waziri wa Nishati, EPA na kashfa nyingi ambazo rais alipaswa kuzitolea maamuzi kwa mujibu wa maelekezo ya bunge na hakufanya hivyo.
Vipi leo mgongano wa mihimili uonekane.

Ni kifungu gani cha katiba ambacho kinamzuia rais kutopinga mswada kutoka bungeni, tukijua wazi kuwa kipo kifungu kinachompa fursa ya kusaini au kutosaini na ikibidi anaweza kuurudisha mswada bungeni.
 
Na kwa kuongezea nafikiri uwanja wa Wapinzani kuelezea hoja zao waliufanya wenyewe kuwa finyu sana.
Mathalani ilitakiwa mwanzo kabisa kabla muswada haujaanza kujadiliwa Waziri kivuli autolee ufafanuzi wa kina na kila
udhaifu uwekwe hadharani, hapa wangepata "political gain" kwenye siasa za Kitaifa kama Watu makini wanaotarajia kuongoza dola.

Nachokiona ni kama hawa wote wanategemea watu wawili watatu waseme nao wafuate mkumbo.

Pili, hawakujadili kwa kina namna Tume ya Warioba ilivyominywa pale ambapo inatakiwa kuvunjwa ili kupisha Bunge la Katiba. Wangelisemea hili kwa lugha nyepesi wangepata uungaji mkubwa zaidi wa Wananchi, na hapa wangeonekana si tu wanajali maslahi ya upande mmoja (kwa maana ya kusisitiza "Utaifa") bali wangeonekana wanaitetea Tume na kwamba CCM inaivuruga kwa maslahi yake na siyo ya Kitaifa.

Tatizo la Wabunge wengi ikiwemo wa Upinzani hawajishughulishi kusoma na kuchambua makabrasha kabla ya kuzungumza. Nimewaona mara nyingi Dodoma hata nyakati ambazo kuna hoja nyeti inaletwa kesho Bungeni wao jioni mpaka usiku wa manane wanapiga pombe!!
Nakubaliana nawe kuwa kulikuwa hakuna mkakati mzuri wa kukabiliana na hoja licha ya ukweli kuwa wapinzani walizembea kuanzia mwanzo.(drop the ball)

Labda nikumbushe wakati wa mswada wa kuunda mabaraza ya kata CCM walikomalia suala la wakuu wa Wilaya na maafisa tawala kushirikishwa. Tulishangaa pale kiongozi wa upinzani KUB alipokubali hoja za CCM ili kuondoa mvutano na kukokoa jahazi! KUB alisahahu kuwa wao wana ilani na CCM hawana ilani ya katiba hivyo hawawezi kuaminika kwa lolote na huo ulikuwa mtego wa mwanzo

Kinachoonekana ni kupoteza focus ya kueleza kwanini wanapinga mswada.
Juzi nimemsikia Tundu Lissu akihutubia na nachelea kusema nilimshangaa sana.
Kwanza aliongelea suala la muungano kufa kwasababu hadi sasa rais wa znz anapigiwa mizinga.

Lissu akasema wajumbe wa bunge la katiba wanapaswa kuwa sawa na si katika uwiano kwasababu znz ni nchi.
Akaendelea kudai kuwa kama znz hawatasimama kidete wataendelea kuumizwa na muungano.
Mh Lissu akasema katika mswada huu znz haikushirikishwa.

Kwanza, kama anatambua muungano umekufa siku nyingi kwa znz kuwa huru yeye anafanya jitihada gani kwa Tanganyika kupata serikali yake ili kama ipo haja serikali mbili zikae pamoja.

Pili, anapoangalia uwiano je anatenda haki kwa upande mwingine wa muungano katika suala zima.
Haiwezekani tuongelee wajumbe katika usawa na kuepeuka gharama kwa kutumia udogo au ukubwa.
Wapi Lissu anasimama kama mbunge wa Singida na mwananchi wa Tanganyika.

Tatu, kama anadai muungano ulishakufa kwanini adai tena znz kushirikishwa katika kuandaa katiba ya muungano uliokufa tayari. Kwanini asiwashauri wzn wajitoe kabisa ili wawe huru kama alivyosema.
Sidhani kama Tundu Lissu anawajibu wa kuongelea znz huru.

Focus ilitakiwa kujibu hoja za wananchi kwanini walisusia bunge. Majibu yapo wazi.
Sasa kunapokuwa na kupoteza focus kiasi hiki inatia wasi wasi sana.

Lissu hapaswi kuongelea historia kwasababu hilo si muhimu kwa sasa.
Na kazi ya kuongelea wnz aiche kwa Uamsho, SMZ, BAKAZA na kamati ya maridhiano.
Yeye aangalie masilahi mapana ya Tanganyika na si kutafuta ushawishi usiojibu mambo ya wakati tulio nao.
 
Mkuu wewe ndiyo huna hoja hata chembe muungano wenyewe wa mbowe mbatia na lipumba halafu usipende kupotosha rasimu bado haijatoa msimamo juu ya serikali ngapi zinafaa ila ni mapendekezo tu.

Kama hukuelewa kabisa bora usingejibu. Kwanza uelewe Kiswahili kuwa Rasimu maana yake ni mapendekezo au draft. Hivyo kusema hayo ni mapendekezo tu na siyo rasimu inakuwa siyo sahihi.

Rasimu ya katiba inasema wazi kutakuwa na serikali tatu. Muungano, Tanganyika na Zanzibar. Hiyo ndiyo rasimu.

Jambo jingine ambalo baadhi ya wajumbe wamelisema huko nyuma ni kuwa KATIBA HII NA TAASISI ZAKE IMEZINGATIA SERIKALI TATU. Hivyo hao walevi wanaosema serikali mbili watuambie na muuondo wa hiyo katiba utakuwaje.
 
Swala la katiba siyo swala la kushinikizwa na akina mbowe ni swala ambalo liko na taratibu zake ndizo zifuatwe kuvuta bangi na kufoka majukwaani hakuna mpango wa maana.

Moderator tafadhari ndugu zangu tunaomba mtuondolee huyu kiumbe kwenye uzi huu!
 
USULI: Wapinzani hawakuzingatia.
Mkuu si kweli nadhani wewe hujaielewa moral authority na commitment ya unaowaita wapinzani.
Sasa wameungana kuzuia mswada usisainiwe na rais baada ya kufanyiwa vitimbwi bungeni.
Hawajaungana kuzuia muswada usisainiwe wanatoa elimu na mrejesho wa yaliyotokea ili kuwa"empower" wananchi na elimu ya suala hili ili watakapotakiwa kufanya maamuzi wafanye maamuzi "infomed".
Pengine ushirika ulipaswa kuanza mapema ili kukabiliana na nia mbaya.
Demokrasia inaheshimu kukubaliana na kukubaliana kutokubaliana hakuna shinikizo hapa ni hoja zinachukua mkondo wake.
Pamoja na kuchelewa au kukosa maono bado wanaendelea na makosa waliyoyafanya mwazoni,kuimba nyimbo za CCM!
Hawajachelewa na wala hawajawahi ila wanatekeleza dhamiri zao katikati ya changamoto DHALIMU.
NYIMBO ZA CCM
CCM wanarudisha hoja ya serikali 2 makusudi kabisa wakivuta muda. (Tutaangalia mbele)
Huo wimbo umezikwa kwa matakwa ya wananchi na siyo kwa jitihada za CCM kutumia mihili ya dola. Mkakati wa muungano huu una ishara kuwa kuna focus na dhamira ya kupata Katiba ya Kitaifa. CCM wanajua kuwa mwisho wa yote Katiba itapigiwa kura labda na hilo walibadiri kwa mikakati ya kutumia mihimili ya dola. Mwisho wake CCM wenyewe wataanzisha vurugu ambayo itachukua muda mrefu. ILA HAITAWANUSURU.
KUSUSIA BUNGE NA MSWADA.
Marekebisho ya sheria ya mchakato wa katiba yameletwa na serikali ya CCM kwa hofu ya kushindwa hoja.

Watake radhi tafadhali kwani hawakususia mchakato wa katiba bali ulifanywa mkakati wa kuwaengua ikabidi waje kwenye mahakama ya wenye nchi. Tayari sisi wengine tumeyajua tusiyokuwa tunayajua
Nini kitafuta?
Uchakachuaji. Rasimu ya CCM kwa jina la wananchi itapatikana!.
Hakuna kitu kama hicho usikate tamaa kitu cho chote kizuri lazima kipitie kwenye tanuru. Hiyo unayoitaja itayotokana na CCM hata wao wanajua; ila wanatafuta muda wa kujipanga yaani kuchelewesha katiba ya wananchi ambayo lazima itapatikana ndani ya hila hizi hizi. Kwa taarifa yako hata wao wanajiuliza kwa makini kuwa wanakwama wapi. WANAKWAMA KWENYE UUNGWAJI MKUBWA MKONO WA WANANCHI KUHUSU HOJA NA ELIMU INAYOTOLEWA na unaowaita wapinzani. WANASUTWA NA DHAMIRA AMBAZO NI CHANZO CHA CCM KUFANYA MAKOSA WASIYOYATARAJIA.
MAKOSA YA WAPINZANI
Natumaini kuna maono tofati juu ya hili. Wanajamvi karibuni tujadili, tukosoane, tuelekezane kwa mustakabali wa taifa.
Maoni tofauti yapo, ni kuwa JITIHADA ZA CCM NI "SURVIVAL" wakati unaowaita wapinzani JITIHADA ZAO NI KUPATA KATIBA MUAFAKA YENYE MASLAHI KWA KILA MTANZANI PAMOJA NA CCM. Hapo jiulize shetani atakuwa upande gani.

SAMAHANI NIMECHANGIA BILA KUWEPO KWENYE ORODHA YAKO NIPO NAFUATILIA KWA MAKINI
 
Mkuu si kweli nadhani wewe hujaielewa moral authority na commitment ya unaowaita wapinzani.Hawajaungana kuzuia muswada usisainiwe wanatoa elimu na mrejesho wa yaliyotokea ili kuwa"empower" wananchi na elimu ya suala hili ili watakapotakiwa kufanya maamuzi wafanye maamuzi "infomed".Demokrasia inaheshimu kukubaliana na kukubaliana kutokubaliana hakuna shinikizo hapa ni hoja zinachukua mkondo wake.Hawajachelewa na wala hawajawahi ila wanatekeleza dhamiri zao katikati ya changamoto DHALIMU.Huo wimbo umezikwa kwa matakwa ya wananchi na siyo kwa jitihada za CCM kutumia mihili ya dola. Mkakati wa muungano huu una ishara kuwa kuna focus na dhamira ya kupata Katiba ya Kitaifa. CCM wanajua kuwa mwisho wa yote Katiba itapigiwa kura labda na hilo walibadiri kwa mikakati ya kutumia mihimili ya dola. Mwisho wake CCM wenyewe wataanzisha vurugu ambayo itachukua muda mrefu. ILA HAITAWANUSURU.
Watake radhi tafadhali kwani hawakususia mchakato wa katiba bali ulifanywa mkakati wa kuwaengua ikabidi waje kwenye mahakama ya wenye nchi. Tayari sisi wengine tumeyajua tusiyokuwa tunayajua Hakuna kitu kama hicho usikate tamaa kitu cho chote kizuri lazima kipitie kwenye tanuru. Hiyo unayoitaja itayotokana na CCM hata wao wanajua; ila wanatafuta muda wa kujipanga yaani kuchelewesha katiba ya wananchi ambayo lazima itapatikana ndani ya hila hizi hizi. Kwa taarifa yako hata wao wanajiuliza kwa makini kuwa wanakwama wapi. WANAKWAMA KWENYE UUNGWAJI MKUBWA MKONO WA WANANCHI KUHUSU HOJA NA ELIMU INAYOTOLEWA na unaowaita wapinzani. WANASUTWA NA DHAMIRA AMBAZO NI CHANZO CHA CCM KUFANYA MAKOSA WASIYOYATARAJIA.Maoni tofauti yapo, ni kuwa JITIHADA ZA CCM NI "SURVIVAL" wakati unaowaita wapinzani JITIHADA ZAO NI KUPATA KATIBA MUAFAKA YENYE MASLAHI KWA KILA MTANZANI PAMOJA NA CCM. Hapo jiulize shetani atakuwa upande gani
Mkuu Mimibaba , kwanza nataraji safari yako ni njema na nashukuru kwa mchango wako.

Katika mambo uliyogusia kuna hili la kutoa elimu kwa umma. Kwanza niseme ndilo hasa kiini cha mada.
Tutakubaliana au kutofautiana kuwa elimu inayotolewa ina walakini.
Nimetoa mifano ya Tundu Lissu ambaye ujumbe wake kwa umma umekuwa unakwenda mbele na nyuma.

Elimu ya umma ni pamoja na kuuleza umma huo tatizo, sababu na njia mbadala.
Ukisikiliza jinsi wanavyojenga ni kama wanalalamika tena kwa jambo lisiloleta mantiki. Ukweli ni kuwa wana mantiki kubwa sana isipokuwa communication skills zao zinaniacha na maswali.

Hoja ya wao kutoka bungeni ni wachache sana wanaelewa jinsi walivyoenguliwa kwa hila na naibu spika Ndugai.
Hicho ni miongoni mwa mambo wanayopaswa kuyaeleza na sababu zinazopelekea wao kuenguliwa.
Waeleze mkakati wa CCM na bunge la CCM katika kuburuza umma.

Ukisoma mada ambayo pengine kuna nisiyoyajua kama ulivyosema, hakuna shaka kuwa mkakati wa CCM kwanza ni kuhakikisha tume ya Warioba inapokwa majukumu. Pili kutumia fursa hiyo kuandaa mazingira ya uharibifu, uchakachuaji na ubambikizaji wa katiba.

Tume ya Warioba inatakiwa ikome utendaji wake wakati wa bunge la katiba. Hiyo itatoa nafasi kwa CCM kushika hatamu za mchakato kwa kuweka Spika wao na kutumia wajumbe 166 binafsi wa rais.

Hapo tutarudi kwenye kosa lile lile la kuenguliwa kwa kutumia wingi kama ilivyofanyika bungeni. Je, hilo wapinzani wamelifikiria?

Pili, hoja yao ya rais kutoteua wajumbe bado ni mfumu. Wajumbe 166 kutoka taasisi nyingine wanapaswa kupatikana kwa njia isiyomhusu rais. Wapinzani wanakubali majina apewe rais bila kuyafanyia uchakachuaji.
Kwanini apewe rais? Nilidhani hoja yao ingekuwa uwepo wa wajumbe 166 kutoka katika taasisi bila kumshirikisha rais.

Katika mchakato huu rais hahusiki na haipaswi kumpa hata fursa ya kuidhinisha majina.
Aidhinishe kwa minajili gani ili hali wananchi wanaandika katiba yao?
Hapo mkuu elimu ya umma huoni ina mapungufu?

Nadhani ni muhimu wapinzani wakajikita katika hoja zinazogusa wakati na mambo ya sasa.
Ni ajabu wao kurudi katika kueleza historia wakati hilo ni jambo lililopita na sasa tunakwenda mbele.

Kwa ufupi wapinzani walitekwa mapema sana walipoachia suala jili liendeshwe na serikali na haionekani kama wamejifunza.

Jukumu la katiba ni la wananchi hilo halina majadala. Lakini basi kuna viongozi wanaopaswa kutoa elimu ya umma kwa nafasi zao. Hawa wanapaswa kutumia fursa hiyo kikamilifu bila kupeleka ' hoja mchanganyiko' ambazo huwachanganya wananchi wa kawaida. Ujumbe wao haujaeleweka na sijui kama mahakama ya wananchi inaelewa kwa kadri hali inavyoonekana.

 
Last edited by a moderator:
Kwani bunge la katiba likimaliza kazi yake na kuandaa rasimu ya pili ya katiba itarudi kwa wananchi na kupigiwa kura ya maoni (maamuzi yote yako mikononi mwa wananchi kupitia kura zao za maoni juu ya rasimu ya pili ya katibu) tufunguke jamani
 
Kwani bunge la katiba likimaliza kazi yake na kuandaa rasimu ya pili ya katiba itarudi kwa wananchi na kupigiwa kura ya maoni (maamuzi yote yako mikononi mwa wananchi kupitia kura zao za maoni juu ya rasimu ya pili ya katibu) tufunguke jamani
Nadhani hujaelewa jambo. Tume ya Warioba kwa mujibu wa marekebisho ya mswada itakoma kazi bunge la katiba likianza.

Swali langu kwako, ni nani ataielezea rasimu hiyo ndani ya bunge la katiba?
Pili, kwanini rais apewe uwezo wa kueteua wajumbe wake 166 ambao ni sawa na robo ya wajumbe wote wa bunge la katiba.

Ukishanifahamisha hayo tutaendelea kujadiliana vema tu.

 
Swali la tatu; kama rais anapewa mamlaka ya kuteua wajumbe hao, tuna uhakika kiasi gani kwa patakuwa hamna upendeleo?
 
Swali la tatu; kama rais anapewa mamlaka ya kuteua wajumbe hao, tuna uhakika kiasi gani kwa patakuwa hamna upendeleo?
Ni definite atafanya anachoona ni kwa masilahi yake na hakuna atakayemuuliza kwasababu sheria ina mruhusu. Na kwanini awe na wajumbe binafsi, katiba ya nchi inaandikwa na mtu au watu?
 
Kwa muono wangu kuhusu maswala ya katiba, ili kweli kiwe chombo cha kidemokrasia, pande zote mbili zisikilizwe kwanza.

Halafu, ushabiki usiohusisha fikra bungeni ufe mara moja.
 
Back
Top Bottom