Wapinzani na Wanaharakati acheni kuilaumu Marekani na nchi za EU

Wapinzani na Wanaharakati acheni kuilaumu Marekani na nchi za EU

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Nimeona kwenye mitandao ya kijamii wapinzani na wanaharakati wakishambulia na kulaumu tamko la ubalozi wa Marekani kuhusu kukamatwa na kuwachiwa kwa viongozi wa CHADEMA kwamba ni tamko dhaifu sana lakini zaidi wakiilamu Marekani na Washirika wake Ulaya kutoweka shinikizo la kutosha kwa serikali ya Tanzania kuhusiana na masuala ya demokrasia.

Huku ni ukosefu mkubwa sana wa uelewa wa geopolitics hasa ulewa kuhusiana na nafasi ya Tanzania kwa Marekani.

Ili kutoendelea na hizi lawama zisizo za msingi ni muhimu kufahamu haya

Tanzania sio mshirika muhimu wa kimkakati wa Marekani kwa Africa katika uchumi na usalama wa taifa. Hatuna rasilimali muhimu kwa wingi ambazo zinaivutia sana Marekani, hatuna biashara kubwa na Marekani na pia masuala ya ugaidi na dawa za kulevya sio masuala makubwa hapa nchini.

Tanzania sio mmojawapo ya mataifa mengi ya Africa yaliyo karibu kiutamaduni na Marekani. Siasa za ujamaa ziliufanya muelekeo wetu kuwa wa siasa za Mashariki/ Ukomunisti na imetufanya kuwa karibu zaidi na China, hata chama tawala mshirika wake mkubwa wa nje ni chama cha CCP cha China.

Tanzania sio jirani na Marekani, ujirani ni jambo muhimu sana kwenye geopolitics. Kama tungekuwa karibu na Marekani tungeweza kutazamwa kwa jicho la ziada.

Marekani inapitia wimbi la siasa za kujitenga(isolationism) na hivyo sio rahisi kujiingiza sana kwenye siasa za ndani za nchi nyingine.

Marekani inapitia changamoto kubwa ya ukuu wake/hegemony duniani baada ya vita vya Urusi na Ukraine. Marekani ilipigwa na butwaa baada ya kuona nchi nyingi za Africa zikiunga mkono au kubaki neutral katika uvamizi wa Urusi kwa Ukraine. Kuna sauti za raia katika nchi nyingi za Africa wanafurahia hili kwa sababu tu wanaamini ni "balance of powers". Marekani Isengetaka kuendelea kutibua sehemu ambazo bado inakubalika na watawala.

Jambo muhimu zaidi ni bora kufahamu Marekani inapokuwa nje ya taifa lake demokrasia sio kipaumbele kwake bali maslahi ya taifa lake hasa ya usalama na uchumi ndio vitu muhimu zaidi. Ndio maana kuna nchi nyingi sana ambapo inashirikiana na tawala za kiimla mfano Saudi Arabia, Misri na Angola.

Mwisho pia Marekani imeanza kukubaliana na ukweli kwamba huwezi kuwalazimisha ng'ombe kunywa maji mtoni. Marekani kila raia anaamini katika demokrasia ila wanapishana tu katika sera na itikadi. Katika taifa ambalo kuna raia wengi hawaamini katika demokrasia, wengine wanawazia utawala wa sharia na wengine wanaona uimla unawafaa zaidi kwa sababu wanaamini demokrasia inachelewesha na kukwamisha baadhi ya mambo muhimu huku ikiwaleta pia mambo wasiyoyahitaji unafanyaje??
 
Tanzania is not a vassal or proxy state. kwahiyo tamko la balozi yeyote halina.CDM waelewe wa kuwalaumu ni sisi wananchi yenyewe..ukiona kamata kamata yote hii bado watu wako kimya,ujue majority wanakubaliana na yanayotokea.

Kama wanabisha, wakamate yule mchungaji wa Kawe uone jinsi wafuasi wake watakavyoingia barabarani
 
"Marekani inapitia wimbi la siasa za kujitenga(isolationism) na hivyo sio rahisi kuujingiza kwenye siasa za ndani za nchi nyingine".

ni karibu kabisa US Itafika kwenye pick ya ISOLATION,lakini sioni kama itaondoka midomoni mwa watu kirahisi ama Pengine isiwezekane kabisa.

tazama Francophones countries, francophone kupinduana ni jadi yao toka dahali..uko nyuma lawama alizibeba Mkoloni(france) wao kila mapinduzi yalipofanyika na tunaendelea kuona anaendelea kutupiwa lawama hata baada kuondoka katika hizo nchi.
Mfn, Ibrahim Traore hata akijikwaa ama akipaliwa na Maji utasikia watu wanalaum France.
so,the something kitatokea kwa Marekani pia ila yote katika yote muda utawaumbua waliodhani US has subject them to poverty
 
The tweet and memo (attached) by Sauti ya Watanzania, signed by Arthur Chilipweli, is a good start.

Screenshot_20240813_164437_X.jpg


20240812_183552.jpg


However, it is vague, tactless, undiplomatic and inconsiderate to the conditions of the fine kabuki dance that is The Vienna Convention on International Relations.

I also feel like it is low key outsourcing the job of our own second liberation. Before jumping on the foreign missions, what are we as a nation doing?

These envoys frequently visit Sugu and his ilk, what do they talk about? How is blasting them on X more helpful than plotting with them in confidence?

They (Sauti ya Watanzania) should have at least documented a litany of the abuses and press coverage and linked to the tweet.

I can't shake the feeling that, by this style of engagement, Tanzanian activists and their allies abroad are rudely and publicly imposing on the foreign missions to get into our fights. Essentially saying "Why are you guys not fighting our war?" on X.

If you want other people to fight your wars, at least have the courtesy to ask nicely, preferably privately.

They don't have to do jack. They can say we are going Chinese in preparation for a Trump world that is going to drop all these shithole countries. "We have seen it all before, tried to help, ended up being blamed for interfering in other sovereign nations internal affairs" type of attitude. What then?

Arthur Chilipweli wrote like a State Department/Foreign Office overlord evaluating the perfomance of underlings in the embassies/high commissions.

What type of entitlement is that?

The US Embassy has released a statement.

IMG-20240813-WA0013.jpg
 
The tweet and memo (attached) by Sauti ya Watanzania, signed by Arthur Chilipweli, is a good start.

View attachment 3069220

View attachment 3069212

However, it is vague, tactless, undiplomatic and inconsiderate to the conditions of the fine kabuki dance that is The Vienna Convention on International Relations.

I also feel like it is low key outsourcing the job of our own second liberation. Before jumping on the foreign missions, what are we as a nation doing?

These envoys frequently visit Sugu and his ilk, what do they talk about? How is blasting them on X more helpful than plotting with them in confidence?

They (Sauti ya Watanzania) should have at least documented a litany of the abuses and press coverage and linked to the tweet.

I can't shake the feeling that, by this style of engagement, Tanzanian activists and their allies abroad are rudely and publicly imposing on the foreign missions to get into our fights. Essentially saying "Why are you guys not fighting our war?" on X.

If you want other people to fight your wars, at least have the courtesy to ask nicely, preferably privately.

They don't have to do jack. They can say we are going Chinese in preparation for a Trump world that is going to drop all these shithole countries. "We have seen it all before, tried to help, ended up being blamed for interfering in other sovereign nations internal affairs" type of attitude. What then?

Arthur Chilipweli wrote like a State Department/Foreign Office overlord evaluating the perfomance of underlings in the embassies/high commissions.

What type of entitlement is that?

The US Embassy has released a statement.

View attachment 3069225
Hakika, kufikiria kwamba ubalozi wa Marekani una wajibu wa kupigania haki zako Mtanzania ni entitlement iliyopitiliza. Hawa watu wanapaswa kuelewa wajibu wa kwanza na mkuu wa ubalozi wa Marekani ni maslahi ya Marekani, mengine yote ni secondary.
 
Hakika, kufikiria kwamba ubalozi wa Marekani una wajibu wa kupigania haki zako Mtanzania ni entitlement iliyopitiliza. Hawa watu wanapaswa kuelewa wajibu wa kwanza na mkuu wa ubalozi wa Marekani ni maslahi ya Marekani, mengine yote ni secondary.
Lakini ujue hawa wengine Wamarekani-Watanzania wanaihimiza serikali yao itimize maneno yake.
 
"Marekani inapitia wimbi la siasa za kujitenga(isolationism) na hivyo sio rahisi kuujingiza kwenye siasa za ndani za nchi nyingine".

ni karibu kabisa US Itafika kwenye pick ya ISOLATION,lakini sioni kama itaondoka midomoni mwa watu kirahisi ama Pengine isiwezekane kabisa.

tazama Francophones countries, francophone kupinduana ni jadi yao toka dahali..uko nyuma lawama alizibeba Mkoloni(france) wao kila mapinduzi yalipofanyika na tunaendelea kuona anaendelea kutupiwa lawama hata baada kuondoka katika hizo nchi.
Mfn, Ibrahim Traore hata akijikwaa ama akipaliwa na Maji utasikia watu wanalaum France.
so,the something kitatokea kwa Marekani pia ila yote katika yote muda utawaumbua waliodhani US has subject them to poverty
Ni kweli hakuna namna ya kukwepa kuiongolea Marekani kwa miaka mingi sana ijayo lakini pia ni vizuri kuelewa kiasi cha umuhimu wako kwa mtu fulani ili kutojipa matumaini hewa.
 
Nimeona kwenye mitandao ya kijamii wapinzani na wanaharakati wakishambulia na kulaumu tamko la ubalozi wa Marekani kuhusu kukamatwa na kuwachiwa kwa viongozi wa CHADEMA kwamba ni tamko dhaifu sana lakini zaidi wakiilamu Marekani na Washirika wake Ulaya kutoweka shinikizo la kutosha kwa serikali ya Tanzania kuhusiana na masuala ya demokrasia.

Huku ni ukosefu mkubwa sana wa uelewa wa geopolitics hasa ulewa kuhusiana na nafasi ya Tanzania kwa Marekani.

Ili kutoendelea na hizi lawama zisizo za msingi ni muhimu kufahamu haya

Tanzania sio mshirika muhimu wa kimkakati wa Marekani kwa Africa katika uchumi na usalama wa taifa. Hatuna rasilimali muhimu kwa wingi ambazo zinaivutia sana Marekani, hatuna biashara kubwa na Marekani na pia masuala ya ugaidi na dawa za kulevya sio masuala makubwa hapa nchini.

Tanzania sio mmojawapo ya mataifa mengi ya Africa yaliyo karibu kiutamaduni na Marekani. Siasa za ujamaa ziliufanya muelekeo wetu kuwa wa siasa za Mashariki/ Ukomunisti na imetufanya kuwa karibu zaidi na China, hata chama tawala mshirika wake mkubwa wa nje ni chama cha CCP cha China.

Tanzania sio jirani na Marekani, ujirani ni jambo muhimu sana kwenye geopolitics. Kama tungekuwa karibu na Marekani tungeweza kutazamwa kwa jicho la ziada.

Marekani inapitia wimbi la siasa za kujitenga(isolationism) na hivyo sio rahisi kujiingiza sana kwenye siasa za ndani za nchi nyingine.

Marekani inapitia changamoto kubwa ya ukuu wake/hegemony duniani baada ya vita vya Urusi na Ukraine. Marekani ilipigwa na butwaa baada ya kuona nchi nyingi za Africa zikiunga mkono au kubaki neutral katika uvamizi wa Urusi kwa Ukraine. Kuna sauti za raia katika nchi nyingi za Africa wanafurahia hili kwa sababu tu wanaamini ni "balance of powers". Marekani Isengetaka kuendelea kutibua sehemu ambazo bado inakubalika na watawala.

Jambo muhimu zaidi ni bora kufahamu Marekani inapokuwa nje ya taifa lake demokrasia sio kipaumbele kwake bali maslahi ya taifa lake hasa ya usalama na uchumi ndio vitu muhimu zaidi. Ndio maana kuna nchi nyingi sana ambapo inashirikiana na tawala za kiimla mfano Saudi Arabia, Misri na Angola.

Mwisho pia Marekani imeanza kukubaliana na ukweli kwamba huwezi kuwalazimisha ng'ombe kunywa maji mtoni. Marekani kila raia anaamini katika demokrasia ila wanapishana tu katika sera na itikadi. Katika taifa ambalo kuna raia wengi hawaamini katika demokrasia, wengine wanawazia utawala wa sharia na wengine wanaona uimla unawafaa zaidi kwa sababu wanaamini demokrasia inachelewesha na kukwamisha baadhi ya mambo muhimu huku ikiwaleta pia mambo wasiyoyahitaji unafanyaje??
[emoji7][emoji7]
 
Marekani ilimuwekea Makonda vikwazo wakati wa utawala wa Magufuli sababu ilikuwa nini ?
 
Back
Top Bottom