Wapinzani na wanaharakati, andaeni maandamano ya amani kutaka uwazi wa mikataba ukiwemo wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo

Wapinzani na wanaharakati, andaeni maandamano ya amani kutaka uwazi wa mikataba ukiwemo wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Naomba nitoe wito kwa wanasiasa upinzani pamoja na wanaharakati, waombe kibali cha kufanya maandamano ya amani kushinikiza uwazi wa mikataba ukiwemo mkataba wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo.

Mradi huu ni mkubwa sana na kwa maana hiyo, unaweza kuleta matokeo makubwa kwa nchi yetu ambayo yanawe kuwa ni chanya( positive) au hasi(negative) kwa nchi yetu9 hivyo hatupawi kukaa kimya.

Mradi huu ukiwa na matokeo chanya, utafaidisha mpaka vitukuu wetu, na ukiwa na matokeo hasi, basi utaathiri mpaka vitukuu wetu pia kwahiyo ni lazima sisi wananchi tushirikishwe.

Tungekuwa na Bunge imara, tungeshirikishwa kupitia wawakilisha wetu (wabunge) , ila kwakuwa hatuna Bunge la aina hiyo(kwa mtazamo wangu), basi mkataba uwekwe wazi kwa umma na wananchi tutoe maoni yetu kama mradi huo uanze au vinginevyo.

Kamwe tusiwaachie wanasiasa waaamue peke yao jambo kubwa na nyeti kama hili hasa ukizingatia wanasiasa wetu wmekosa msimamo katika mambo nyeti kama haya. Zaidi wao huangalia watawala wameegemea upande gani na wao huunga mkono mawazo yao.

Kujadili huu mradi pasipo kujua nini hasa kimo katika huo mkataba huku wengine wakiupinga na wengine wakiutetea,ni uwendawazimu na ujinga mtupu na zaidi ni kupotezeana muda.

Bila shinikizo, tutajadili wee halafu tutachojadili hakitabadilisha kitu chochote, na mwisho wa siku, wataingia makubaliano wanayoyajua wao huku sisi tukibaki kuomba Mungu mkataba uwe fair kwa pande zote( kelele zote hizi zitakuwa ni sawa na kelele za chura ambazo hazimzui Tembo Kunywa maji).

Hivyo, natoa wito wa kufanyika maandamano ya amani kutaka uwazi juu ya mkataba huu vinginevyo tukubali matokeo hapo baadae.

Kumbukeni ya gesi ya Mtwara na maneno mazuri ya watawala wakati ule- Tanzania ya uchumi wa gesi.
 
Unajifurahisha tu, bandari ya Bagamoyo itajengwa tu na tutalipa hilo deni la 10bn USD hadi wajukuu na vitukuu huko, tulia mama asiye na vision uliyekuwa unampigia vigelegele atunyooshe wote nchi nzima.
We endelea kutetea CCM iliyotufikisha hapa.
 
Kuweka wazi mkataba siyo jambo rahisi kwa sababu za kibiashara muhimu kamati ya bunge ya miundo mbinu inaweza kuupitia kwa niaba yetu na pengine washirikishe jopo la wanasheria maarufu wakiwemo viongozi wa dini waangalie maslahi ya nchi.
 
hana lolote huyo naye ni nyumbu wahed tu.

kazi yao kubwa ni kupiga nduru"MATAGA,MATAGA,MATAGA"
sasa mama anaupiga mwingi mpaka anarenga goli la nyumbani,wanashindwa kumwelewa anaupiga kushinda au kushindwa!!!
Nyumba ni nyie mliotufikisha hapa huku mkienda kama kuku aliekaatwa kichwa.

Hata kwenye gesi ya Mtwara mlikuwa kama vipofu matokeo yake leo hii mnakuja kutuambia gesi hii ni ya mabeberu wakati mlikuwa mnashangilia na kugonga meza.

Pathetic and hopeless creatures!
 
Kuweka wazi mkataba siyo jambo rahisi kwa sababu za kibiashara muhimu kamati ya bunge ya miundo mbinu inaweza kuupitia kwa niaba yetu na pengine washirikishe jopo la wanasheria maarufu wakiwemo viongozi wa dini waangalie maslahi ya nchi.
Wakati magufuli anaukataa hadharani alianisha japo kwa mdomo,mapungufu yaliyopo mule.

Sijui ni nani alitafuta mwekezaji yule,na kwa lengo gani!

Trillion 21 tsh ni pesa nyingi sana mtu kuwekeza halafu asiweke mazingira ya hiyo pesa kurudi.

Magufuli ali sound logically zaidi.

Bado ukweli wa uwekezaji huo una maswali mengi sana.
 
Toa hizi stress zako hapa!

Wanaoshangilia huo mradi humu si nyie michadema mkifikiri kuna mtu mnamkomoa?

Unajiona akili kumbe mjinga tu

Toa sababu za kueleweka pia faida na hasara kwa mradi wa bandari ya bagamoyo.

Bavicha umewatoa wapi ..... punguani wewe
 
Unajiona akili kumbe mjinga tu

Toa sababu za kueleweka pia faida na hasara kwa mradi wa bandari ya bagamoyo.

Bavicha umewatoa wapi ..... punguani wewe
Lowasa alikuwa waziri mkuu na akasema katika kipindi cha kampeni kupitia UKAWA ya wakati huo kabla haijaharibiwa na akina amstwrdm kwamba akiwa rais huo mradi agavunja mkataba wake maana hauna maslahi kwa nchi.

Magufuli akiwa rais akisema amesitisha huo mradi kwa sababu kuna vipengele ni mzigo kwa taifa na akavitaja.

Wote hao ni viongozi wa kitaifa na walipinga huo mradi!

Wewe mbugilambugila una kipi cha kusaport huo mradi zaidi ya chuki zako za kijinga ukifikiri unamkomoa Magufuli?
 
Lowasa alikuwa waziri mkuu na akasema katika kipindi cha kampeni kupitia UKAWA ya wakati huo kabla haijaharibiwa na akina amstwrdm kwamba akiwa rais huo mradi agavunja mkataba wake maana hauna maslahi kwa nchi.

Magufuli akiwa rais akisema amesitisha huo mradi kwa sababu kuna vipengele ni mzigo kwa taifa na akavitaja.

Wote hao ni viongozi wa kitaifa na walipinga huo mradi!

Wewe mbugilambugila una kipi cha kusaport huo mradi zaidi ya chuki zako za kijinga ukifikiri unamkomoa Magufuli?

1. Umeeilewa mada?

2. Nini mchango wako katika maada hii

👇👇👇👇

Wapinzani na wanaharakati, andaeni maandamano ya amani kutaka uwazi wa mikataba ukiwemo wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo​

 
Back
Top Bottom