Wapinzani na wanaharakati, andaeni maandamano ya amani kutaka uwazi wa mikataba ukiwemo wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo

Kuweka wazi mkataba siyo jambo rahisi kwa sababu za kibiashara muhimu kamati ya bunge ya miundo mbinu inaweza kuupitia kwa niaba yetu na pengine washirikishe jopo la wanasheria maarufu wakiwemo viongozi wa dini waangalie maslahi ya nchi.
unaongea kuhusu bunge gani? bunge 100% ni ccm , wengi wao hata la 7 hawakumaliza
 
Huu mraddi wa bandari ya Bagamayo siyo mradi wa kuingia kichwa kichwa. Kama serikali haitakuwa makini Huu utaturudisha utumwani, watakao uidhinisha huu mkataba wanatakiwa wafahamike kwa majina ili majina yao yaingie kwenye historia ya nchi yetu.
 
huu mradi wa bagamoyo ni wizi mtupu, sidhani kaa mama samia anauelewa sawa, hii mradi ni hatari kwa taifa letu, ukome mara moja, uangaliwe umpya, mkataba uandikwe upya na uwekwe wazi kabla ya kutiwa sign
 
..kwanini mataga msiandamane kupinga mradi wa bagamoyo?

..kila jambo baya mnasubiri lipingwe na vyama vya upinzani?

..naona ktk hili mnakimbia wajibu wenu.
Hao wanasubiri "kupozwa" wafunge midomo, midomo yao ni strategy.
 
Kuweka wazi mkataba siyo jambo rahisi kwa sababu za kibiashara muhimu kamati ya bunge ya miundo mbinu inaweza kuupitia kwa niaba yetu na pengine washirikishe jopo la wanasheria maarufu wakiwemo viongozi wa dini waangalie maslahi ya nchi.
Sisi tunaiga nchi zilizotutangulia, hakuna nchi inayofanya hivyo hapa duniani/Afrika?

Kamati ipi ya bunge? Kwa wabunge wapi? Hawa waliopitisha mikataba ya gesi usiku kwa usiku? Hawa wanaoshangaa sheria kandamizi zilizopitishwa na bunge? Hawa walipitisha kodi za kizalendo zisizowagusa wao? Hawa walioukataa mradi wa bandari ya bagamoyo jana na leo wanautaka?

Viongozi wa dini wapi hao? Wale waliopokea zawadi ya Rugemalira? Au hawa waliopo bungeni leo?

Wanasheria wapi? Wakina Chenge wa vijisenti?

Waweke tu hadharani, wote tujue, kama inaliwa wote tujue inaliwa na hatuna cha kufanya baaaasi, tuendelee kuwa mazoba hivi hivi.
 
Ulichokiandika hapa ni tofauti kabisa na mada inayojadiliwa.
Hebu nenda KWA nyumbu wenzio kina yericko,malisa,na wale wanaharakati waliomaliza period zao wakiwa ccm kisha urudi kusoma kilichoandikwa
 
Jiwe ni muongo na lagahi kama shetani, usimuamini kwa lolote
 
We nae hujulikani unataka nini, pole Sanaa mkuu
 
Kile kipengele cha mchina kumiliki ardhi miaka 99 alichosema JPM kinatisha.mchina akifanikiwa tuu basi kwingine utakapo kopa utaambiwa nao wnataka ardhi kama ulivyompatia mchina au hatukupi mkopo je tutaishia wapi? sasa ni wangapi ambao tutakao kopa na kuwapa ardhi miliki miaka 99? je mwisho wa siku watoto wetu watamiliki kipande gani cha ardhi? hii ni lazima iwekwe wazi tujue mkataba huo utatuletea keki au bange?
 
Jiwe si mtu wa kuamini maneno yake,alisema tunajenga nchi kwa pesa zetu za ndani wakati ameacha deni kubwa sana
deni kubwa sana unalijua wewe,subiri utalisoma 2025.
 
We endelea kutetea CCM iliyotufikisha hapa.
Salary slip huyu mama anawapa chadema rushwa ndogo ndogo ,ili mkae kimya.Mara Mbowe arudishiwe pesa zake.Mara Lissu alipwe pesa zake.Kumbe anataka kutengeneza mikataba ya kifisadi kama JK.Niwaulize.Tanzania inaongoza kwa uzalishaji wa gesi.Je,mtwara na Lindi wanafaidika chochote.?Kwa sababu ya JK .
 
Kuna maswali mengi sana ya kujiuliza au kuuliza wanaoandaa kuuangalia upya mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo.
1. Je hii siyo furahisha Kikwete?
2. Je tunashindana kimikoa?
3. Wanaoungalia upya ni wepi? walioshiriki kuunda kipindi cha Kiwete au walioshiriki kuusimamisha kipindi cha JPM?
4. Kama ni wapya wametokea wapi na wana sifa gani?
5. Je vetting ilifanyika?
6. Kamati za Bunge zitahusishwa?
7. Vyuo vikuu vitahusishwa?
8. Mabalozi wetu kwenye nchi jirani zilizoingia mikataba kama hiyo ambayo leo hii inawatesa wanashiriki kutoa ushauri? Je wanafahamu lolote? Wamepewa kazi ya kutafuta undani wa mikataba iliyoshindikana?
9. Wastaafu serikalini wamepewa nafasi ya kutoa ushauri?
10. Watakao upitisha huu mradi wapo tayari kuweka majina yao wazi wananchi wawafahamu?
11. Kama viongozi wanaamini ni wenye manufaa kwa Taifa, Je serikali iko tayari kuuweka wazi mkataba wananchi watoe maoni yao?
12. Mkataba sensitive namna hii unaotishia kuturudisha utumwani, viongozi wako tayari kukubali pindi watokapo madarakani na ikathibitika kwamba mkataba hauna manufaa kwa nchi watakuwa tayari kuondolewa kinga zao na kukubali kufunguliwa mashtaka?
13. ....Je itafanyika tathmini makini ya kuonyesha itakavyoathiri bandari za Tanga, Dar, Mtwara? Kuonyesha kwanini si bora kuzipanua hizo zilizopo badala yake kupendekeza kuingia mkataba huu hatari?
14.......

Endelea
 
Ni kweli kabisa, ila kwa sasa kupata kibali itakua ngumu sababu tushatangaza uwepo wa wimbi la tatu la Covid -19
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…