Wapinzani wa nchi hii Uchaguzi huru na haki ni mpaka nyie mshinde? ACT- Wazalendo Konde mmeshinda kwa Tume gani ya Uchaguzi?

Wapinzani wa nchi hii Uchaguzi huru na haki ni mpaka nyie mshinde? ACT- Wazalendo Konde mmeshinda kwa Tume gani ya Uchaguzi?

Halafu wewe! Kwani chadema ya wakati ule unaweza kuilinganisha na hili genge la wahuni la sasa hivi?
Chadema ya dr slaa ilikuwa chama halisi cha kisiasa iliyojikita kwenye kupigania issues zilizokuwa zinawakabili wananchi na nchi kwa ujumla. Chadema ya sasa hivi haina chochote inachosimamia zaidi ya porojo, matusi na sasa ugaidi!
Uko sahihi 100%
 
Uchaguzi wowote ule unaotokana na nguvu ya kura kwenye sanduku la kura ndio halali ila sio hizi chaguzi za Tanzania ambazo kikundi flani Cha watu ndio kinaamua nani ashinde
 

Hivi upinzani wa nchi hii Uchaguzi huru na haki ni mpaka nyie mshinde tu | Je! ACT- Wazalendo Konde mmeshinda kwa tume gani ya Uchaguzi? Hongera Rais Samia kwa kusimamia demokrasia nchini​

"Hakuna kama Samia "​


Upinzani wa nchi hii umekuwa ukipoteza sifa ( credibility ) siku baada ya siku kutokana na kauli na matendo ya viongozi wake pale uadilifu na uaminifu wao unapolinganishwa na viongozi wa Chama cha Mapinduzi | Chama tawala yaani CCM ni kama mashariki na magharibi,

Upinzani wa Tanzania ukitaka kuwaamini hawaaminiki ukitaka kuwasikiliza wanapiga kelele,Ukiwahurumia wanasema umewaogopa kwa kifupi Wapinzani wa Tanzania hawajui wanataka nini,

Wakati Chadema wanasusia Uchaguzi kwa kisingizio cha Tume ya Uchaguzi Tanzania kuwa si huru wakati huohuo ACT Wazalendo wanashinda Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Konde huko Zanzibar kwa tume hii hii ya NEC|ZEC "nimazingaombwe haya"

Chaajabu zaidi,Upinzani wa Tanzania adui yake namba moja ni dola wala sio Umasikini wa Watanzania, wala sio maradhi ya Watanzania wala sio Ujinga wa Watanzania wao kutwa ni ligi na Rais, ligi na IGP, ligi na Msajili, ligi na spika kwa kifupi hawajui wanataka nini kwa nani na kwanini.

Kwa msiofahamu,Vyama hivi vimepoteza sana dira za vijana wengi kwa vijana hao kutokufahamu origin ya vyama hivyo kabla ya kujiunga, hebu fikiria Chadema ni matokeo ya Ugomvi baina ya Mwl Nyerere na Gavana Edwin Mtei ndio ikazaliwa Chadema wewe unayejiita kamanda Chama zao la mgogoro unadhani kitakufikisha au kitafika wapi kama sio migogoro kila siku? au Ugomvi wa Mbowe na Zitto ikazaliwa ACT-Wazalendo vyie Ngome ya Vijana kwanini mtumike kuchagiza gomvi za watu !? Is there any bright future kweli ACT | CHADEMA ?

Hivi kweli mtu aache kuchagua SGR toka Dar-Mwanza masaa 9,aache MW 2,115 toka JNHPP aache kuvuta Umeme kwa Tshs 27,000,aache chama kinachonunua ndege mpya 16,aache kuchagua chama kinachosomesha watoto wake wote bure,aache chama kinachotoa mikopo ya HESLB kwa wanachuo wote,aache chama kinachosimamia mikopo kwa riba ya 10%,aaache chama kinachosimamia bando kwa bei chee Africa nzima, aache chama kinachouza umeme chee Africa Mashariki yote ni $0.099/KWh leo achague hizo NGOs zenu kweli, don't waste your time bro's & sisters,

" Ukweli mchungu,Tanzania bado hakuna Chama mbadala wa CCM tukitegemee labda miaka ya 2060 "

#VIJANA NJOONI CCM TUMSAIDIE MAMA SAMIA KUJENGA NCHI TUNAJUA MNAZO NGUVU ACHENI KUCHAGIZA MIGOGORO YA WATU HUKO,

View attachment 1970343

MBUNGE MTEULE ACT-WAZALENDO

ILA TUME NI ILEILE ISIYOHURU-ZEC
Wewe hivi una akili gani?
Maana hata uandishi wako ni kama umetoroka mirembe
 
Uchaguzi wowote ule unaotokana na nguvu ya kura kwenye sanduku la kura ndio halali ila sio hizi chaguzi za Tanzania ambazo kikundi flani Cha watu ndio kinaamua nani ashinde
No, Mwogope Mungu Tanzania chaguzi ni huru sana shida maandalizi
 
Rudi kwenye shule ya propaganda, hapa ni kama unapaka upepo rangi. Hiki sio kizazi cha ccm, kuendelea kukaa madarakani kwa shuruti hakuwasaidii. Rejea idadi ndogo sana ya wapiga kura huko Ushetu ndio ujue hiki sio kizazi cha ccm. Maendeleo yanaletwa na kodi za watanzania sio mishahara ya wanaccm. Kama miradi ya maendeleo ni kigezo cha kukaa madarakani, makuburu wa Afrika kusini walipaswa kuwa madarakani mpaka leo.
Huyu jamaa ni sawa na samaki pono tu maana anaonekana bado yupo usingizini.
 
Halafu wewe! Kwani chadema ya wakati ule unaweza kuilinganisha na hili genge la wahuni la sasa hivi?
Chadema ya dr slaa ilikuwa chama halisi cha kisiasa iliyojikita kwenye kupigania issues zilizokuwa zinawakabili wananchi na nchi kwa ujumla. Chadema ya sasa hivi haina chochote inachosimamia zaidi ya porojo, matusi na sasa ugaidi!

Tusiende mbali hivi majuzi kabla ya kifo cha dhalimu cdm walikuwa wanasema kuna corona na hatua stahiki zichukuliwe, wakati huo ccm walikuwa wanafuata atakacho dhalimu kuwa hakuna corona na tutumie nyungu. Leo dhalimu yuko kuzimu ccm wote wanashawishi watu wachanje na hakuna anayeongelea nyungu tena. Niendelee?
 
Rudi kwenye shule ya propaganda, hapa ni kama unapaka upepo rangi. Hiki sio kizazi cha ccm, kuendelea kukaa madarakani kwa shuruti hakuwasaidii. Rejea idadi ndogo sana ya wapiga kura huko Ushetu ndio ujue hiki sio kizazi cha ccm. Maendeleo yanaletwa na kodi za watanzania sio mishahara ya wanaccm. Kama miradi ya maendeleo ni kigezo cha kukaa madarakani, makuburu wa Afrika kusini walipaswa kuwa madarakani mpaka leo.
Mkuu kwa mchezo mnaochezewa na Mbowe CCM Itaitawala TZ kwa mda mrefu sana. Sasa hv amepiga marufuku CDM kugombea uongozi wowote hii inazidi kuidhoofisha CDM. Na nyie wanachama wa CDM mlivyo mazombi mnashangilia. Kuficha ukweli wa hilo la kudhoofisha chama wanacheza mchezo wa kuigiza na CCM kuwa Mbowe anashitakiwa kwa ugaidi. Na nyie mmekomaaa Mbowe siyo gaidi Pasipo kujua huu ni mchezo wa kuigiza kati ya Mbowe na CCm ili kuunga mkono kauli ya kutoshiriki uchaguzi. Mbuzi sana nyie CDM. Hata akili ya kupambanua michezo ya kuigiza hamna.
 
Mkuu kwa mchezo mnaochezewa na Mbowe CCM Itaitawala TZ kwa mda mrefu sana. Sasa hv amepiga marufuku CDM kugombea uongozi wowote hii inazidi kuidhoofisha CDM. Na nyie wanachama wa CDM mlivyo mazombi mnashangilia. Kuficha ukweli wa hilo la kudhoofisha chama wanacheza mchezo wa kuigiza na CCM kuwa Mbowe anashitakiwa kwa ugaidi. Na nyie mmekomaaa Mbowe siyo gaidi Pasipo kujua huu ni mchezo wa kuigiza kati ya Mbowe na CCm ili kuunga mkono kauli ya kutoshiriki uchaguzi. Mbuzi sana nyie CDM. Hata akili ya kupambanua michezo ya kuigiza hamna.
Amka ww kumekucha maana utachafua godoro. Hapo unaona ndio umeniambia ukweli kana kwamba mimi siujui ukweli. Uza ubongo huo maana unakaa nao kwa hasara. Kama Mbowe anacheza mchezo na CCM, hivyo vyama vingine mbona havishindi?
 
Tusiende mbali hivi majuzi kabla ya kifo cha dhalimu cdm walikuwa wanasema kuna corona na hatua stahiki zichukuliwe, wakati huo ccm walikuwa wanafuata atakacho dhalimu kuwa hakuna corona na tutumie nyungu. Leo dhalimu yuko kuzimu ccm wote wanashawishi watu wachanje na hakuna anayeongelea nyungu tena. Niendelee?
Shida zaidi hata wanachadema wenyewe ambao ni wengi kuliko wana ccm wameshindwa kuzimaliza chanjo milion1 ambazo walizipigania kabla hata ya huyo wanayemwita dhalim. Hii inanipa picha kuwa chadema ni wachache sana na kura hawaibiwi
 
Amka ww kumekucha maana utachafua godoro. Hapo unaona ndio umeniambia ukweli kana kwamba mimi siujui ukweli. Uza ubongo huo maana unakaa nao kwa hasara. Kama Mbowe anacheza mchezo na CCM, hivyo vyama vingine mbona havishindi?
Mnachoweza ni matusi nyie vijana wa CDM. Mm ni mtanzania niliekuwa nikiuhusudu sana upinzani lakini kwa michezo hii ya kijinga ya upinzani na CCM nimelazimika kubakia neutral.

Unavyosemea vyama vingine ndiyo hivyo vyama vinavyoongozwa na Lipumba na Zitto. Ina maana tabia ya hao wawili huijui? Sumbua akili yako kufanya utafiti wako acha kufanyia kazi akili za watu wengine mkuu. Pia elewa wengi malipo katika vyama vya siasa shida Yao ni pesa na si vinginevyo. Slaa, kafulila, Nyalandu, Lowasa, Sumaye, nk ni mfano aina ya wanasiasa tulionao.
 
Anzisha chama mkuu ukiendeshe vizuri.
Mnachoweza ni matusi nyie vijana wa CDM. Mm ni mtanzania niliekuwa nikiuhusudu sana upinzani lakini kwa michezo hii ya kijinga ya upinzani na CCM nimelazimika kubakia neutral.

Unavyosemea vyama vingine ndiyo hivyo vyama vinavyoongozwa na Lipumba na Zitto. Ina maana tabia ya hao wawili huijui? Sumbua akili yako kufanya utafiti wako acha kufanyia kazi akili za watu wengine mkuu. Pia elewa wengi malipo katika vyama vya siasa shida Yao ni pesa na si vinginevyo. Slaa, kafulila, Nyalandu, Lowasa, Sumaye, nk ni mfano aina ya wanasiasa tulionao.
 
Shida zaidi hata wanachadema wenyewe ambao ni wengi kuliko wana ccm wameshindwa kuzimaliza chanjo milion1 ambazo walizipigania kabla hata ya huyo wanayemwita dhalim. Hii inanipa picha kuwa chadema ni wachache sana na kura hawaibiwi
Msimamo wa chama sio lazima uwe wa wafuasi wake. Una maoni zaidi?
 
Back
Top Bottom