Wapinzani wa Simba Washtuka, Washuka na Bordguards Kibao Airport

Wapinzani wa Simba Washtuka, Washuka na Bordguards Kibao Airport

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wapinzani wa Simba SC, Al-Ahli Tripoli kutoka Lybia, wamewasili nchini na tayari wameshuka kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakiwa na Bordguards kibao. Timu hiyo inajiandaa kukabiliana na Simba SC katika mechi ya marudio itakayochezwa Jumapili, Septemba 22, katika Dimba la Benjamin Mkapa saa 10:00 jioni.
1726729935746.png
Al Ahli Tripoli wamejipanga vyema na kuajiri timu ya usalama ya Watanzania itakayowalinda kuanzia uwanja wa ndege hadi siku ya mechi. Wamefanya makubaliano ya kuwajibika kwa usalama wao, na pia wameahidi kuwazawadia timu hiyo ya usalama ikiwa watatekeleza kazi yao kwa ufanisi.
Video: Mwanaspoti
 
Wapumbavu tu hao, tukiamua kuwadunda, tunawadunda vizuri tu, ila sisi wakubwa hatuna mpango wa kuwafanyia utoto kama waliotufanyia wao kule kwao..
Naona Kama Ma bodyguard ni wa bongo
 
Watakuwa ni mabodigadi WA Yanga😂😂. Hivi kale katabia Kao Ka kupokea wageni walikaacha?. Timu INA vituko!😂😂
Kuandika kitu ambacho huna uhakika nacho, ni dalili ya wazi kabisa ya umbumbumbu.

Halafu imekaaje hii!! Unajibu swali, na kuuliza tena swali hilo hilo kwa lengo la kupata jibu lingine!!
 
Wapinzani wa Simba SC, Al-Ahli Tripoli kutoka Lybia, wamewasili nchini na tayari wameshuka kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakiwa na Bordguards kibao. Timu hiyo inajiandaa kukabiliana na Simba SC katika mechi ya marudio itakayochezwa Jumapili, Septemba 22, katika Dimba la Benjamin Mkapa saa 10:00 jioni.
Al Ahli Tripoli wamejipanga vyema na kuajiri timu ya usalama ya Watanzania itakayowalinda kuanzia uwanja wa ndege hadi siku ya mechi. Wamefanya makubaliano ya kuwajibika kwa usalama wao, na pia wameahidi kuwazawadia timu hiyo ya usalama ikiwa watatekeleza kazi yao kwa ufanisi.
Video: Mwanaspoti
Jambo jema..watanzania wenzetu watapata rizki..ila kwa ustaarabu tusingewafanyia jambo lolote baya
 
Hata wangeshuka na VIFARU bado adhuma yetu iko pale pale aliyeua kwa upanga naye atakufa kwa upanga. 📌
 
Ni bodyguard siyo bordguard

Haya tuendelee...
 
Hao wabeba vyuma hawataruhusiwa kuingia maeneo yoyote ya viunga vya kwa Mkapa. Na kama wakikataa kuipa ushirikiano Simba ambaye ndiye mwenyeji wake, lolote baya likiwakuta Simba haitaweza kuhusishwa. Pona yao ilikuwa kuomba radhi hadharani na kuja kinyonge hata kama ni kinafki.
 
Wapinzani wa Simba SC, Al-Ahli Tripoli kutoka Lybia, wamewasili nchini na tayari wameshuka kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakiwa na Bordguards kibao. Timu hiyo inajiandaa kukabiliana na Simba SC katika mechi ya marudio itakayochezwa Jumapili, Septemba 22, katika Dimba la Benjamin Mkapa saa 10:00 jioni.
Al Ahli Tripoli wamejipanga vyema na kuajiri timu ya usalama ya Watanzania itakayowalinda kuanzia uwanja wa ndege hadi siku ya mechi. Wamefanya makubaliano ya kuwajibika kwa usalama wao, na pia wameahidi kuwazawadia timu hiyo ya usalama ikiwa watatekeleza kazi yao kwa ufanisi.
Video: Mwanaspoti
Ila caf lazima iangalie jinsi ya kutunga sheria ili kudhibiti vitendo vya kishenzi kwenye michezo ,mbona ujinga kama huu atuusikii huko uefa, caf imelala sana hawapo inovative
 
Woga wao tu Simba haina ushamba huo, hawa tutawashughulikia kwenye pitch kwa dakika 90.
 
Back
Top Bottom