Kwanza: Wao sera yao ni ya majimbo .hivyo miradi mikubwa ya kitaifa kwao haina maana maana miradi mikubwa ya kitaifa ni kwa ajiri ya taifa na siyo jimbo.Hivyo mtu kutoka majimbo ya sera ya chadema anaona wivu mkubwa kwa sababu anahisi kodi yake ingebaki jimboni Kwake ili inufaishe watu wake na siyo wengine .kwa maana hiyo miradi kama hiyo siyo keki ya taifa Bali keki ya jimbo.
Sera hii ya majimbo inapingana vikali na sera ya ujamaa ambayo inawaleta watu karibu katika umoja kama baba wa taifa Hayati Mwalimu kambarage Nyerere alivyotuacha tukiwa wa moja.wanaoshabikia sera ya majimbo ndani mwao lazima kuna ubinafsi.
Pili: Mashabiki wa chadema na wanaopinga miradi mikubwa ya taifa ni watu wa elimu ya chini,wasomi wa elimu ya dot com ambao Hawajui history ya Dunia kwa ujumla na historia ya Tanzania,lakini pia ni watu ambao kwa sasa Hawana Ajira, ni wale ambao wanataka upate leo ule leo,ni watu wa hapa hapa yani hata kutoka nje ya mkoa hawajawai kabisa.ukimwambia train ya umeme anajiuliza hivi hicho ni kidudu gani?hata kuona ndege ikitua hajawahi ona.
3. CHADEMA ilishaishiwa sera dhabiti za kuleta maendeleo ya taifa hili ,hivyo kwa sababu siasa Mahala pengine ni mchezo mchafu wakaona wawadanganye watanzania kuwa miradi hiyo haina maana kwa mtanzania wa hali ya chini.Lakini watu wa hali ya juu na wenye kujielewa ambao wao siyo nipate leo Nile leo,wanafurahia miradi mikubwa hii kwa sababu hata usipopata Matunda leo kesho au kesho kutwa watafurahia watoto wetu ana wajukuu wetu na vizazi vijavyo.
Kuwadanganya watanzania kuwa miradi mikubwa iliyojengwa na awamu ya Tano ni kete kubwa sasa kwa wa wapinzani. CCM msibwete maana huu ni uchaguzi mhimu sana kuliko Nyengine zote maana ni uchaguzi wa kuonyesha kati ya mjinga na mwelewa, mzalendo na msaliti,msomi mwelewa na smomi wa kukarili, mshamba na mtoto wa mjini,mkweli na muongo, nipate leo Nile leo na mwekezaje, mmjamaa na mbepari. CCM mkiruhusu kutoka madarakani hamtarudi milele maana historia itakuwa imeandikwa. mtakuwa mmeisaliti kazi nzuri mliyowatendea watanzania hasa kipindi cha awamu ya tano na kukubariana na ujinga kama siyo upumbavu.
Mimi binafsi (pamoja na u CCM wangu) nimewaelewa sana wapinzani, hususani Tundu Lissu.
Tundu Lissu anasema wazi wazi kabisa na tena kwa kurudia rudia mara kadhaa kwamba yeye hana shida na miradi mikubwa inayotekelezwa chini ya awamu ya 5 kwani ni wajibu wa serekali yoyote iliyo madarakani kufanya hivyo (ni sawa na kazi ya ATM (serekali) kuchukua pesa kwenye akaunti yako mwenyewe (kodi & tozo) - hii ni nyongeza yangu si maneno ya Lissu!).
Tundu anaendelea kutukumbusha kwamba hakuna rais wa awamu za huko nyuma tangu enzi za Mwalimu (RIP mzee wetu) ambaye hakuwahi kutekeleza miradi mikubwa. Mifano ipo mingi na sote tunaijua.
But (a very big "but" according to Tundu Lissu).......
1. chini ya awamu ya 5 hakuna uwazi katika matumizi ya fedha kwenye miradi hiyo kitu ambacho kinawafanya watu washuku uwezekano wa kuwepo kwa ufisadi kupitia ikulu yenyewe:
- tuhuma kwamba kuna unasaba kati ya muidhinishaji wa malipo na mlipaji
- kwamba kuna miradi mingine imetekelezwa kwa upendeleo wa kinasaba (nepotism) katika kutoa tenda
- kwamba gharama za matumizi kwenye miradi hii hazipo wazi (mimi naweza kuamini hili kwani kwani ATCL haikaguliwi na CAG)
- nk
2. chini ya awamu ya 5 kumeongezeka vitendo vya ukandamizaji kwa wale waliojitokeza kupinga hayo yaliyotajwa kwenye kipengele # 1 hapo juu:
- yeye mwenyewe Tundu Lissu amekuwa mhanga wa kufunguliwa kesi lukuki mahakamani
- "watu wasiojulikana", serekali imeshindwa kuwapata pamoja na kuwa na zana zote. Jaribio la kuuliwa kwake ni mfano hai
- watu kutekwa hovyo hovyo na kupotezwa
- watu kufunguliwa mashitaka yasiyo na kichwa wala miguu na wengine kuachiwa baada ya kukamuliwa pesa. convicts wengine wameishia hata kuteuliwa kwenye vyeo au kugombea nafasi kupitia CCM - kitu ambacho kinaacha maswali mengi kama kweli serekali inapinga ufisadi au inaogelea nao
3. ukandamizaji na unyanyasaji kama ulivyoainishwa hapo kwenye kipengele # 2 umepelekea udidimizwaji wa sekta binafsi kitu ambacho kimepelekea kuporomoka kwa uwekezaji, kodi na ajira kwa Watanzania
4. taasisi ya urais chini ya awamu ya 5 haikusimama vyema katika nafasi yake ya kuwa mfariji na msaada wa Watanzania pale wafikwapo na madhira mbalimbali. Badala yake kumekuwepo na kauli za kejeli, masimango na kudhalilisha kwa Watanzania.
Yapo mengi, lakini kwa leo wacha niishie hapo.
Wakatabahu.... Ijumaah Kareem!