Wapo Watanzania wapambanaji lakini hawajafanikiwa kwasababu ya kurogwa na ndugu au majirani zao

Watu kukutoa roho ni dk sifuri tu
 
Kuna hii kauli umeisema


"Mimi mwenyewe niliwahi kufungua duka la bidhaa mchanganyiko, nikawekeza mamilioni. Lakini cha kushangaza, mauzo kwa siku yalikuwa shilingi elfu 20, elfu 30, mara chache elfu 40. Watanzania wana wivu na uchawi mwingi sana. Kama hujui namna ya kuwakabili, hutafanikiwa hata uwe na juhudi na ubunifu kiasi gani.."



Mkuu,Uliwezaje kujua uchawi ndio sababu pia ulifanyaje ili ku-solve
 
Kuna jamaa bush flan aliuziwa ndinga na mzungu rafiki yake.Ila mzungu alikua jiji flani kaskazini huko,ikabidi jamaa atume dereva wa palepale bush akaifate ndinga.Kuna raia wakampigia dereva simu akiwa njiani anarudi kuwa sijui kama hiyo ndinga itafika salama.Kweli ndinga ikapiga chini ikaja inavutwa hadi gereji.Ikaitengenezwa halafu usiku mmoja kabla jamaa hajaichukua gereji,fundi akaenda kupigia misele viwanja vyake akazinguana na wahuni wakaivunja vioo,akiwa anakimbia msala wa wahuni agonga mtu akafa.Fundi akala kona mkoa mwingine.Ndinga ikaenda polisi
 

Wachawi ni wale wanaokujua. Mtu baki au mpita njia hawezi kukuloga. Yule unaye msaidia mara kwa mara muangalie sana.
 

Hayo ni mauza uza
 
Kuna kajiukweli fulani ila sidhani kama ni ndugu labda washindani
Mtu wa kwanza kunukuliwa kifo chake, amenukuliwa kwenye Biblia.

Ni Habili mdogo wake na Kaini (yaani toka nitoke)

Chanzo cha kifo, wivu wa baraka.

Yaani Habili alibarikiwa na Mungu, Kaini hakubarikiwa, akaona wivu.

Kama hicho kisa huwa unakipitapita tu ukidhani hakina maana rejea mstari huu

1 Wakorintho 10:11
[11]Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

Niendelee na mifano ya ndugu kuoneana wivu na kuangushana iliyopo ndani ya Biblia?

Nimechoka, kasome mwenyewe kisa cha Yusufu mtoto wa Yakobo kuanzia sura ya 37 ya kitabu cha Mwanzo.
 
Hahaha! Watu wa jadi kutoka vijijini wakienda kununua gari mbali kwanza hawaagi. Pili, wanaenda wakiwa wamejipanga. Wanaifunga tunguri na kurudi nayo vijijini salam salminj
 
Omba haya mambo ya kurogwa uyasikie kama story namna hii yakikukuta ni zaidi ya mateso. Sisi tuliorogwa tunayajua vizuri sana.
Kuna watu wana bahati miili yao haijaguswa ila siku ukinyooshwa wa leo sio wa jana, utasikia alipigwa stroke yule kijana
 
Hiyo ni imani ya hovyo ,hakuna anayeweza kukurudisha nyuma ...Hakuna ndugu Yako anayekuroga ..

Ukishaanza kuamini hayo mambo basi unakuwa kama zombie.
Hakika,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…