Waraka wa Marehemu Chacha Wangwe na Hatma ya Siasa za CHADEMA

Waraka wa Marehemu Chacha Wangwe na Hatma ya Siasa za CHADEMA

Nashukuru ushuzi.1 sikuwa na issue juu ya jamaa...ila nasikia jamaa ana form 6 tu...ni kweli?
 
Utangulizi :

Jarida hili la Mheshimiwa Chacha Zakayo Wangwe lina sehemu
tatu. Sehemu ya kwanza litaweka bayana na kufafanua sababu
za mimi kuchafuliwa kisiasa na baadhai ya viongozi wa ngazi
za juu za Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, na
sehemu ya pili itaonyesha baadhi ya maswali ya msingi
niliyopata kuuliza Bungeni na majibu yake na sehemu ya tatu
itakuwa na michango mbalimbali niliyopata kuchangia kwa muda
wa miezi miaka miwili na nusu.

Lengo hasa la Jarida hili ni kumwelewesha Mtanzania na
hususan MWANADEMOKRASIA juu ya tuhuma zilizoelekezwa kwangu
kwa lengo la kunichafua kisiasa huku viongozi wa CHADEMA
wakidai kukisafisha chama jambo ambalo si kweli na ni
kampeni chafu zilizoandaliwa na baadhi ya viongozi wa Chama
na kuwarubuni wajumbe 31 wasiokuwa wanademokrasia na
kunipaka matope ya siasa zao zisizo na hata chembe ya
Demokrasia.

Nasema hivi nikijua wazi kwamba, CHADEMA kama chama
kinaendeshwa kwa katiba na kwa wakati huo huo kikiwa
kinaendeshwa kidikteta na kauli za NDIYO MZEE.
Ninajua wazi kwamba, viongozi wa sasa wa chama changu
wanatofautiana sana na viongozi wa mwanzo wakati CHADEMA
ikianzishwa kwani wanatofautiana kiitikadi, kisera na hata
kimtazamo.

Kwa mfano, mzee Mtei alikuwa akikieneza chama hasa vijijini
miaka ya 95 kwa kutumia magari chakavu na alifanikiwa kwa
kiasi kikubwa kuwashawishi wananchi na wakijua kuwa CHADEMA
si chama cha mjini, na hapa ndipo mwanzo wa CHADEMA kuwa
Chama Tawala kule Tarime hadi sasa. Ila katika uongozi huu
wa kizazi kipya basi kila kitu kinaenda kwa kauli za
“Mheshimiwa Mwenyekiti kasema ” na matumizi mabaya huku
ufisadi ukikitafuna chama kwa matumizi hewa na kwa kigezo
kuwa eti wanajilipa madeni ya Kampeni.

Nililia sana juu ya matumizi ya helkopta katika kampeni
lakini nikaanza kuonekana kuwa mini ni mbaya. Binafsi
sikuona sababu za Chama kutumia helkopta ilhali bado
wanachama wa vijijini hawakijui chama wala sera zake huku
viongozi wa wilaya na mikoa wakishindwa hata kutoa durufu
(photocopy) za viepeperushi vya chama kwa kukosa ruzuku. Hii
si sawa.

SEHEMU YA KWANZA

Sababu za baadhi ya Viongozi wa CHADEMA kuamua kunichafua
kisiasa.
Baadhi ya Kampeni za chini chini dhidi yangu, tarehe 28 na
29 Juni 2008 katika kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika
Dodoma ambacho kiluhudhuriwa na wajumbe 31 kiliridhia mimi
kuondolewa kwenye wadhifa niliokuwa nao ndani ya chama kama
Makamu Mwenyekiti kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na
kutuhumiwa kuwa navujisha siri za chama kwa CCM. Binafsi
kwangu kama mwanasiasa wa kiwango cha juu ni pigo kubwa sana
kisiasa kuchafuliwa na watu 31 tu ndani ya chama.

Ninachokiamini hapa ni kwamba, kutokana na msimamo wangu wa
siku nyingi hata kabla sijawa makamu mwenyekiti CHADEMA,
ndiyo sababu rasmi ya kupigiwa kampeni na baadaye kura za
kutokuwa na imani na mimi kwa taarifa nilizo nazo ni kwamba
anaandaliwa Dr. Slaa kushika nafasi hiyo. Hapa ikumbukwe
kuwa Mke wa Dr. Slaa ni diwani kupitia CCM hivyo kuna
uwezekano wa sera za chama zikavuja kupitia Mama huyu katika
njia mbalimbali.

Ofisi ya Katibu Mkuu (Ofisi ya Slaa) ndiyo ya kwanza
kunituhumu kuwa nawaingilia majukumu yao katika suala zima
la matumizi mabovu ya fedha za ruzuku ya chama. Chama hupata
zaidi ya milioni 60 kila mwezi. Ni fedha nyingi sana
kukijenga chama kama zikipata mipango mizuri na kuachana na
matumizi mabovu kama matumizi ya helkopta kwenye kampeni
kama ilivyotokea kwenye chaguzi zetu pamoja na baadhiya
viongozi kudai kuwa wanajilipa madeni waliokikopesha chama
wakati wa kampeni za 2005.

Mhe. Philemon Ndesamburo Mbunge wa Moshi Mjini inadaiwa kuwa
anakidai chama milioni 100 alizokopesha wakati wa kampeni za
2005.

Mhe. Philemon Ndesamburo Mbunge wa Moshi Mjini inadaiwa kuwa
anakidai chama milioni 100 alizokopesha wakati wa kampeni za
2005, Freeman Mboe ambaye hadi sasa ni Mwenyekiti wa chama
changu katika ngazi ya Taifa naye kwa taarifa nilizo nazo ni
kwamba kila mwezi hulipwa shilingi milioni 10 ili kufidia
fedha anazodai kukikopesha chama ambazo ni zaidi ya milioni
500 katika kampeni hizo hizo na hadi sasa anaendelea kukidai
chama mamilioni ya shilingi.

Mimi nilipoonyesha wasiwasi juu ya madeni haya yasiyoisha,
ikaundwa tume ya kampeni za kutokuwa na imani na mimi.
Binafsi sijui kama viongozi wanaojiita makini kama kina Dr.
Slaa na Kabwe Zitto wangeweza kuusimamia ufisadi mkubwa kama
huu ndani ya chama huku wakiwa mstari wa mbele kuwafichua
mafisadi Serikalini.
Au ni kawaida kuwa Mganga hajigangi?
CHADEMA kuna ufisadi wa aina nyingi sana kuanzia uchapaji
bendera hadi manunuzi ya vifaa vya chama!

Katika ofisi ya Vijana nako kunanuka ufisadi kwani ni vijana
wachache sana ambao hupata nafasi ya kwenda nje ilhali
mikoani nako kuna vijana wanaohitaji kujifunza. Ofisi hii
ina watu maalumu wa kwenda kwenye Semina na Matamasha
mbalimbali. Na watu hao hupangwa na John Mnyika.

Pamoja na hayo, Kurugenzi hii inayoendeshwa na John Mnyika
imekuwa ikifanya hesabu za “Mbili mara Mbili toa nne”.
Nakumbuka matamasha mbalimbali yaliyowahi kuratibiwa na
Kurugenzi hii kwa kutumia fedha za chama yamekuwa hayana
maslahi yoyote kwa chama ….labda kwake mwenyewe kwani
itakumbukwa kwamba Kurugenzi ilizindua mfuko ulioitwa
Tumaini jipya Septemba 16, 2007 katika hafla ya wafanyakazi
vijana na akaunti ya Tumaini Jipya 01810301 NBC
ilifunguliwa.
Jumla ya shilingi milioni 6,176,500 zimekusanywa na shilingi
milioni 6,064,300 zimetumika kwa shughuli mbalimbali za
vijana ikiwemo gharama za hafla yenyewe. Hafla nyingine kama
hiyo ilifanyika Arusha.

Hafla hii ilifanyika tarehe 29 Machi, 2008 The New Polygon
Triangel Arusha na kuhudhuriwa na washiriki 67 mgeni rasmi
akiwa Mhe. Mzee Edwin Mtei. Jumla ya shilingi milioni
2,300,700 zilikusanywa na shilingi milioni 1,885,000.
Zimetumika kwa shughuli mbalimbali za vijana ikiwemo gharama
za hafla yenyewe. Sasa najiuliza, kulikua na mantiki gani ya
kutumia fedha za chama kiasi cha shilingi 6,064,300 na
kukusanya shilingi 6,176,500/=? Ni faida ya shilingi ngapi
ilipatikana kama ameamua kukiingiza chama katika kufanya
biashara ya matamasha?

Jingine, tangu nimekuwa mbunge Chadema na Baadaye Makamu
Mwenyekiti sijawahi kuandaliwa safari za kibunge ama za
kukiwakilisha chama ilhali kuna watu wasio na uwezo kiakili,
kifikra na hata nafasi za uongozi lakini waliandaliwa safari
za nje.

Chama kimefikia hatua ya kuwakilishwa kimataifa na watu
wasio na vigezo kwa ajili ya utawala mbovu! Siandiki haya
kwa kuwa nimeondolewa katika uongozi, hapana! Hizi ni
harakati zangu za muda mrefu juu ya utawala bora. Tazama,
wafuatao wamewahi kusafiri katika mataifa mbalimbali kwa
shughuli mbalimbali kukiwakilisha chama. Mhe. Suzan Lymo
(Mb. Viti maalumu) Cape Towan, Afrika Kusini kwa Mkutano wa
Interparliamentary Union. Susan pia amesafiri kwenda USA kwa
High Level meeting ya HIV/AIDs mwezi June, 2008.

Mhe. Zitto Kabwe, (Mb) alisafiri kwenda Berlin mara mbili
– Mhe. Zitto pia alisafiri kwenda Marekeani kwa wiki 3 kwa
mwaliko wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani pamoja na
Wabunge vijana toka dunia nzima ambako walipata nafasi ya
kutembelea majimbo mbalimbali ya Marekani.

Mhe. Mhonga Said (Mb – Viti maalum) alisafiri kwenda
Burundi kwa Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu. Mhe. Dr. Slaa
amesafiri kwenda Johannesburg, Windhoek na Manzini Swaziland
kwa vikao vya Kamati na Bunge la SADC. Dr. Slaa ni Makamu
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya InterParliamentary
Cooperation Committee ya Bunge la SADC. Mhe. Maulida Komu
(Mb. Viti Maalumu)
alisafiri kwenda Nairobi na pia Finland. Mhe. Ndesamburo
(Mb) alisafiri kwenda Australia kama Commissioner wa Bunge.

Wafuatao walisafiri kichama; Mhe. Mhonga Said (Mb – Viti
Maalum), Maulida Komu (Mb – Viti Maalum), Suzan Kiwanga
(Afisa Msaifizi Idara ya Uchaguzi na Kampeni) na John Mnyika
Mkurugenzi wa Idara ya Vijana) walisafiri kwenda Norway na
Sweden. Anthony Komu (Mkurugenzi wa Fedha na Utawala)
alisafiri kwenda Norway kwa mwaliko wa Centre Party, Mhe.
Balozi Ngaiza (Mjumbe wa heshma wa kamati kuu wa kuteuliwa
na Mwenyekiti), John Mnyika (Mkurugenzi katika Ofisi ya
Vijana), John Mrema (Afisa katika Kurugenzi ya Halmashauri
na Bunge), walisafiri kwenda Windhoek Namibia kwa Mkutano wa
Dua, na Mhe. Kimesera (Katibu Mtendaji wa kuteuliwa na
Mwenyekiti), Suzan Lymo (Mb) Viti maalum, na John Mrema
walisafiri kwenda Kampala, Uganda kwa Mkutano wa Dua.

Ndugu Regia Mtema (Afisa katika Kurugenzi ya Vijana)
alisafiri kwenda Malawi kwa Mkutano wa NIMD.
Mama Naomi Kaihula (Mkurugenzi katika Idara ya Wanawake) na
Regia Mtema walisafiri kwenda Finland kwa mwaliko wa Shirika
la Demo Finland. Johna Mrema, Msafiri Mtemelwa na Happiness
Mwaipopo (Sina hakika kama ni Mwanachama) walisafiri kwenda
London/Uingereza kwa mwaliko wa Conservative Party/WFD
wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Mhe. Benson Kigaila
(Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Mafunzo) alienda Zimbabwe
katika uchaguzi uliofanyika 27 June, 2008 kupita Ofisi ya
Msajili wa Vyama.

Suala la ukabila ni jambo ambalo halihitaji kupingwa kwani
asilimia karibu 85 ya viongozi wa CHADEMA wametoka katika
mikoa ya Kilimanjaro na Arusha pamoja na kwamba baada ya
mimi kulishupalia jambo hili wameanza kubadilisha majina.

Wapo wanachama kama mimi ambao nao wakipewa nafasi za
uongozi ndani ya chama hiki watafanya vizuri zaidi ya hawa
na wengine ambao ni Jobless! Pengine niweke wazi hapa kuwa,
mimi ni kiongozi shupavu nisiye kuwa na hata chembe ya woga
katika kuteta na kusimamia haki za mwanachama wa CHADEMA
tena nisiyependa siasa za kisanii.

Ukweli huu ndio uliowafanya kina Mbowe, Slaa kuwa mstari wa
mbele katika kupiga kampeni na baadaye kura ya kutokuwa na
Imani na mimi. Binafsi naamini katika chama cha siasa mtu
muhimu ni Mwanachama na si Mwenyekiti au Katibu. Hapa mimi
siandiki maneneo haya kukufanya udhani kuwa nataka kuwa
king’ang’anizi kwenye wadhifa niliovuliwa, la hasha bali
napenda upate picha halilisi ya uendeshwaji wa Siasa ya
CHADEMA na kisha uweze kugundua uhalisia wa mgogoro ulivyo.

Viongozi wa CHADEMA Makao Makuu wamening’oa kutoka katika
wadhifa niliokuwa nao kwa sababu zao binafsi na si sababu za
chama kama chama, na wanajitahidi kuzunguka mikoani kwa siri
kuendelea kunichafua kisiasa kuwa sifai. Kweli sifai kwa
wafuja ruzuku ya chama, kweli sifai kwa mafisadi ndani ya
chama ila nafaa kukiendesha chama katika ngazi ya taifa
katika nafasi yoyote na siku zote.

Nafaa kwa sababu nimefukuzwa kwa kusema ukweli hivyo
nikageuka mwiba kati kati ya majipu, nikatolewa. Ndiyo,
nafaa kwa sababu siko tayari kufanya kazi na watu waliozoea
kukaa ofisini kama mafaili! Nafaa kwa sababu mimi ni
mpambanaji, kamanda shujaa niliye tayari kuwajibishwa kwa
ajili ya kuwatetea WANADEMOKRASIA hususan WANACHADEMA nchi
nzima.

Kuliendesha Taifa kama Tanzania hakuhitaji siasa za kisanii,
fitina, na chuki. Kinachotakiwa ni nani abadilike alete
mabadiliko katika siasa ili aweze kukabidhiwa dola na alete
mabadiliko. Wananchi wamechoshwa na siasa zetu ndio maana
wanaziita siasa za kisanii. Wanahitaji mabadiliko. CHADEMA
maana yake ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo, lakini huku
wanakoelekea tayari uongozi wa Mbowe na Slaa wameiondosha
Demokrasia kwa kunitoa katika wadhifa wa umakamu Mwenyekiti
kwa kupiga kampeni ndogo ya wajumbe 31 tu! Tena huku
wakinituhumu kuwa navujisha siri za chama!!. Dhahama kama
hii siwezi kuivumilia hata kidogo na ni wazi kuwa hata
wanachama wetu hawajafurahishwa na jambo hili.

Mimi nilipokuwa kwenye ngazi hiyo ndipo fedha zilipoanza
kupelekwa mikoani kwa viwango halali, ndipo ukarabati wa
Makao Makuu ulifanyika. Niweke wazi hapa kuwa, jambo
lililonifanya niandike jarida hili si kuwashawishi Freeman
Mbowe na Slaa kunirudisha kwenye nafasi waliyonitoa kwa
matusi, la hasha! Lengo ni kuweka wazi kwa wanachama wajue
aina ya uongozi uliopo Makao Makuu ya Chama. Kama ni suala
la mimi kurudi katika nafasi hiyo ni mimi mwenyewe nikiamua
na kwa kutumia Demokrasia.

Ikumbukwe kuwa, Freeman ndiye aliyesema kuwa hataki kufanya
kazi na mimi na kutokana na UMANGIMEZA na Kauli za NDIYO
MZEE akapata kuungwa mkono na wajumbe 31 tu! Baada tu ya
mimi kutangazwa kuwa nimetolewa kwenye wadhifa niliokuwa nao
nilipata simu nyingi sana za wanachama na hata baadhi ya
watendaji Makao Makuu wakiniambia kuwa kama Mbowe hayuko
tayari kufanya kazi na mimi, wao bado wananihitaji katika
Uongozi Taifa.

Kuna mila ya kichagga kuwa, katika eneo la kazi/biashara,
ukimuona anayekusababisha ukose maslahi Fulani unatakiwa
kumuondoa kwa gharama yoyote! Na hili ndilo lililojiri
kwangu na mwenyekiti wangu.
Aluta Continue…………………..
Wangwe Chacha Zakayo,
Mbunge wa Tarime-CHADEMA

KAULI YANGU KWA MSOMAJI
Awali ya yote, nasikitika sana kwa maamuzi yaliyofikiwa na
wajumbe 31 kule Dodoma aidha, kwa hasira, chuki au majungu
na kuamua kuniondoa katika wadhifa niliokuwa nao wa Makamu
Mwenyekiti Tanzania Bara wakitumia kivuli cha Katiba ya
Chama.

Pili nimezidi kuumia zaidi pale nilipotuhumiwa kuwa eti
navujisha siri za Chama kwa CCM! Niliwapa siku Arobaini (40)
kuwaza kuthibitisha juu ya tuhuma hizo lakini wameshindwa
hadi leo! Inamaanisha kuwa walitumia tuhuma hizo ili kunitoa
kati yao ili nisiendelee kutetea ahadi za wanachama wa
CHADEMA na nisiendelee kupinga ubadhirifu wa fedha za chama.


Pengine kutokana na hasira, chuki na majungu hayo hayo
wakaamua kuzidi kunichafualia jina katika mkutano
uliofanyika Tanga kwa kunisema kuwa mimi ni mhuni. Hapa
sintakuwa na huruma wala urafiki na yeyote aliye mstari wa
mbele kunichafua kisiasa nitahakikisha nawafungulia mashtaka
na waweze kuthibitisha tuhuma hizo. Mpendwa msomaji, pamoja
na hayo ni vyema ukumbuke kuwa, uongozi wa CHADEMA Taifa
umeshindwa kukieneza chama hadi vijijini. Ni kwa ajili ya
majungu haya haya!.

Kimsingi, tusiposhikamana kwa sauti moja, lengo moja na kwa
msimamo, ni dhahiri kuwa chama cha mapinduzi kitaendelea
kushika Dola hadi Ukamilifu wa Dahari! Chama kisipokuwa
madhubuti hakitaweza kushika Dola hakiwezi kuaminika na
Wananchi. CHADEMA tufike mahali tugeuke, tujue tuna lengo la
kuiongoza Tanzania na si vinginevyo. Badala ya kulewa katika
kuwafichua mafisadi. Tumejisahau!.

Naamini kuwa, nguvu za umma ndiyo nguvu inayoweza kuleta
mabadiliko ya kweli.Naamini kuwa, katika chama chochote cha
siasa, mwanachama ndiye bora kuliko Kiongozi.Naamini kuwa
msingi bora wa chama hujengwa na watu makini.
Naamini pia baada ya kusoma Jarida hili ukiwa kama
mwanachama au Mwanademokrasia utaungana nami katika kupiga
vita UFISADI ndani ya CHADEMA wangwe.JPG
 
Mbowe ni mchawi balaa hata kule Musoma alituma watu kwenda kuwanunua wazee wa Mila wasifanye Tambuko juu ya kumuua Chacha, Wauaji wa Chacha wanajulikana mmojawapo ni Deus malya mwingine ni mbunge wa kasikazini na mwingine ni mbunge jijini Dsm na woote ni Wachaga na ni ndugu wa Mbowe.

ile damu ya kaka yetu itawala sana waliomuua bora hata wangemkata kama EL Kuliko kumuua na kuleta shida kubwa tarime na kwa watanzania.
 
Si kweli hata chembe Ile haikuwa ajali yale yalikuwa maigizo ya Deus Malya tu baada ya kutekeleza alivyoagizwa na Mbowe. Chacha wangwe alipigwa Risasi mdomoni kisha kijiko kikaibinua ile gari na kuiponda kwa juu kisha kikatikomea, Lema anaijua Sinema yooote lakini Rushwa ni Adui wa haki ndiyo maana kila kitu kiliminywa.

Lema, marya,mbowe na wanaharakati wote wanafiki na wauaji mda wenu utafika tu, auaye kwa upanga naye atauawa kwa upanga vile vile ili wenye ufahamu wamjue na kumuogopa Mungu aliye juu awezaye kupatiliza maovu hata kizazi cha nne. Subirini tu!
 
Hivi hii mikutano ya Chadema ifanyika kwa Pesa za baba zenu? mbona mna mawazo mgando hivyo?
 
Siku si nyingi wewe utaanza kuitwa msaliti pia!

Sikuwahi kuuona huu waraka kusema ukweli, lakini machache yaliyoandikwa ni yale yale ya kwenye ripoti ya Mwigamba

Mfano matumizi ya fedha za wadhamini kama Sabodo, ruzuku kutofika mikoani.

Chacha kazungumzia Mbowe kujilipa gharama za uchaguzi zaidi ya Tshs 200,000,000 mwaka 2005, kuna malalamiko ya kujilipa mil zaidi ya Mil 500 mwaka 2010, hope anatarajia zaidi ya Bil 1 mwaka 2015 kwa sababu trend imekuwa ni mara mbili ya uchaguzi uliopita.

Kazi tunayo! Inaniuma kuendelea kusubiri sana.

wauaji wa chacha wangwe ile damu ipo juu yenu tu mafisadi wa ndani ya chama nyie auaye kwa upanga atauawa kwa upanga pia.
 
Wewe mtoa mada umechelewa sana na kwa ushauri tu..acha maigizo. wewe sio chadema umetumwa ila umesahau kuwa watanzania wa sasa husoma hadi ndani kabisa ya bongo za maspy....timekujua wewe ni mjumbe mwaminifu wa CCM ila umechelewa kawaambie waliokutuma kua tumekushtukia...
 
Wewe hufukuzwi unarudishwa ulikotoka...acha hizo porojo za kale
 
Ila watu wa kali wa maigizo.. yaani mtu unajifanya eti unaumizwa na hali ya chama chako ili hali ukijua kabisa umetumwa kukiharibuu...maajabu haya
 
Wewe mtoa mada umechelewa sana na kwa ushauri tu..acha maigizo. wewe sio chadema umetumwa ila umesahau kuwa watanzania wa sasa husoma hadi ndani kabisa ya bongo za maspy....timekujua wewe ni mjumbe mwaminifu wa CCM ila umechelewa kawaambie waliokutuma kua tumekushtukia...

ndio ametumwa kama mlivyomtuma marya kumuua chacha wangwe, tambueni hamtadumu bila upanga kuwapitia tena ipo siku ile damu itawachanganya tu na kuwamaliza! Mafisadi wanaharakati na wauaji hamuwezi kuingia ikulu na laana ya kamanda wetu chacha Wangwe bado ipo juu yenu!
 
Wewe hufukuzwi unarudishwa ulikotoka...acha hizo porojo za kale

poa ila ukale unaouzungumzia ndio laana inayowala japo taratibu mtakuja kujua mmekwisha, na wewe unayetetea mauaji ni muuaji pia mwenye fikra za ndio mwenyekiti, ikulu hamuingii mkiwa na laana ya damu ya chacha wangwe mlioimwaga. Subirini.
 
Hizi hadithi pelekeni huko kwa mabwana zenu. Jambo hili tumeshasahau. Habari ya mjini kwa sasa ni repoti ya Human right watch kuwa Mbowe ni kiongozi was Upinzani bora zaidi barani Afrika (sio TZ Bali afrika kwa ujumla)
 
Wewe mtoa mada umechelewa sana na kwa ushauri tu..acha maigizo. wewe sio chadema umetumwa ila umesahau kuwa watanzania wa sasa husoma hadi ndani kabisa ya bongo za maspy....timekujua wewe ni mjumbe mwaminifu wa CCM ila umechelewa kawaambie waliokutuma kua tumekushtukia...

kwani siyo kweli kwamba Wangwe aliuwawa na Mbowe? au na wewe ni Mchagga?
 
Ukiangalia kwa kina na kuacha ushabiki usio na tija, waweza pata jibu la kwa nini ukombozi wa kweli uko mbali, maana kama hayo yanayosemwa ndio aliyonayo huyo anayeitwa kiongozi bora wa upinzani Afrika, haitostajaabisha wakipata madaraka wakawa zaidi ya hawa CCM wa sasa au sawa nao, yaani twahitaji kuzisafisha nafsi zetu kwanza kabla ya kuwafikiria wenzako.
 
Waraka wa Chacha Wangwe kabla hajafa kwenye ajali tata

UTANGULIZI.

Jumamosi, June 28 mwaka huu wajumbe kadhaa wa Kamati Kuu ya CHADEMA walidai kuwa wamesitisha Umakau Mwenyekiti wangu katika kikao kilichofanyika mjini Dodoma siku hiyo. Kesho yake Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe. FREEMAN MBOWE akaitisha mkutano wa waandishi wa habari na kutaja sababu za kunisimamisha uongozi.


Inatosha tu kusema kuwa sababu zote alizotoa ni za uzushi kama ile inayodai kuwa mimi navujisha siri za chama kwa viongozi wa CCM bila hata kutaja siri hizo, au kusema nimezitoa lini, wapi, na kwa kiongozi yupi?Kikao hicho kinachosemekana kunisimamisha uongozi, kilikuwa na wajumbe 31 ambao takribani nusu hawakuwa na uhalali wa kupiga kura kinyume cha katiba na kanuni za CHADEMA kwa vile walikuwa wameandaliwa kwa kazi hiyo. Wajumbe 7 walikataa kushiriki njama hizo.

Kufuatia jaribio hilo la kunivua uongozi kutokubalika kwa wanachama walio wengi wa CHADEMA , Mwenyekiti MBOWE na wafuasi wake wameendelea kuhaha kwa kuongeza sababu nyingine mbalimbali ili kuhalalisha njama zao. Sasa hivi wameingia hatua ya kuwashawishi wanachama wa Tarime eti wanifukuze uanachama.Kwa kuzingatia katiba, kanuni na taratibu za CHADEMA, nilichokifanya mimi baada ya kubaini njama zao ni kukata rufaa kwa Baraza Kuu la Chama, kupinga upotoshaji unaofanywa chini ya uongozi wa Mhe. MBOWE anayeonekana kutaka kuendesha chama kinyume na matarajio ya wanachama walio wengi.Hivyo basi zipo habari za uhakika kuwa kikao hicho cha Baraza Kuu hakitaitishwa ama kabisa, au kitacheleweshwa kwa makusudi, kwa visingizio mbalimbali ikiwemo kutokuwa na fedha za kukidhi gharama za kikao hicho.

Naomba nikiri kuwa ninakerwa sana na mtiririko mzima wa sakata hili linalozua mgogoro unaokiyumbisha chama. Ukweli ni kwamba mimi niligombea Umakamu Mwenyekiti nikiwa na agenda ya kufufua uhai wa chama kwa kukaripia vitendo visivyostahili katika kuendesha chama. Agenda yangu haijabadilika. Yote niliyoyasema wakati nagombea nafasi hii yanafahamika kwa wana CHADEMA wote.

Walikuwepo walioyalalamikia na walikuwepo walioyapongeza matamshi yangu hayo.Mwisho wa yote wana CHADEMA waliridhika kuwa ajenda yangu ilikuwa sahihi na hivyo wakanichagua kuwa Makamu Mwenyekiti. Hivyo basi hata kama ni kweli kuwa ulikuwepo mvutano wakati wa kampeni ile, lakini hilo ni jambo la kawaida katika uchaguzi. Nijuavyo mimi hayo yalitakiwa yawe si ndwele nasi tugange yajayo kwani wanachama walikwisha fanya uamuzi halali kupitia kura zao.

Baada ya kuingia kwenye wadhifa wa Makamu Mwenyekiti Taifa, nilifanikiwa kuzungumza na Mhe. MBOWE kuhusu mambo, hususan yale, niliyoyapigania wakati wa kinyang?anyiro kile na kumuomba tukae chini na kutafuta jinsi ya kufanikisha azma hiyo.Ni imani yangu kuwa waraka huu utawasaidia wanaCHADEMA wenzangu na watanzania wote kwa ujumla, kuelewa vizuri ukweli wa mambo niliyoyapigania kabla ya kuwa Makamu Mwenyekiti, na ninayoendelea kuyasimamia hivi sasa nikiwa Makamu Mwenyekiti, na inshallah nitakayoyatekeleza baadae kama Taifa Mwenyekiti wa CHADEMA.

Kimsingi mambo tunayotofautiana na Mhe. MBOWE ni haya yafuatayo:-

MATUMIZI YA RUZUKU
CHADEMA hupata ruzuku ya Tshs. 66,000,000 kwa mwezi (Milioni sitini na sita). Mimi nasema si haba hasa tukizingatia chama kilikotoka. Naamini kuwa kiasi hiki cha fedha kikisimamiwa vizuri kinaweza kukirahisishia chama kujieneza katika ngazi zote toka Tawi, Wilaya, Mkoa na Taifa.

Si kweli kwamba matatizo yote yatamalizwa na fedha hizi lakini basi hata ofisi za chama zinaweza kuwa hai nchi nzima kitu ambacho kwa sasa hakipo. Mahesabu yanaonesha kuwa mtaji wa laki moja (Tshs.100,000/=) kwa wilaya moja nchini inatosha, hivyo kwa Wilaya 126 kwa mwezi jumla yake ni Tshs. milioni 12 (Tshs. 12,600,000/= ) zinahitajika ( Wilaya 126 x 100,000 kila wilaya = 12,000,000/=)Hata tukisema tupeleke kiasi hicho kwa kila jimbo la uchaguzi jumla yake ni Tshs. Milioni 23 (Tshs. 23,000,000/=) kwa maana ya majimbo 213 x 100,000 = 23,000,000/=.
Mhe. MBOWE anasema hizo ni pesa nyingi sana kwa uimarishaji wa chama. Mimi nasema hapana, kiwango hiki kwa kila Wilaya au Jimbo la uchaguzi ni muafaka kwani haba na haba hujaza kibaba.Chini ya uongozi wa Mhe. MBOWE na wafuasi wake hawastaajabu kuwa kati ya Tshs. 374,144,000.40 zilizopatikana kama ruzuku katika ya Januari 1 na Juni, 30, 2008, Tshs. 350,000,000/= zilitumika Makao Makuu ya CHADEMA na Tshs. 25,000,000/= tu ndizo zilikwenda Wilayani kuimarisha chama.Mimi naona mgao huu unayatukuza Makao Makuu ya
CHADEMA isivyostahili wakati huo huo ukidhalilisha chama nchi nzima.

MADENI YA UCHAGUZI
Kufuatia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, Mhe. MBOWE alitufahamisha wanachama kuwa alikuwa anakidai chama US $ 181,949.00 sawa na Tshs. 218,338,546. Mpaka sasa chama kimekwisha mlipa Tshs. 175,000,000/=Baada ya kupata wadhifa wa Makamu Mwenyekiti, na kwa kuzingatia takwimu zionekanazo hapo juu katika kulinganisha matumizi ya fedha Wilayani na Makao Makuu niliamua kumshauri MBOWE asitishe kujilipa deni kutokana na fedha za ruzuku kwani siamini kuwa kulipa madeni yaliyopita kunaendana na utaratibu wa usimamizi wa fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa toka serikalini.

Mhe. MBOWE alichachamaa na ndipo nilipomshauri kuwa kama ni hivyo basi atuthibishie pesa hizo anazodai alikikopesha chama ziliingia kwenye akaunti gani ya CHADEMA, kupitia hundi ipi, na lini? Nilimuomba pia kutaja ni kikao gani cha chama kiliidhinisha matumizi ya fedha hizo kwani kama hakuna ushahidi wa maidhinisho, ni dhahiri kuwa matumizi hayo hayakudhibitiwa na chama na kwa mantiki hiyo kuyafanya kuwa matumizi binafsi ya Mhe. MBOWE.Vilevile, nilimueleza kuwa matumizi ya fedha hizo alizodai alikikopesha chama yalikuwa yakinuka harufu ya UFISADI.

Stakabadhi zote kuhusiana na matumizi hayo zilionesha kuwa gharama za aidha ununuzi na / au ukodishaji wa vifaa hivyo, hazikutofautiana na viwango wanavyolipishwa watalii kwa huduma kama hizo, kwa maana ya gharama ya juu sana.Na kwa kuwa hata baada ya kuwa Mhe. MBOWE amekwisha lipwa zaidi ya nusu ya deni alilodai kuikopehsa CHADEMA, vifaa vyote yakiwemo magari, vipaza sauti na kadhalika vimebakia kuwa mali yake binafsi, basi bila kumficha nilimueleza kuwa huko ni kukinyonya chama kwa kukigeuza kitega uchumi cha watu binafsi.Kuhusu suala la kulipa madeni kupitia ruzuku ya serikali, nilimuomba Mhe. MBOWE afuatilie kwa Msajili wa Vyama vya siasa ili tupate ufafanuzi kama kweli fedha za ruzuku ya serikali kwa vyama vya siasa, inaweza kutumika kulipia madeni ya viongozi wa vyama hivyo yatokanayo na uchaguzi ili CHADEMA isiathirike kisheria.

Niseme kweli hapa kwamba, kwa vile wanaCHADEMA wengi walinichagua kuwa Makamu Mwenyekiti, na hata mimi mwenyewe tulikuwa wagombea wa nafasi za ubunge, udiwani n.k katika uchaguzi wa mwaka 2005 ningefarijika sana iwapo na sisi tungerejeshewa angalau chochote cha kufidia gharama zetu, kwa maana kwamba kama chama kimeamua kurudisha gharama hizo kiwalipe wote badala ya kulipa madeni kwa wateule wachache.

UTEUZI WA WABUNGE WA VITI MAALUM
Naamini ukweli wa suala hili hauna mjadala. Kwamba Mhe. MBOWE na wafuasi wake walighushi orodha ya majina ya viti Maalum badala ya kupeleka yaliyopendekezwa na Kamati Kuu sio siri.

Naamini hata Mhe. MBOWE anakubaliana nami kuwa suala hili si moja ya siri anazodai nimevujisha! Yamesemwa mengi juu ya mtafaruku uliojitokeza kuhusu viti maalum hadi baadhi ya waasisi wa chama wakataka kujitoa na hivyo kumlazimisha Mwenyekiti Taifa ( FREEMN MBOWE) na Katibu Mkuu (DR WILBROAD SLAA) kukiomba radhi kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kwa kukiuka katiba, kanuni na maadili ya chama katika suala hili la kugushi viti maalum.

Ni ukweli ulio wazi kuwa kitendo hicho cha upendeleo bado kina iumiza taswira ya CHADEMA. Chama kinaonekana kuendekeza ujanja ujanja kiasi kwamba watu na binti zao, wakwe zao, shemeji zao, waume wenzao, wachumba wa shemeji zao, wake wenza na kwa kiwango kikubwa watu wa kabila moja ndiyo wamekuwa sura ya CHADEMA bungeni.Katika hili nilichoweza kumueleza Mhe. MBOWE ni kuwa chaguzi mbalimbali tangu za Mitaa, Ubunge na Urais zinakaribia ni vizuri tufanye bidii kusambaza nguvu zetu nchi nzima tuwe na mtaji wa kura maeneo mengi ili kashfa kama hii isijirudie. Hii ni kwa msingi kuwa chama kikijitanua kutakuwa hakuna sababu ya kuwaona watu wa eneo fulani tu kuwa ndiyo mhimili wa CHADEMA na hivyo zikitokea fursa itakuwa rahisi chama kuwakilishwa na mtandao wake mpana badala ya koo au kabila fulani.Sasa kwa kuwa kuimarisha chama kitaifa maana yake ni matumizi ya fedha, nalo hili likawa nongwa ingawa kwa mtazamo wa Makao Makuu kulipa madeni kwa wateule wachache si nongwa.

Cha ajabu ni kwamba Mhe. MBOWE hakukana kuwa hili la viti maalum na hata upangaji wa ajira kwa ukabila una leta athari mbaya kwa mustakabali wa CHADEMA

Katika maongezi yangu nae nilikuwa wazi nilipotahadharisha kuwa:

1. Watanzania wakiendelea kuona kwamba CHADEMA inaendeshwa kwa misingi ya kikabila hawatajiunga na chama chetu na tutakosa wafuasi.

2. Watanzania wakiona kuwa sisi tumeweka mbele ukabila kuliko utaifa hawatatupa madaraka na kutawala kwa kuhofia yale yanayotokea nchi jirani kama Rwanda, Burundi, Kenya na kadhalika ambako nafasi za raia wote zimehodhiwa na kabila moja na hatma yake watu wamechinjana kama kuku kwa kupinga hilo.
Pia nilimwambia kwamba, kwa jinsi sura ya uteuzi wa Wakurugenzi na watendaji wengine wa Makao Makuu inavyoonekana, sasa tayari chama chetu kimebatizwa jina la CHAMA CHA WACHAGA, na hii si kuwatendea haki raia wengine na makabila yao ambao wataonekana kama punguani kujihusisha na chama na ukabila.Yote haya ninayosema kuhusu ukabila, upendeleo na kadhalika sio dhana tu. Kufuatia malalamiko mengi yaliyokuwa yakisikika nchi nzima kuhusu masuala haya, Kamati Kuu ya CHADEMA ilikwisha unda Tume kutafuta ukweli wa mambo hayo. Tume hiyo ya watu watano iliongozwa na Mhe. Merky Lugendo Mziray ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA nayo imekwisha toa taarifa yake kwamba Makao Makuu ya CHADEMA yanatawaliwa na ubaguzi wa kikabila, kidini na kielimu.

UTENDAJI WA KIBABE
CHADEMA ni chama kilicho njia panda kwa sasa kutokana na utendaji wa kibabe wa Mhe. MBOWE. Ninafahamu jinsi vyama vingine vya upinzani hapa nchini kama vile NCCR ? Mageuzi vilivyoporomoka haraka haraka mithili ya nyumba ya mabua. Chama NCCR ? Mageuzi kilifikia mahali pazuri tu hadi watu wakaanza kufikiria kuwa kingekuwa chama mbadala kwa CCM.

kwa bahati mbaya uchu wa madaraka, ulafi wa ruzuku, na tabia za kimangimeza kwa pamoja vikakiathiri hadi kupoteza umaarufu wake.Na hata vyama vingine vya upinzani vina dalili hizo hizo japo kwa viwango vinavyotofautiana. Ila badala ya kujichunguza na kujua kasoro zetu, kila siku vyama vyetu, vimekuwa vikidai kuwa ni chama tawala ndicho kinachoviroga, kama ambavyo Mhe. MBOWE ameanza kuweweseka kupitia vyombo vya habari.Napenda kuthibitisha kuwa katika mgogoro unaopaliliwa sasa na Mhe. MBOWE ndani ya CHADEMA kutokana na ufisadi, ufuska, ulevi wa madaraka na umangimeza chanzo chake ni tabia yake ya kuendesha chama kibabe. Mathalan kumzuia Martin Mung?ong?o Mkurugenzi aliyechaguliwa kwa kura kutofanya kazi zake ndani ya chama, madai ya kupigana na watendaji wa chama ndani ya baa na vitendo vingine vya aina hiyo ni ushahidi tosha wa hulka hii.

Hadi sasa Mhe. MBOWE amefanikiwa kukizuia chama hiki kisifanye kazi ya siasa mkoa wa Dar es salaam kwa miaka minne.Ninavyoongea hivi sasa CHADEMA imekuwa ikikimbia vikao vya Democratic Union of Afrika (DUA), Muungano wa Vyama Vya Upinzani, uliofanikisha CHADEMA kujuana na Conservative Party ya Uingereza na Republican ya Marekani. Vyama dada hivi vyote vinaulalamikia uongozi wa CHADEMA kwa kufuja fedha ya misaada na kuwasilisha kwao risiti za kugushi, kama ilivyofanyiwa Conservative Party baada ya kutoa msaada wa Tshs. 78,000,000 kwa ajili ya ununuzi wa baiskeli na pikipiki ambazo hazikununuliwa.Katika mkutano wa Kamati Kuu ya CHADEMA huko Dodoma hivi majuzi tu, Mhe. MBOWE kwa kauli yake aliwatisha wajumbe kuwa alikuwa amethibiti uwezekano wowote wa wajumbe kujisikia huru kwa kutoa mawazo ambayo yangepingana na ajenda yake aliyoitoa ghafla kikaoni kunisimamisha Umakamu Mwenyekiti.

Mhe. MBOWE Alikifahamisha kikao kuwa alitoa taarifa kwa IGP, SAID MWEMA kuwa kuna wahuni ambao walitaka kuuchafua mkutano wake, naye IGP akahakikisha kuwa mkutano ule unalindwa kwa kiwango cha kushtua kama ambavyo hata vyombo vya habari vimethibitisha.Hayo ni baadhi tu ya mambo yanayobainisha Mhe. MBOWE ni kiongozi wa aina gani.

HITIMISHO
Kama nilivyokwisha sema hapo awali, sijaacha na sintoacha ajenda yangu ya kufufua uhai wa CHADEMA kwani ndiyo ahadi iliyofanikisha kuchaguliwa kwangu kuwa Makamu Mwenyekiti Taifa. Nilipopata wadhifa huo nilianza kuitekeleza ajenda hiyo kupitia mahojiano na Mwenyekiti MBOWE kuhusu matumizi ya ruzuku, madeni ya uchaguzi, uteuzi wa wabunge wa viti maalum, nafasi za ajira Makao Makuu, na kuhusu mwenendo wa chama Mkoa wa Dar es salaam.

Nilijikuta katika mvutano mkubwa kila nilipogusa eneo lolote katika haya. Nakiri kuwa kwa kiwango kikubwa sikuwa na uwezo wa kubadili mambo hayo yaliyokuwa yakiratibiwa kwa ukaribu na Mhe. MBOWE na wafuasi wake kwani sikupewa ushirikiano wa aina yoyote na chama pale Makao Makuu.

Ni vigumu kuamini, lakini ni kweli kuwa sikuwa na ofisi Makao Makuu, sikupewa vitendea kazi kama magari, vipaza sauti na/au vyombo vya habari, na sikuwahi kupata taarifa yoyote ya kiutendaji toka Makao Makuu.Kwa kuzingatia yote hayo, naomba nichukue fursa hii kuwashukuru kwa dhati wanachama wa CHADEMA mkoa wa Dar es salaam ambao kwa pamoja tulisimama kidete kufufua uhai wa chama hapa jijini. Niseme tu ushirikiano wao wa hali na mali uliniwezesha kushughulikia masuala muhimu ya kitaifa na kimataifa.

Rai yangu kwa wana CHADEMA na wale wote wanaokitakia mema chama chetu na nchi yetu kwa ujumla ni kwamba kazi ya kupigania demokrasia ya kweli ndani na nje ya chama, kukiepusha chama na vitendo vya ukabila, migogoro, ubadhirifu, umangimeza, ufisadi na ubaguzi wa aina yoyote bado inaendelea na nawaombeni mniunge mkono kwa hali na mali katika vita hii. Naamini tutashinda.Mungu Ibariki CHADEMA Mungu Ibariki TANZANIA Mungu Ibariki AFRIKA
 
Wakuu kwa wale ambao hamkupata kusoma ule waraka aliokuwa ameuandaa marehemu CHACHA WANGWE huu hapa, lengo lilikuwa zuri kusaidia chama kujisahihisha.

UTANGULIZI.

Jumamosi, June 28 mwaka huu wajumbe kadhaa wa Kamati Kuu ya CHADEMA walidai kuwa wamesitisha Umakau Mwenyekiti wangu katika kikao kilichofanyika mjini Dodoma siku hiyo. Kesho yake Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe. FREEMAN MBOWE akaitisha mkutano wa waandishi wa habari na kutaja sababu za kunisimamisha uongozi.

Inatosha tu kusema kuwa sababu zote alizotoa ni za uzushi kama ile inayodai kuwa mimi navujisha siri za chama kwa viongozi wa CCM bila hata kutaja siri hizo, au kusema nimezitoa lini, wapi, na kwa kiongozi yupi?Kikao hicho kinachosemekana kunisimamisha uongozi, kilikuwa na wajumbe 31 ambao takribani nusu hawakuwa na uhalali wa kupiga kura kinyume cha katiba na kanuni za CHADEMA kwa vile walikuwa wameandaliwa kwa kazi hiyo. Wajumbe 7 walikataa kushiriki njama hizo.

Kufuatia jaribio hilo la kunivua uongozi kutokubalika kwa wanachama walio wengi wa CHADEMA , Mwenyekiti MBOWE na wafuasi wake wameendelea kuhaha kwa kuongeza sababu nyingine mbalimbali ili kuhalalisha njama zao. Sasa hivi wameingia hatua ya kuwashawishi wanachama wa Tarime eti wanifukuze uanachama.Kwa kuzingatia katiba, kanuni na taratibu za CHADEMA, nilichokifanya mimi baada ya kubaini njama zao ni kukata rufaa kwa Baraza Kuu la Chama, kupinga upotoshaji unaofanywa chini ya uongozi wa Mhe. MBOWE anayeonekana kutaka kuendesha chama kinyume na matarajio ya wanachama walio wengi.Hivyo basi zipo habari za uhakika kuwa kikao hicho cha Baraza Kuu hakitaitishwa ama kabisa, au kitacheleweshwa kwa makusudi, kwa visingizio mbalimbali ikiwemo kutokuwa na fedha za kukidhi gharama za kikao hicho.

Naomba nikiri kuwa ninakerwa sana na mtiririko mzima wa sakata hili linalozua mgogoro unaokiyumbisha chama. Ukweli ni kwamba mimi niligombea Umakamu Mwenyekiti nikiwa na agenda ya kufufua uhai wa chama kwa kukaripia vitendo visivyostahili katika kuendesha chama. Agenda yangu haijabadilika. Yote niliyoyasema wakati nagombea nafasi hii yanafahamika kwa wana CHADEMA wote.

Walikuwepo walioyalalamikia na walikuwepo walioyapongeza matamshi yangu hayo.Mwisho wa yote wana CHADEMA waliridhika kuwa ajenda yangu ilikuwa sahihi na hivyo wakanichagua kuwa Makamu Mwenyekiti. Hivyo basi hata kama ni kweli kuwa ulikuwepo mvutano wakati wa kampeni ile, lakini hilo ni jambo la kawaida katika uchaguzi. Nijuavyo mimi hayo yalitakiwa yawe si ndwele nasi tugange yajayo kwani wanachama walikwisha fanya uamuzi halali kupitia kura zao.

Baada ya kuingia kwenye wadhifa wa Makamu Mwenyekiti Taifa, nilifanikiwa kuzungumza na Mhe. MBOWE kuhusu mambo, hususan yale, niliyoyapigania wakati wa kinyang?anyiro kile na kumuomba tukae chini na kutafuta jinsi ya kufanikisha azma hiyo.Ni imani yangu kuwa waraka huu utawasaidia wanaCHADEMA wenzangu na watanzania wote kwa ujumla, kuelewa vizuri ukweli wa mambo niliyoyapigania kabla ya kuwa Makamu Mwenyekiti, na ninayoendelea kuyasimamia hivi sasa nikiwa Makamu Mwenyekiti, na inshallah nitakayoyatekeleza baadae kama Taifa Mwenyekiti wa CHADEMA.



Kimsingi mambo tunayotofautiana na Mhe. MBOWE ni haya yafuatayo:-

MATUMIZI YA RUZUKU

CHADEMA hupata ruzuku ya Tshs. 66,000,000 kwa mwezi (Milioni sitini na sita). Mimi nasema si haba hasa tukizingatia chama kilikotoka. Naamini kuwa kiasi hiki cha fedha kikisimamiwa vizuri kinaweza kukirahisishia chama kujieneza katika ngazi zote toka Tawi, Wilaya, Mkoa na Taifa.

Si kweli kwamba matatizo yote yatamalizwa na fedha hizi lakini basi hata ofisi za chama zinaweza kuwa hai nchi nzima kitu ambacho kwa sasa hakipo. Mahesabu yanaonesha kuwa mtaji wa laki moja (Tshs.100,000/=) kwa wilaya moja nchini inatosha, hivyo kwa Wilaya 126 kwa mwezi jumla yake ni Tshs. milioni 12 (Tshs. 12,600,000/= ) zinahitajika ( Wilaya 126 x 100,000 kila wilaya = 12,000,000/=)Hata tukisema tupeleke kiasi hicho kwa kila jimbo la uchaguzi jumla yake ni Tshs. Milioni 23 (Tshs. 23,000,000/=) kwa maana ya majimbo 213 x 100,000 = 23,000,000/=.

Mhe. MBOWE anasema hizo ni pesa nyingi sana kwa uimarishaji wa chama. Mimi nasema hapana, kiwango hiki kwa kila Wilaya au Jimbo la uchaguzi ni muafaka kwani haba na haba hujaza kibaba.Chini ya uongozi wa Mhe. MBOWE na wafuasi wake hawastaajabu kuwa kati ya Tshs. 374,144,000.40 zilizopatikana kama ruzuku katika ya Januari 1 na Juni, 30, 2008, Tshs. 350,000,000/= zilitumika Makao Makuu ya CHADEMA na Tshs. 25,000,000/= tu ndizo zilikwenda Wilayani kuimarisha chama.Mimi naona mgao huu unayatukuza Makao Makuu ya

CHADEMA isivyostahili wakati huo huo ukidhalilisha chama nchi nzima.

MADENI YA UCHAGUZI

Kufuatia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, Mhe. MBOWE alitufahamisha wanachama kuwa alikuwa anakidai chama US $ 181,949.00 sawa na Tshs. 218,338,546. Mpaka sasa chama kimekwisha mlipa Tshs. 175,000,000/=Baada ya kupata wadhifa wa Makamu Mwenyekiti, na kwa kuzingatia takwimu zionekanazo hapo juu katika kulinganisha matumizi ya fedha Wilayani na Makao Makuu niliamua kumshauri MBOWE asitishe kujilipa deni kutokana na fedha za ruzuku kwani siamini kuwa kulipa madeni yaliyopita kunaendana na utaratibu wa usimamizi wa fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa toka serikalini.

Mhe. MBOWE alichachamaa na ndipo nilipomshauri kuwa kama ni hivyo basi atuthibishie pesa hizo anazodai alikikopesha chama ziliingia kwenye akaunti gani ya CHADEMA, kupitia hundi ipi, na lini? Nilimuomba pia kutaja ni kikao gani cha chama kiliidhinisha matumizi ya fedha hizo kwani kama hakuna ushahidi wa maidhinisho, ni dhahiri kuwa matumizi hayo hayakudhibitiwa na chama na kwa mantiki hiyo kuyafanya kuwa matumizi binafsi ya Mhe. MBOWE.Vilevile, nilimueleza kuwa matumizi ya fedha hizo alizodai alikikopesha chama yalikuwa yakinuka harufu ya UFISADI.

Stakabadhi zote kuhusiana na matumizi hayo zilionesha kuwa gharama za aidha ununuzi na / au ukodishaji wa vifaa hivyo, hazikutofautiana na viwango wanavyolipishwa watalii kwa huduma kama hizo, kwa maana ya gharama ya juu sana.Na kwa kuwa hata baada ya kuwa Mhe. MBOWE amekwisha lipwa zaidi ya nusu ya deni alilodai kuikopehsa CHADEMA, vifaa vyote yakiwemo magari, vipaza sauti na kadhalika vimebakia kuwa mali yake binafsi, basi bila kumficha nilimueleza kuwa huko ni kukinyonya chama kwa kukigeuza kitega uchumi cha watu binafsi.Kuhusu suala la kulipa madeni kupitia ruzuku ya serikali, nilimuomba Mhe. MBOWE afuatilie kwa Msajili wa Vyama vya siasa ili tupate ufafanuzi kama kweli fedha za ruzuku ya serikali kwa vyama vya siasa, inaweza kutumika kulipia madeni ya viongozi wa vyama hivyo yatokanayo na uchaguzi ili CHADEMA isiathirike kisheria.

Niseme kweli hapa kwamba, kwa vile wanaCHADEMA wengi walinichagua kuwa Makamu Mwenyekiti, na hata mimi mwenyewe tulikuwa wagombea wa nafasi za ubunge, udiwani n.k katika uchaguzi wa mwaka 2005 ningefarijika sana iwapo na sisi tungerejeshewa angalau chochote cha kufidia gharama zetu, kwa maana kwamba kama chama kimeamua kurudisha gharama hizo kiwalipe wote badala ya kulipa madeni kwa wateule wachache.

UTEUZI WA WABUNGE WA VITI MAALUM

Naamini ukweli wa suala hili hauna mjadala. Kwamba Mhe. MBOWE na wafuasi wake walighushi orodha ya majina ya viti Maalum badala ya kupeleka yaliyopendekezwa na Kamati Kuu sio siri.

Naamini hata Mhe. MBOWE anakubaliana nami kuwa suala hili si moja ya siri anazodai nimevujisha! Yamesemwa mengi juu ya mtafaruku uliojitokeza kuhusu viti maalum hadi baadhi ya waasisi wa chama wakataka kujitoa na hivyo kumlazimisha Mwenyekiti Taifa ( FREEMN MBOWE) na Katibu Mkuu (DR WILBROAD SLAA) kukiomba radhi kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kwa kukiuka katiba, kanuni na maadili ya chama katika suala hili la kugushi viti maalum.

Ni ukweli ulio wazi kuwa kitendo hicho cha upendeleo bado kina iumiza taswira ya CHADEMA. Chama kinaonekana kuendekeza ujanja ujanja kiasi kwamba watu na binti zao, wakwe zao, shemeji zao, waume wenzao, wachumba wa shemeji zao, wake wenza na kwa kiwango kikubwa watu wa kabila moja ndiyo wamekuwa sura ya CHADEMA bungeni.Katika hili nilichoweza kumueleza Mhe. MBOWE ni kuwa chaguzi mbalimbali tangu za Mitaa, Ubunge na Urais zinakaribia ni vizuri tufanye bidii kusambaza nguvu zetu nchi nzima tuwe na mtaji wa kura maeneo mengi ili kashfa kama hii isijirudie. Hii ni kwa msingi kuwa chama kikijitanua kutakuwa hakuna sababu ya kuwaona watu wa eneo fulani tu kuwa ndiyo mhimili wa CHADEMA na hivyo zikitokea fursa itakuwa rahisi chama kuwakilishwa na mtandao wake mpana badala ya koo au kabila fulani.Sasa kwa kuwa kuimarisha chama kitaifa maana yake ni matumizi ya fedha, nalo hili likawa nongwa ingawa kwa mtazamo wa Makao Makuu kulipa madeni kwa wateule wachache si nongwa.

Cha ajabu ni kwamba Mhe. MBOWE hakukana kuwa hili la viti maalum na hata upangaji wa ajira kwa ukabila una leta athari mbaya kwa mustakabali wa CHADEMA


Katika maongezi yangu nae nilikuwa wazi nilipotahadharisha kuwa:


1. Watanzania wakiendelea kuona kwamba CHADEMA inaendeshwa kwa misingi ya kikabila hawatajiunga na chama chetu na tutakosa wafuasi.

2. Watanzania wakiona kuwa sisi tumeweka mbele ukabila kuliko utaifa hawatatupa madaraka na kutawala kwa kuhofia yale yanayotokea nchi jirani kama Rwanda, Burundi, Kenya na kadhalika ambako nafasi za raia wote zimehodhiwa na kabila moja na hatma yake watu wamechinjana kama kuku kwa kupinga hilo.

Pia nilimwambia kwamba, kwa jinsi sura ya uteuzi wa Wakurugenzi na watendaji wengine wa Makao Makuu inavyoonekana, sasa tayari chama chetu kimebatizwa jina la CHAMA CHA WACHAGA, na hii si kuwatendea haki raia wengine na makabila yao ambao wataonekana kama punguani kujihusisha na chama na ukabila.Yote haya ninayosema kuhusu ukabila, upendeleo na kadhalika sio dhana tu. Kufuatia malalamiko mengi yaliyokuwa yakisikika nchi nzima kuhusu masuala haya, Kamati Kuu ya CHADEMA ilikwisha unda Tume kutafuta ukweli wa mambo hayo. Tume hiyo ya watu watano iliongozwa na Mhe. Merky Lugendo Mziray ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA nayo imekwisha toa taarifa yake kwamba Makao Makuu ya CHADEMA yanatawaliwa na ubaguzi wa kikabila, kidini na kielimu.


UTENDAJI WA KIBABE

CHADEMA ni chama kilicho njia panda kwa sasa kutokana na utendaji wa kibabe wa Mhe. MBOWE. Ninafahamu jinsi vyama vingine vya upinzani hapa nchini kama vile NCCR ? Mageuzi vilivyoporomoka haraka haraka mithili ya nyumba ya mabua. Chama NCCR ? Mageuzi kilifikia mahali pazuri tu hadi watu wakaanza kufikiria kuwa kingekuwa chama mbadala kwa CCM.

kwa bahati mbaya uchu wa madaraka, ulafi wa ruzuku, na tabia za kimangimeza kwa pamoja vikakiathiri hadi kupoteza umaarufu wake.Na hata vyama vingine vya upinzani vina dalili hizo hizo japo kwa viwango vinavyotofautiana. Ila badala ya kujichunguza na kujua kasoro zetu, kila siku vyama vyetu, vimekuwa vikidai kuwa ni chama tawala ndicho kinachoviroga, kama ambavyo Mhe. MBOWE ameanza kuweweseka kupitia vyombo vya habari.Napenda kuthibitisha kuwa katika mgogoro unaopaliliwa sasa na Mhe. MBOWE ndani ya CHADEMA kutokana na ufisadi, ufuska, ulevi wa madaraka na umangimeza chanzo chake ni tabia yake ya kuendesha chama kibabe. Mathalan kumzuia Martin Mung?ong?o Mkurugenzi aliyechaguliwa kwa kura kutofanya kazi zake ndani ya chama, madai ya kupigana na watendaji wa chama ndani ya baa na vitendo vingine vya aina hiyo ni ushahidi tosha wa hulka hii.

Hadi sasa Mhe. MBOWE amefanikiwa kukizuia chama hiki kisifanye kazi ya siasa mkoa wa Dar es salaam kwa miaka minne.Ninavyoongea hivi sasa CHADEMA imekuwa ikikimbia vikao vya Democratic Union of Afrika (DUA), Muungano wa Vyama Vya Upinzani, uliofanikisha CHADEMA kujuana na Conservative Party ya Uingereza na Republican ya Marekani. Vyama dada hivi vyote vinaulalamikia uongozi wa CHADEMA kwa kufuja fedha ya misaada na kuwasilisha kwao risiti za kugushi, kama ilivyofanyiwa Conservative Party baada ya kutoa msaada wa Tshs. 78,000,000 kwa ajili ya ununuzi wa baiskeli na pikipiki ambazo hazikununuliwa.Katika mkutano wa Kamati Kuu ya CHADEMA huko Dodoma hivi majuzi tu, Mhe. MBOWE kwa kauli yake aliwatisha wajumbe kuwa alikuwa amethibiti uwezekano wowote wa wajumbe kujisikia huru kwa kutoa mawazo ambayo yangepingana na ajenda yake aliyoitoa ghafla kikaoni kunisimamisha Umakamu Mwenyekiti.

Mhe. MBOWE Alikifahamisha kikao kuwa alitoa taarifa kwa IGP, SAID MWEMA kuwa kuna wahuni ambao walitaka kuuchafua mkutano wake, naye IGP akahakikisha kuwa mkutano ule unalindwa kwa kiwango cha kushtua kama ambavyo hata vyombo vya habari vimethibitisha.Hayo ni baadhi tu ya mambo yanayobainisha Mhe. MBOWE ni kiongozi wa aina gani.

HITIMISHO

Kama nilivyokwisha sema hapo awali, sijaacha na sintoacha ajenda yangu ya kufufua uhai wa CHADEMA kwani ndiyo ahadi iliyofanikisha kuchaguliwa kwangu kuwa Makamu Mwenyekiti Taifa. Nilipopata wadhifa huo nilianza kuitekeleza ajenda hiyo kupitia mahojiano na Mwenyekiti MBOWE kuhusu matumizi ya ruzuku, madeni ya uchaguzi, uteuzi wa wabunge wa viti maalum, nafasi za ajira Makao Makuu, na kuhusu mwenendo wa chama Mkoa wa Dar es salaam.

Nilijikuta katika mvutano mkubwa kila nilipogusa eneo lolote katika haya. Nakiri kuwa kwa kiwango kikubwa sikuwa na uwezo wa kubadili mambo hayo yaliyokuwa yakiratibiwa kwa ukaribu na Mhe. MBOWE na wafuasi wake kwani sikupewa ushirikiano wa aina yoyote na chama pale Makao Makuu.

Ni vigumu kuamini, lakini ni kweli kuwa sikuwa na ofisi Makao Makuu, sikupewa vitendea kazi kama magari, vipaza sauti na/au vyombo vya habari, na sikuwahi kupata taarifa yoyote ya kiutendaji toka Makao Makuu.Kwa kuzingatia yote hayo, naomba nichukue fursa hii kuwashukuru kwa dhati wanachama wa CHADEMA mkoa wa Dar es salaam ambao kwa pamoja tulisimama kidete kufufua uhai wa chama hapa jijini. Niseme tu ushirikiano wao wa hali na mali uliniwezesha kushughulikia masuala muhimu ya kitaifa na kimataifa.

Rai yangu kwa wana CHADEMA na wale wote wanaokitakia mema chama chetu na nchi yetu kwa ujumla ni kwamba kazi ya kupigania demokrasia ya kweli ndani na nje ya chama, kukiepusha chama na vitendo vya ukabila, migogoro, ubadhirifu, umangimeza, ufisadi na ubaguzi wa aina yoyote bado inaendelea na nawaombeni mniunge mkono kwa hali na mali katika vita hii. Naamini tutashinda.Mungu Ibariki CHADEMA Mungu Ibariki TANZANIA Mungu Ibariki AFRIKA
 
ha ha ha, tegemea matusi na vihoja

kwa sababu ya unafiki wetu na mahaba kwa tunavyovipenda, hakuna CDM mwenye akili za unyumbu atakayekuelewa hapa!

wanaoelewa ni wachache sana, aghalabu kuwakuta humu

Waraka wa chacha wangwe nido kiini cha tatizo CDM, CDM si taasisi, sio chama, sio watu

CDM ni mtu, ni kampuni ya mtu, aliyeweka ionekane kma ni chama; ni fanyabiashara moja ambalo limekusanya wanaojielewa na waisojielewa...linawatumia kwa manufaa yake!


pity
 
Back
Top Bottom