Adui mkubwa wa wakatoliki duniani pote ni waislamu.
sasa waislamu wameligundua hilo. sasa jino kwa jino
Adui mkubwa wa wakatoliki duniani pote ni waislamu.
sasa waislamu wameligundua hilo. sasa jino kwa jino
Mi shida yangu katika kuuelewa waraka huu ni pale unapooneka kuupinga ukatoliki. Kwani waraka huu umeandikwa kwa ajili ya kuchafulia jina wakatoliki? Maana hapa anayepingwa ni mkatoliki. Mkatoliki anaonekana mbaya katika waraka huu, swali langu ni kwamba kama mkatoliki ni mbaya, mbona muda wote huo waislamu hamkusema? Hii inaonekana kuwa ni wazi kwamba waraka huu unataka kuleta majibizano na kanisa katoliki, lakini walioandika wakumbuke kuwa nadhani kanisa katoliki halina haja ya kujibishana na wao kwa kuwa halina ugomvi na wao. Waislamu mulielewe hilo.
Mnaposema kuwa Nyerere ni Mbaya, nashindwa kuelewa kitu kimoja! Mbona hamkusema wakati wa uhai wake? Halafu, mbona Ali Hassan Mwinyi ni chaguo la Nyerere? Kwani Mwinyi si Muislamu? Je, Nyerere hakuwa na madaraka ya kumchagua mtu wa dini nyingine? Sasa kama alimchagua Mwinyi ni mbaya kwa Waislamu kivipi?
Kama Nyerere angekuwa mbaya, ingekuwaje leo tuna Rais Mwislamu, Makamu wake ni Mwislamu, Katibu wa Chama tawala ni Mwislamu, na viongozi wengi tu ni waislamu, hata Rais wa Zanzibar ni mwislamu, sasa waislamu mnaonewa vipi? Ubaya wa wakatoliki uko wapi?
Tena wakati tunapata uhuru, Waislamu walikuwa nyuma kielimu. Hilo halikuwa kosa la Nyerere. Nyerere alilikuta hilo. Akafanya kila mbinu kutoa elimu bure kwa Watanzania wote Waislamu included, sasa mnapomkashifu Nyerere mimi nashindwa kuwaelewa. Ni wapi Nyerere aliwakataza Waislamu wasiende shule au misikitini? Naomba mnisaidie.
Waraka unaelekea kuipinga serikali ya Rais Kikwete kama umeusoma vizuri. Tena unapinga pia utawala wa Ben. Sasa kama Ben angelikuwa hawapendi waislamu, Kikwete angekuwa Rais sasa? Naomba mnijibu. Sasa huo uonevu wa wakatoliki unatoka wapi?
Kumbukeni pia uhuru ulipiganiwa na watanzania wote bila ya kujali dini zao. Sasa isiwe nongwa kusema kwamba waislamu tu ndio waliopigania uhuru.
Mimi nawaheshimu sana ndugu zangu waislamu. Nadhani waraka wao uliandaliwa kwa haraka haraka. Ila maoni yangu ni kuwa kuna hoja ambazo zinatatanisha ndio maana hata inakuwa vigumu kwa BAKWATA kuukubali waraka huo, na ndio maana inakuwa vigumu vile vile kwa watu kuujadili kama vile walivyofanya kwa ule wa wakatoliki.
Kwa heshima na taadhima nilizo nazo kwa ndugu zangu waislamu, ninachofanya hapa ni kuonyesha ni jinsi gani mimi kama mtu wa dini nyingine ninavyouelewa waraka wenu. Ili mpate picha ya upande mwingine. Sina ugomvi na nyinyi ila tunaujadili tu waraka kiustaarabu bila matusi au kashfa. Naomba mnielewe kama vile nilivyowaelewa wakati mkijadili waraka wa wakatoliki. Naomba ndugu na rafiki zangu wa Kiislamu tuelimishane kama kuna sehemu niliyokosea au kutokuelewa vizuri. Asanteni sana nasubiri comment za kujenga na si za kubomoa. Sisi sote ni Watanzania hivyo lazima tuelewane! Tutaelewana tu kama tutakuwa na dialogue nzuri. Asanteni!
Ndio maana BAKWATA hawautambui, umeandaliwa na waislam feki kina Ponda na wenzake, waislam safi hawauungi mkono huo upuuzi.
Mwongozo huu wa kiislamu ni mzuri sana kwa watu makini na wenye kuipenda Tanzania, umeonyesha maeneo ya kipaumbele ya kufanyia kazi haraka kwa amani ya nchi! viongozi wa serikali inabidi wausome, na kuuzingatia. Anayeupinga ni mbaguzi na mnafiki asiyetaka kusikia ukweli . bravo shura ya maimamu.
Mwongozo huu wa kiislamu ni mzuri sana kwa watu makini na wenye kuipenda Tanzania, umeonyesha maeneo ya kipaumbele ya kufanyia kazi haraka kwa amani ya nchi! viongozi wa serikali inabidi wausome, na kuuzingatia. Anayeupinga ni mbaguzi na mnafiki asiyetaka kusikia ukweli . bravo shura ya maimamu.
Kwa sababu wa kikatoliki unalenga ubaguzi na wa kiislamu umeonyesha facts, facts ambazo ni muhimu kwa uhai wa taifa.Mnafiki ni wewe uliye pinga waraka wa wakatoliki lakini unausifia waraka wa waislamu.
Kwa sababu wa kikatoliki unalenga ubaguzi na wa kiislamu umeonyesha facts, facts ambazo ni muhimu kwa uhai wa taifa.
Kwa sababu wa kikatoliki unalenga ubaguzi na wa kiislamu umeonyesha facts, facts ambazo ni muhimu kwa uhai wa taifa.
hilo jina TUMAINI badilisha uwe majuto, pia nahisi unajifunza kusoma na kutumia computer kwani unatumia akili nyingi kutafuta key ya kubonyeza thats why unashindwea kufikiria vizuri!! nakushauri uwe unasoma uandike pembeni ktk paper ndo ucopy ktk pc yako!hapo utaandika lenye maaana
Tujikumbuke tulikotoka, mwaka 2007 na Dr Slaa.
BAADA ya serikali kufuatilia kwa kina tuhuma za ufisadi dhidi ya viongozi wa serikali zilizotolewa na Mbunge wa Karatu, Dk. Willibrod Slaa, imebaini ni za uzushi na upotoshaji wa makusudi wa ukweli...
Tamko la serikali lililotolewa jana jijini Dar es Salaam lilieleza tuhuma za Dk. Slaa zinalenga kujengea umaarufu vyama vya siasa vya upinzani kwa kudhoofisha umoja wa kitaifa.
Kwa ujumla, tuhuma za Dk. Slaa dhidi ya viongozi wa umma hazina ukweli wowote, bali zina lengo la kuchochea chuki dhidi ya serikali na kutaka kudhoofisha umoja na mshikamano wa taifa letu, ilieleza sehemu ya tamko hilo.
Septemba 15, mwaka huu, Dk. Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CHADEMA, akiwa na viongozi wa muungano wa vyama vya siasa vya upinzani, alitoa tamko hadharani linalowataja watuhumiwa wa ufisadi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Temeke, Dar es Salaam.
Miongoni mwa tuhuma zilizotolewa na Dk. Slaa ni ubadhirifu wa mali za umma dhidi ya taasisi mbalimbali kama Benki Kuu ya Tanzania (BoT), NBC, NMB, mikataba ya ubinafsishaji na ununuzi wa mali za umma.
Serikali imefafanua kuwa, waliotajwa kuingiza fedha za kigeni nchini na baadaye kulipwa na BoT, walikuwa wameagiza bidhaa kutoka nje ya nchi miaka ya 1980, ambapo BoT ilipokea malipo yao kutoka NBC.
Tamko hilo lilisema BoT ilishindwa kuwalipa kwa wakati, baada ya kupokea fedha hizo NBC kwa sababu haikuwa na fedha za kutosha za kigeni.
Tuhuma kwamba kulikuwa na shinikizo kwa kampuni ya Alex Stewart (Assayers) Government Business Corporation ya Washington, Marekani, kupewa kazi ya kukagua hesabu za kampuni za uchimbaji dhahabu, serikali ilisema si kweli.
Ilieleza kuwa kampuni hiyo ilipatikana kwa kuzingatia sheria na kanuni za ununuzi wa umma na hakukuwa na shinikizo lolote.
Juu ya rushwa katika mkataba kati ya serikali na Alex Stewart, serikali ilisema suala hilo liko mahakamani, hivyo haina uwezo wa kulizungumzia.
Kuhusu tuhuma za uuzaji wa rasilimali za taifa, ununuzi wa ndege ya Rais, ubinafsishaji wa NBC na NMB, serikali ilisema hazina msingi wala ushahidi wowote, bali zinajaribu kujenga mazingira ya kujipatia umaarufu usiostahili.
Serikali imetafsiri tuhuma hizo kuwa jaribio la kuwavunja moyo wananchi, kuhusu manufaa ya utekelezaji wa programu iliyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 na kama ilivyotafsiriwa katika bajeti ya mwaka 2007/2008.
Serikali inawahakikishia wananchi kuwa inapinga vitendo vya rushwa nchini kwa nguvu zake zote na msimamo wake ni thabiti kuhusiana na suala hili, ilieleza sehemu ya tamko hilo .