Warioba amewasilisha rasimu ya katiba au rasimu ya serikali tatu?

Warioba amewasilisha rasimu ya katiba au rasimu ya serikali tatu?

Takribani zaidi ya masaa matatu aliyotumia Mwenyekiti wa Mchakato wa Katiba Mpya, Jaji Joseph Sinde Waryoba kuwasilisha kile kinachoitwa(nasema ni kile kinachoitwa kwa vile sasa maana halisi ya Katiba Mpya haipo tena) Rasimu ya Katiba Mpya alitetea (na siyo kuwasilisha maoni ya wananchi) muundo wa Serikali tatu.

Watanzania wengi kutoka makundi mbali mbali wakiwemo Wakulima, Wafugaji, Walemavu, Watoto, Vijana, Wanawake, Wazee na mengine mengi wamebaki wameduwaa na kujiuliza maswali mengi kama kilichowasilishwa jana bungeni ni Rasimu ya Katiba Mpya au ni Rasimu ya namna gani ya Muundo wa Muungano unawafaa watanzania, hoja ambayo pasi na shaka ni kwa manufaa ya wanasiasa.

Jmbo kubwa ambalo watu wamebaki wakijiuliza ni namana ambavyo Waryoba alitumia nguvu nyingi kutetea hoja ya serikali tatu huku akijua kabisa katika mchakato mzima wapo watanzania tena wengi tu ambao ni waumini wa Serikali mbili na wengine akiwemo yeye mwenyewe ni auminini wa serikali moja.

Watu wanajiuliza Waryoba ambaye ni muumini wa serikali moja alishikwa na nini au kuna nini kimejificha juu ya msimamo wake katika serikali tatu na kusahau kabisa kugusia hata serikali moja ambayo yeye anaaamini ni nguzo imara ya Muungano?

Lakini kubwa ambalo Makungi ambayo jana yamesaulika kwenye hotuba ya Jaji waryoba yanajiuliza ni wapi watasimama kuhoji haki zao kwenye Katiba itakayopatikana wakati tangu mwanzo wameonekana kusahaulika?

Mytake: Iko haja kubwa kabisa ya Wabunge wa Bunge maalum la Katiba kujitazama upya kuhusiana na rasimu hiyo la sivyo kuna kila dalili kuwa Katiba inayokwenda kuandikwa ni kwa ajili ya Wanasiasa na watu kama akina Waryoba ambayo yawezekana kabisa kuna kitu wameahidiwa na kufumba macho yao bila kujali athari ambzo zianweza kujitokeza ikwamo kuvunjika kwa Muungano ulioasisiwa na Wazee wtu Julius Kmabarage Nyerere na Abeid Aman Karume.

Mtatoka sana povu; lakini judge kawafunika kwa hoja zenye nguvu; mwenyekiti wenu atafungua bunge kwa mipasho na maneno ya kwenye kanga; CCM mnaweza kushinda kubadili rasimu kwa wingi wenu lakini si kwa hoja za maana!!!
 
Nilishawahi kuandika humu kuwa, kuna tofauti kubwa sana pale CCM wanapotamka neno "Mwananchi" na pale watu wengine wapotamka "Mwananchi". Mwanachi kwa wana CCM ni wale ambao ni WANACHAMA WA CCM.THE RESTS ARE NOT CITIZENS.Hili ndilo litakaloiua CCM.Hii nchi ni ya Watanzania wote, kama wapo wananchi waliosema wanataka serikali tatu unategemea Warioba angewakatalia tu kwa sababu inapingana na wanaCCM?Mliunda mabaraza ya Katiba na mkajaza wanaccm huku mkiwakaririsha waseme serikali mbili, walipotakiwa kutoa hoja kutetea point zao wakawa Tabularassa, ulitaka Warioba afumbe macho na kuafikiana nao?Zanzibar ni nchi, na imetamka hivyo katika katiba yao kuwa yenyewe ni nchi, nini hatma ya Tanganyika katika Muungano?Mna point gani ya kutetea hoja yenu ya Serikali tatu?Alichowasilisha Warioba kinapaswa kujibiwa kwa hoja nzito na Si mipasho mliyoianza na mnayotegemea kuhitimishwa na Mwenyekiti wenu Taifa. Think Beyond your Nose!
 
Hahahaaaaaaa no wonder mlikuwa mnataka atumie dkk 120 ili asimalize!!!!!
 
mtu na akili timamu kabisa anakuja hoja ya mizimu? hii nchi ina watu wagonjwa sana. warioba hawasilisha maoni yake. hili wengi hawalijui.warioba kawasilisha maon ya watanzania ambao walikuwa sample kuwakilisha maoni ya wengi. ufumbuzi ni kuwa na Serikali moja au Serikali tatu. kwa mnaoleta hoja za kulinda Muungano kwa nin hamsemi kuwe na Serikali moja? huu Muungano wa sasa ni Muungano gan fafanue. ni nchi gan ma nchi gan zimeungana?
 
kuna mambo mengi sana muhimu yanatakiwa kujadiliwa kwenye hii katiba, lakini cha kushangaza baada ya kujadili haya muhimu tumejikita katika hili oooh mara serikali 2 mara serikali 3, wanasiasa wameshaiteka katiba tayari, muda unakwenda, hili la serikali 2 au 3 linatusaidia nini sisi wananchi, kwani hata muungano ukivunjika kuna shida gani? tuna kero nyingi sana Za kujadiri kwenye katiba ili itusaidie sisi wananchi,, baadala ya sisi kuishinikiza katiba iwe yenye msaada kwetu, tunawasaidia wanasiasa kupiga domo, au ndio kila mtanzania mwanasiasa sasa??? watanzania tuache Kuwa mashabiki wa wanasiasa hebu tuwe kitu kimoja kuwakemea Hawa wanasiasa kwa manufaa ya sisi wengi,,, ili isaidie maendeleo ya kizazi kijacho.
tuache ushabiki wa kisiasa, tuamke tuwe kitu kimoja.
 
Rasimu nzima ya katiba imeandaliwa kwa msingi wa serikali tatu.

Yani mambo yote ya kwenye rasimu ya katiba yamewekwa kwa kuzingatia serikali tatu.

Sasa sijui Warioba amepatwa na maswaibu gani!?

Maana ni wazi kuwa kuna Watanzania wengi wanahitaji muundo wa sasa wa muungano, tena wengi sana. Sasa 'sample' yake aliyoitumia sijui ameipataje kufikia maamuzi ya kuandaa rasimu ya wale wa serikali tatu?

Basi kama Warioba ameamua kuandaa rasimu kwa misingi ya serikali tatu, angefanya vyema pia kuandaa na nyingine ya serikali mbili pamoja na ile ya mkataba ambayo CUF wanaitaka.

Hayo mawazo yaliyotolewa ni ya wale waliohojiwa tu kijana, hata kama wapo wengi wasiotaka huo mfumo wa serikali tatu na hawajatoa mawazo yao hayawezi kuingizwa. Kama unataka yawekwe basi na wewe andaa rasimu yako na mi-CCM wenzio.
 
Rasimu nzima ya katiba imeandaliwa kwa msingi wa serikali tatu.

Yani mambo yote ya kwenye rasimu ya katiba yamewekwa kwa kuzingatia serikali tatu.

Sasa sijui Warioba amepatwa na maswaibu gani!?

Maana ni wazi kuwa kuna Watanzania wengi wanahitaji muundo wa sasa wa muungano, tena wengi sana. Sasa 'sample' yake aliyoitumia sijui ameipataje kufikia maamuzi ya kuandaa rasimu ya wale wa serikali tatu?

Basi kama Warioba ameamua kuandaa rasimu kwa misingi ya serikali tatu, angefanya vyema pia kuandaa na nyingine ya serikali mbili pamoja na ile ya mkataba ambayo CUF wanaitaka.
Tunapojadili hoja ya serikali tatu au mbili, au muundo wa Muungano tunatakiwa kuja na vielelezo ambavyo vitang'amua ukweli na kuthibitisha hoja zetu, vinginevyo tunakuwa tunaongelea ushabiki tu usiokuwa na vithibitisho. Binafsi nampongeza sana Warioba, kwani kathubutu kuweka historia kwa kuacha kumumunya maneno kwa kuangalia nini wanasiasa wanataka kaamua kuweka wazi juu ya historia na muungano uliopo sasa na nn wananchi wanahitaji. Kimsingi yawezekana serikali tatu usiwe mwarobaini wa matatizo yaliyopo, lakini ukachangia kwa kiasi kikubwa kupunguza matatizo na changamoto zilizopo kuliko mfumo wa sasa wa serikali mbili nchi mbili.
 
Takribani zaidi ya masaa matatu aliyotumia Mwenyekiti wa Mchakato wa Katiba Mpya, Jaji Joseph Sinde Waryoba kuwasilisha kile kinachoitwa(nasema ni kile kinachoitwa kwa vile sasa maana halisi ya Katiba Mpya haipo tena) Rasimu ya Katiba Mpya alitetea (na siyo kuwasilisha maoni ya wananchi) muundo wa Serikali tatu.

Watanzania wengi kutoka makundi mbali mbali wakiwemo Wakulima, Wafugaji, Walemavu, Watoto, Vijana, Wanawake, Wazee na mengine mengi wamebaki wameduwaa na kujiuliza maswali mengi kama kilichowasilishwa jana bungeni ni Rasimu ya Katiba Mpya au ni Rasimu ya namna gani ya Muundo wa Muungano unawafaa watanzania, hoja ambayo pasi na shaka ni kwa manufaa ya wanasiasa.

Jmbo kubwa ambalo watu wamebaki wakijiuliza ni namana ambavyo Waryoba alitumia nguvu nyingi kutetea hoja ya serikali tatu huku akijua kabisa katika mchakato mzima wapo watanzania tena wengi tu ambao ni waumini wa Serikali mbili na wengine akiwemo yeye mwenyewe ni auminini wa serikali moja.

Watu wanajiuliza Waryoba ambaye ni muumini wa serikali moja alishikwa na nini au kuna nini kimejificha juu ya msimamo wake katika serikali tatu na kusahau kabisa kugusia hata serikali moja ambayo yeye anaaamini ni nguzo imara ya Muungano?

Lakini kubwa ambalo Makungi ambayo jana yamesaulika kwenye hotuba ya Jaji waryoba yanajiuliza ni wapi watasimama kuhoji haki zao kwenye Katiba itakayopatikana wakati tangu mwanzo wameonekana kusahaulika?

Mytake: Iko haja kubwa kabisa ya Wabunge wa Bunge maalum la Katiba kujitazama upya kuhusiana na rasimu hiyo la sivyo kuna kila dalili kuwa Katiba inayokwenda kuandikwa ni kwa ajili ya Wanasiasa na watu kama akina Waryoba ambayo yawezekana kabisa kuna kitu wameahidiwa na kufumba macho yao bila kujali athari ambzo zianweza kujitokeza ikwamo kuvunjika kwa Muungano ulioasisiwa na Wazee wtu Julius Kmabarage Nyerere na Abeid Aman Karume.

Mkuu jipMbnue katika kusolve kiakili big and overiding issue first.
Unapoongelea mfugaji kama kipaumbele atahudumiwa na serikali ipi?
Na fungu lake la kodi ni kutokka kwa watu wepi?

Soma ujiridhishe na mada kwanza
 
Back
Top Bottom