Warioba: Kura ya maoni Aprili ndoto

Mfikirishi

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
8,939
Reaction score
10,403
Nimesoma kwa undani mahojiano ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na gazeti la Nipashe na kubaini kuwa kwa ustawi mzuri na amani ndani ya nchi yetu ni busara tusahau kwa muda masuala yote ya Kura ya Maoni na Katiba Mpya...

Kama kweli nchi yetu ni maskini kama inavyotamkwa na wengi ni bora tukafanya uchaguzi alafu baadaye ufuate mchakato wa Katiba tena kwa kufuata vigezo na masharti si kukurupuka!!

Mimi naomba niongezee "Katiba Mpya Kabla ya 2015 ni Upotoshaji"
Ni aibu kuona kuwa suala la Katiba ya Nchi watu wanalichukulia kirahisi rahisi kama Katiba za NGOs zao tu kule mtaani!!
Tukiendelea kudanganywa na wapiga porojo na wenye mamlaka hii nchi itaishia pabaya!!
TUSIDANGANYIKE!!
=========================

 
Duuh, CCM walizarau ushauri wa huyu mzee, lakini kwa kadri siku zinavyozidi kwenda, kile alichokisema naona kama kitaenda kutimia,,!! Na ikiwa hivyo, sijui itakuwaje?

Aibuu
 
Duuh, CCM walizarau ushauri wa huyu mzee, lakini kwa kadri siku zinavyozidi kwenda, kile alichokisema naona kama kitaenda kutimia,,!! Na ikiwa hivyo, sijui itakuwaje?

Aibuu

Huyu mzee ndio chanzo cha matatizo mengi yanayoikumba ccm kwa sasa. Alitaka kutimiza azma ya chuki yake kwa Mwalimu.
 
Huyu mzee ndio chanzo cha matatizo mengi yanayoikumba ccm kwa sasa. Alitaka kutimiza azma ya chuki yake kwa Mwalimu.

Hivi mtu kama mimi nikitoka nikakwambia wewe ni mlopokqji usiyejua unacholopoka utasema nimekutukana? Hivi chama cha mapinduzi na hili taifa ni kipi bora kwako? Hivi mzee WARYOBA na NYERERE walitofautiana lini?

eti anakiharibu chama? chama ni nini? hivi hujui taifa lako ndio unaweza kujivunia? huu uzubaifu wa akili yako unauleta mbele za watu bila kufikiri kama haukuwa na maana kutuonyesha ulivyo mjinGA...

Jana wakati unasema haya maneno najua ulikuwa na usingizi ebu ukiamka asubui hii utafakari upya.
 

Huna maono, achana na mimi.
 

Sidhani kama Warioba ana lolote la maana. Keshamaliza majukumu yake kuhusu Katiba NA Tume kuvunjwa akae pembeni. Anataka nini huyu mtu ambaye aliwahi kuwa Waziri mkuu. Tumkumbuke kwa lipi alipokuwa Waziri mkuu alilowatendea Watanzania.

Kila kitu na wakati wake na mahali pake. Ukienda Msikitini au kanisani lazima uendane na mahali hapo. Ukikutwa unakula Chakula chooni una walakini hapo si mahala pake.
 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba Jaji Joseph Warioba amesema, kura ya maoni ya katiba pendekezwa iliyopangwa kufanyika April 30 itakuwa ngumu kufanyika kwa vile muda wa elimu kwa wapiga kura hautoshi.

Amedai kisheria zinatakiwa siku 60 za elimu na siku 30 za kampeni.

Kutoka magazetini.
 
Hakuna kushiriki kwny upuuzi wao huo.Kwanza kwani katiba pendekezwa ipo? si yapo mautumbo ya 6 na chenge na vilaza wote waliobaki kwaajili ya posho pale Dodoma.SHAME
 
Kufanya mambo hovyo hovyo ndo imeshakuwa jadi ya Serikali yetu. Mungu atatunusuru tu.

Nawahurumia sana Watz wenye uelewa wa mambo jinsi wanyoumia ndani ya mioyo yao wanapoona mambo yanavyopelekwa pelekwa. Ni huzuni na stress kubwa.
 
Kwani elimu kwa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu inatolewa kwa utaratibu gani?
 
Hakuna kushiriki kwny upuuzi wao huo.Kwanza kwani katiba pendekezwa ipo? si yapo mautumbo ya 6 na chenge na vilaza wote waliobaki kwaajili ya posho pale Dodoma.SHAME
Nyie mkisusa, sisi twala
 
Kwani elimu kwa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu inatolewa kwa utaratibu gani?

Mbona unajitoa ufahamu kwenye mambo ya msingi. Hapa linazungumziwa suala la kura ya katiba mpya kwa kuzingatia sheria iliyowekwa na bunge ya mabadiliko ya katiba, wewe unaongelea uchaguzi mkuu.

Hata hivyo uchaguzi mkuu una elimu kwa wapiga kura? Nyie ndio mnaofanywa watanzania kila siku kuwa na mawazo mgando. Think out of the BOX mkuu, don't be narrow minded
 

Watabadili tu tarehe ili kukidhi hayo matakwa ya siku...inaweza kufanyika may 2015
 
Hakuna kushiriki kwny upuuzi wao huo.Kwanza kwani katiba pendekezwa ipo? si yapo mautumbo ya 6 na chenge na vilaza wote waliobaki kwaajili ya posho pale Dodoma.SHAME

kata yetu imepokea nakala 900 zinazogawiwa kwa makundi mbalimbali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…