Kura ya maoni ni njia pekee ambayo Watanzania wa pande zote watakuwa na haki ya ku-determine their right to self-determination. Haya mengine ya sijui serikali tatu ni kupotezeana muda na matumizi ya fedha yasiyokuwa ya lazima.
Yaani nchi mmoja inakuwa na Marais watatu? Kwa hiyo siku wakitembelewa na mkuu wa nchi nyingine, watakuwa wanajipanga mbele yake na kujitambulisha mimi ni wa Tanzania, mimi wa Tanganyika na mimi ni wa Zanzibar? Hiki ni kioja.
Ukiachilia mbali Urais bado kutakuwa na Bunge la Muungano ambalo litakuwa na wabunge sijui 70 or so achilia mbali Waziri Mwandamizi, Mawaziri wa wizara za muungano, Manaibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu wa Wizara hizo hizo za Muungano. Nadhani na serikali shiriki zitakuwa na watu kama hao pia.
Badala ya ku-address tatizo tunalizungazunga na kulipaka rangi za kuvutia. Wapo wanaodai kuwa pendekezo la serikali tatu limewekwa ili kurahisisha kuvunjika kwa muungano.
But justice delayed is justice denied. Tunajua muungano utavunjika tuu, but the earlier the better.