Wasabato wajibu wenu kufundisha na kuwafanya watu bil 3 duniani wampokee Yesu awe bwana na mwokozi wao, na siyo kuhubiri chuki dhidi ya wakatoliki

Wasabato wajibu wenu kufundisha na kuwafanya watu bil 3 duniani wampokee Yesu awe bwana na mwokozi wao, na siyo kuhubiri chuki dhidi ya wakatoliki

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Wadau hamjamboni nyote?


Huu ni ushauri wa kiroho na kumbusho la msingi kwa Wasabato ulimwenguni kote kuzingatia majukumu na maelekezo ya msingi ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Nimezingatia maandiko matakatifu na wala sikusudii kufanya shambulizi dhidi ya taasisi ya kisabato

Wasabato tunao watu zaidi ya billion 3 wasiomjua Kristo duniani kote hivyo ni vema Kanisa likajikita kuwafundisha na kuwafanya watu hao wampokee Kristo awe bwana na mwokozi wao

Nguvu kubwa ya Kanisa ielekezwe kwenye kuhubiri injili na kuokoa roho zilizo gizani badala ya kuzitumia kushambulia taasisi ya roman Katoliki

Waamini wengi wa kisabato wamepoteza uelekeo na mioyo yao imejazwa sera za chuki dhidi ya taasisi Katoliki na makanisa mengine yanayoabudu Jumapili


Kwa Msabato ni muhimu zaidi kuhubiri chuki dhidi ya wanaoabudu Jumapili kuliko kutumia rasilimali zao kuwahubiri na kuwaokoa kupitia injili wale wasiomjua Kristo

Itakuwa ni furaha kubwa na shangwe mbinguni na duniani pale tutakapoifanya kazi tuliyotumwa na mwokozi wetu.

Uongozi Kanisa la Wasabato tushirikiane kuhubiri injili tuokoe kondoo waliopotea kabla ya marejeo ya Kristo

Taasisi zote zinazoabudu Jumapili hao tayari walishakiri kwa vinywa vyao kuwa Kristo ndiye Bwana hao hivyo tuwe nao sambamba kuwahubiri wale wasiomjua Kristo

Niwatakie siku njema


Takwimu rasmi

Projected size of major religious groups for 2023[1]
ReligionPercent


Christianity- 30.7%
Islam- 24.9%
Unaffiliated-15.6%
Hinduism-15.1%
Buddhism - 6.6%
Folk religions - 5.6%
Sikhism- 0.3%
Other religions-1.2%

Waislamu jumla 1.8 billion
Wahindu jumla 1.2 billion
 
Kwahiyo tukiwaambiwa tunaabudu sanamu na papa ni mnyama inakuwa chuki?

Hizi dini sio za kuzipa airtime sana mi huwa naenda hadi kwenye mikutano yao wanavitabu vizuri sana vya Afya nk
Hayo mengine ya kuabdu jpli wala huwa sijari sijui bikira maria wala sina muda nayo najifunza masomo ya afya then narudi zangu
 
Back
Top Bottom