Wasanii ambao watakumbukwa hata kama muziki ukiwatupa mkono

Kwa Vanessa umepuyanga kaka
 
kwangu ni hawa Dully Sykes, Fid Q, Ray C, afande sele, Ali Kiba, Lady Jaydee, ngwair... hawa unaona wanafanya muziki kwa passion, wana talent na mashairi yanaokujia kichwani kila mara...Diamond naona alikuwa akifanya muziki mzuri enzi za Mbagala na kamwambie, hizi za siku hizi ni Big G hazidumu labda aache legacy kama mwanamuziki aliye exploit muziki kibiashara zaidi
 
Umemsahau BIZIMAN
Umemaliza
 
...kuna nyimbo na sio nyimbo tu, hata movie kuna ambazo ni classic, na nyingine zinakuja kwa kiki kubwa ila baada ya muda zinapoteza ladha hadi unaona aibu kusikiza..kuna zile nyimbo za Mr. Nice zilivyobamba leo hii utamsikia akisikiliza? ila kuna nyimbo za akina dully sykes, ray c, lady jaydee akisililiza mtu haonekani mshamba
 
Mkuu sio kama nashabikia hizi team zisizo na viwanja Ila naoma kuhoji. Hivi ni wimbo gani wa mond ambao hata ukiusikia sasahivi bado haupotezi ubora( hauchuji)???
Op/ chaka, mada na tamko lako haviendani
 
Wanafanya style tofauti ya Muziki.

Hapo unamshindanisha Tupac na R.kelly au Michael Jackson na Bob Marley.

Kila mmoja kafanya lake kwa upande wake.
Sawa ila ujumbe unaobebwa kwenye tungo na ubora wa muziki bado unabaki pale pale. Kwani hao wasanii wanashindwa nini kuandika tungo za kueleweka katika hizo hizo style zao.?
 
Inategemea muziki umeanza kusikiliza lini, Mimi kwangu diamond ndo sitamsahau wengne Hanna kitu laba kidogo prof jay
 
mbn hamjagusa Saleh Jabir...hapo watoto wa 90 hawatamwelewa
 
Wakati MTOTO WA DANDU anafanya mziki MBELE ulimskiliza? Wakati SUGU anaimba na Peter Andre, uliiskia ile ngoma? Wakati JD anaperform KORA SA, AY alikuwa wapi?
Mtoto wa juzi hawezi elewa hata ukimwambia kuna Mtz kapiga cypher BET chin DJ PREMIER hajui
 
Jide, MwanaFA, Afande selle, Mrisho Mpoto
 
Sawa ila ujumbe unaobebwa kwenye tungo na ubora wa muziki bado unabaki pale pale. Kwani hao wasanii wanashindwa nini kuandika tungo za kueleweka katika hizo hizo style zao.?
Kwani hawajawahi kuandika Nyimbo za ujumbe?!

Ulitaka Nyimbo zao zote ziwe za ujumbe?Alafu wapate sifa bila kuwa na hela?!

Muziki ni biashara huria kila mtu anafanya anachoweza....Ila wewe unataka watu wote waimbe ujumbe kama Afande Sele
 
Wewe unaejua Bongo flava unataka kusema Msingi ulijengwa na Sugu peke yake na hakukuwa na Wengine?!

Tuelewane hapa tafadhali Sugu alikuwa na mchango wake na naupa heshima pia ila sio kiasi cha kumfanya kama nabii wakati kuna watu kibao walifanya makubwa kuliko yeye.

Kwangu Profesa Jay anastahili heshima nyingi kuliko Sugu yeye kuanza haimaanishi wote waliokuja baada yake hawana uwezo kuliko yeye.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…