Wasanii hawa hawajawahi kutoka ingawa hawajijui

mtoa post kwa roma umechemka, roma ametoka sana tu!
 
Hizo nyimbo ulizotaja zote hazijawatoa licha ya kupata promo..lakini hukatazwi kuzipenda na kuwapenda waimbaji wake si unajua penzi ni kikohozi!

Umeulizwa ni vigezo gani umetumia kupata wasiotoka?

Anyway hata wewe hukatazwi kuwachukia usio wapenda na kuwa lable HAWAJATOKA
 

Hii thread ya kichoko
 
Luteni Kalama ni mkali sana lakini nadhani hakuwa mzuri katika utunzi! Inspekta, alikuwa mkali sana wa kutunga sasa wakati Gangwe Mob ipo juu, Inspekta alikuwa na tabia akihisi kwamba nyimbo aliyoandika itakuwa kali basi alikuwa anaimba peke yake kv Mtoto wa Ghetto Kali na Asali wa Moyo! Nakumbuka enzi hizo maskani Kalama mwenyewe alishawahi kumnanga Inspekta kwamba alikuwa anamficha asionekane!

Ukitaka kumjua Kalama mbaya, tafuta ngoma moja inaitwa Bundesliga... Kalama kakimbiza balaa!
 
Abdul Kiba naona anategemea sana back up ya Ali Kiba... kwa staili hii, itakua ngumu kidogo hadi atakapoamua kutoka kivyake... huyo Snare, unaleta masihara kv hakustahili kabisa kuwepo hata kwenye hiyo list
 
Best nasso, sajna, sisal madini, jambo squad, mirror, babuu wa kitaa, country boy, stamina, bonta, jose mtambo,
KUsema Jose Mtambo hajatoka sidhani kama ni sahii coz' haielekei kama bado ana-fight kwenye game... jamaa ni old school lakini mpaka kesho anajua ile mbaya lakini kama ilivyo kwa old schools kibao, nadhani kaamua afanye mambo mengine coz' yeye kafanya muziki enzi za kutembea na tape mfukoni, tunatunga mida ya break, watu tunazama Jiteute kushindina kuchana... acha wanafunzi wa Dar tufeli... sie wengine hadi leo tunajiuliza tulifikaje fikaje tulikofika!!!
 
Abdu kiba anaimba vizuri
 

Inspekta mnafki flani ilifika kipindi kule tmk alikua anachukiwa kwa tabia zake!..alipotoka alikua anajiita mtoto wa knyama na sio tmk mshamba flani
 

ipo nyingine inaitwa tunajirusha ameshirikishwa na nesacery noise pia amefanya vizuri
 
ipo nyingine inaitwa tunajirusha ameshirikishwa na nesacery noise pia amefanya vizuri
Sure... jamaa katembea sana kwenye ile ngoma! Sema hata Inspekta nae katembea sana kwenye tunajirusha... ni bonge la collabo hadi umenipa hamu ya kuitafuta tena ile ngoma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…