Ma-chemist
Member
- May 11, 2020
- 36
- 15
Kama kichwa ha habari kinavojieleza hapo juu, msaada tafadhali.
Tunaeleka mwaka wa uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge pamoja na madiwani. Ipo haja sasa kwa Watanzania kukaa na kupima licha ya kwamba Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuweka wazi kabisa katika Ibara zake kuwa kigezo cha mtu kugombea nafasi yeyote ya kuwa kiongozi katika nchi, kubwa kabisa ni ile inayosema lazima ajue kusoma na kuandika. Lakini sasa, wakati umefika kwa Watanzania wenzangu kuangalia na kulinganisha kuwa tuko katika Karne ya ngapi, na sheria hii ilitungwa Karne ya ngapi.
Hatuwezi kuwapa ridhaa watu ambao wanataka kutumia kigezo cha umaarufu walio nao kutaka kuungwa mkono katika hatakati zao za kisiasa na kupata ridhaa ya kuwa akilisha wananchi ndani ya Bunge. Hoja kubwa apa kuna baadhi ya Wasanii kama vile Shilole, Harmonize, Steve Nyerere kutaka kutangaza nia ya kugombea nafasi za ubunge katika majimbo yao.
Watu hawa ambao wanataka kutumia kigezo cha umaarufu wakati hata elimu zao hazijavuka kidato cha nne, wengi wao ni Darasa la Saba, na sina hakika kama walipata cheti, narudia kusema sina hakika kama walipata cheti cha kuhitimu elimu ya msingi maana kigezo cha kupata vyeti vya baraza vipo, lazime uwe umehitmu kikamilifu na kupata alama stahiki.
Watanzania, angalau mtu anaetaka kutangaza nia ya kugombea katika nafasi hizi awe na Elimu isiyopungua angalau kidato cha sita na kuendea kama shahada, shahada za uzamili na shahada za uzamivu katika nyanja yeyote. Hatutaki kuona Bunge la wabunge wa kutuonesha vituko na kiki ndani ya Bunge. Tunataka maendeleo chanya (+) katika karne hii ya 21.
Watanzania wenzangu, kwa hiyo awa wasanii waliochukua hatua ya kutangaza nia ya kugombea nafasi yeyote lazima wajitathmini mara tatu; wasitumie upendeleo wao wa kuwa wasanii maana kipindi hiki cha 2020 haitawezekana. Na ushauri wangu kwao wasije wakaendelea kuhamasisha watu kuwaunga mkono🎓📝
Tunaeleka mwaka wa uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge pamoja na madiwani. Ipo haja sasa kwa Watanzania kukaa na kupima licha ya kwamba Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuweka wazi kabisa katika Ibara zake kuwa kigezo cha mtu kugombea nafasi yeyote ya kuwa kiongozi katika nchi, kubwa kabisa ni ile inayosema lazima ajue kusoma na kuandika. Lakini sasa, wakati umefika kwa Watanzania wenzangu kuangalia na kulinganisha kuwa tuko katika Karne ya ngapi, na sheria hii ilitungwa Karne ya ngapi.
Hatuwezi kuwapa ridhaa watu ambao wanataka kutumia kigezo cha umaarufu walio nao kutaka kuungwa mkono katika hatakati zao za kisiasa na kupata ridhaa ya kuwa akilisha wananchi ndani ya Bunge. Hoja kubwa apa kuna baadhi ya Wasanii kama vile Shilole, Harmonize, Steve Nyerere kutaka kutangaza nia ya kugombea nafasi za ubunge katika majimbo yao.
Watu hawa ambao wanataka kutumia kigezo cha umaarufu wakati hata elimu zao hazijavuka kidato cha nne, wengi wao ni Darasa la Saba, na sina hakika kama walipata cheti, narudia kusema sina hakika kama walipata cheti cha kuhitimu elimu ya msingi maana kigezo cha kupata vyeti vya baraza vipo, lazime uwe umehitmu kikamilifu na kupata alama stahiki.
Watanzania, angalau mtu anaetaka kutangaza nia ya kugombea katika nafasi hizi awe na Elimu isiyopungua angalau kidato cha sita na kuendea kama shahada, shahada za uzamili na shahada za uzamivu katika nyanja yeyote. Hatutaki kuona Bunge la wabunge wa kutuonesha vituko na kiki ndani ya Bunge. Tunataka maendeleo chanya (+) katika karne hii ya 21.
Watanzania wenzangu, kwa hiyo awa wasanii waliochukua hatua ya kutangaza nia ya kugombea nafasi yeyote lazima wajitathmini mara tatu; wasitumie upendeleo wao wa kuwa wasanii maana kipindi hiki cha 2020 haitawezekana. Na ushauri wangu kwao wasije wakaendelea kuhamasisha watu kuwaunga mkono🎓📝