Wasanii wa singeli mlitaka kudharau Nazi wakati embe ni tunda la msimu

Wasanii wa singeli mlitaka kudharau Nazi wakati embe ni tunda la msimu

mayowela

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2014
Posts
2,125
Reaction score
1,753
Muziki wa singeli umeshika sana wakati huu hasa mikoa ya Pwani, na mikoani kila mtu alitaka kujua ni muziki wa aina gani, si kwamba haukuwepo zamani ila jitihada za Efm zilichangia ushike hatamu japo redio ilikuwa haijafika mikoa mingi na walienda mbali mpaka kuanzisha kipindi maalumu kw aajili ya singeli chini ya Kicheko Mtata.

Kila muwamba ngoma huvutia kwake, mziki ukapokelewa kwa nguvu zote wasanii wa singeli wakaanza ona matunda kwa kualikwa kwenye show za Efm, na wengine kufanya dili za matangazo, nakumbuka Man Fongo alishafanya tangazo la Kampeni ya Nitigo pesa kutoka Tigo, Kicheko akasajiliwa Clouds na kuna baadhi ya wasanii wakagawanyika beef zikaanza wengine wakaona upande wa pili ndio wa maana sana

Nakumbuka Kicheko alipofika Clouds kwenye kipindi cha leo tena ilianzishwa segment akawa anapewa muda wake na zinachezwa singeli, sijui hiyo program ilipotelea wapi na Kicheko mwenyewe hasikiki kama zamani, baadae akahamia Jumamosi jioni kabla ya Kipindi cha Peter Moe. Mkazo wa singeli kwa Clouds tena ukawa umeishia hapo.

Efm bado wanalisongesha kipindi cha singeli alichokiacha Kicheko bado kinaendelea na naona mbadala wa Kicheko usajili wake ulikuwa mzuri Semio na Fido wamerudisha hadhi ya kipindi pia wasanii wa singeli bado wanaendelea kufanya show zinazoandaliwa na Efm, mara ya mwisho kuona msanii wa singeli akifanya show iliyoandaliwa na Clouds ni Fiesta 2017, lakini ilikuwa tofauti kwa Fiesta 2016 wasanii wa singeli walikuwa wengi

Nnnachosema msizalau Nazi
 
Kwanza kabisa naomba ujue mziki ni radha, na radha ni mzizi wa hisia za hadhira. Ninachokiona kwenye mziki huo wa singeli, ni mziki unaojaribu kukamata soko kwa segments..... Jambo ambalo sio sahihi (wenye uelewa, wamenielewa). Nadhani kuna haja ya wadau wa mziki huo, kukaa chini na kuutafakari kwa kina......kwa kufanya hivyo, bila shaka watafanikiwa kufikisha mziki huo pale wanapotamania ufike.

Asante.
 
sidharau miziki ya aina hii mana watu wanapata riziki zao ila singeli na taarabu ni aina ya miziki ambazo nazichukia sana.
 
Kwanza kabisa ulichokisema kina ukweli kwa asilimia kubwa sana .
Kwa kiwango kikubwa kwa sasa mziki wa singeri umepotea njia kwa kiasi kikubwa sana hii inatokana na gemu kuingiwa na wapiga dili wengi .
 
Shida ni kwamba hawa jamaa wengi sna hakuna shule, ndio mana, angalia hata wale wa Bongo Fleva, wengi wao akina sisi tuu, wachache kidogo ndio wamejishikizia mpaka tu degree tumoja
 
Singeli Muziki usiokuwa na maadili kbs ufutike kabisa Tanzania kwa afya ya watoto wetu na vizazi vijavyo.
 
Ningekua kiongozi ningepiga marufuku huo mziki, siupendi hata kidogo.

Ni mziki wa ki-uhuni sana
 
Wajitume kwa kufanya kazi nzuri watakiki, hata hao clouds watawafuata wenyewe maana clouds wanachoangalia ni pesa tu
 
Back
Top Bottom