Wasanii wa Tanzania wanaofanya kazi na "World Class Celebrities" watusaidie kuwashawishi ili tuwatumie katika kuitangaza nchi yetu kwa gharama nafuu??

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2012
Posts
15,892
Reaction score
16,476
Shikamooni wakubwa zangu wote wa humu jamiiforums. Mimi mdogo wenu Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.

PLEASE ANZA KWA KUSOMA HII THREAD YANGU

Kwanza ninapenda kutoa shukrani zangu za dhati sana kwa Mh. Waziri wa maliasili na utalii ndugu yangu na kaka yangu Hamisi Kigwangala kwa kuandaa HKKilichallenge iliyokuwa na lengo la kuhamasisha utalii wa ndani.



BACK TO THE TOPIC:
Wasanii wa Tanzania wanaofanya kazi na "World Class Celebrities" watusaidie kufanya ushawishi (lobbying) ili tuitangaze vema nchi yetu kupitia social media platforms. Celebrities wa Tanzania wanaweza kuwashawishi wasanii wa kigeni wanaoshirikiana nao katika kazi za sanaa kuja kupanda mlima Kilimanjaro pamoja na kitembelea mbuga ya Serengeti.

Ukijaribu kutazama picha hapo chini, ni baadhi ya Celebrities wa Tanzanian wakiwa na wenzao wenye umaarufu mkubwa zaidi hapa duniani.

AY AKIWA NA LIL' ROMEO


DIAMOND AKIWA NA RICK ROSS


DIAMOND AKIWA NA OMARIO


A.Y AKIWA NA SEAN KINGSTON

Ninaomba msininukuu vibaya. Sijasema hao "World Class Celebrities" waitanagaze vema nchi yetu BURE. Hapana. Tunaweza tukapata discount nzuri sana tu ya kutangaza vivutio vyetu kama wasanii wetu watafundishwa namna ya kuongea nao kwa lugha njema na ya kistaarabu (lobbying) kwa maana kuna msemo wa Kiswahili unasema "zimwi likujualo halikuli likakwisha"

Kwa mfano Serikali nchini Norway imeanzisha utaratibu wa kununua nakala kadhaa za waandishi wa vitabu ambao kazi zao zimehakikiwa na mamlaka husika ya kiserikali. Soma link hapo chini;


Vp kama idea hii tukiihamishia upande wa kazi za sanaa na kusema serikali kupitia wizara husika (wizara ya sanaa ama ya utalii) itanunua nakala kadhaa za msanii wa ndani pamoja na yule wa nje ambao wote kwa pamoja wataenda kupanda mlima Kilimanjaro au kitembelea mbuga ya Serengeti?

OUR MOTTO: KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
 
Pia Fuatilia makala zangu humu jamiiforums ili upate maarifa zaidi


 
It is a business serikali iweke business mezani uone kama hats Jay Z haletwi. Ila kusaidiwa katika biashara hill suala halipo. Ukitaka kujua mindset ya kibiashara kaangalie video ya Salam SK alipokuwa akihojiwa majuzi kuhusu beef LA WCB na Clouds.
Issue no nchi ipate na wasanii wapate. Kwani Waziri yeye anajitolea? Anasaidia au anafanya kazi na analipwa kwa kazi take.
 
"World Class Celebrities" watusaidie kufanya ushawishi (lobbying) ili tuitangaze vema nchi yetu kupitia social media platforms.

Waanze kwanza kuepewa mafunzo ya kuwa na real smile na kuonekana wako serious na mission, hapa kwenye picha tabasamu lao linaonekana kabisa ni kulazimishwa, na hata hivyo vidole siyo wote wamependezewa kuweka hivyo, possibly hapakuwepo maamuzi ha pamoja kwenye hiyo picha
 
Thanks brother
 
Sasa brother kungekuwa hakuna punguzo la biashara ama kusaidiana kwanini kwa kiingereza kuna maneno kama "discount" pamoja na "bargaining"???
Kwani serikali imeshindwa kulipa bei Fulani sasa wanataka discount? Huenda hata Kigwangala hajawaza unachowaza. Anasubiri luckily Jay Z aje tu, au labda Chris Wizzy ashirikiane na Diamond halafu amlete yeye apitie kitonga.
They need to invest in industry. Kama target yetu ni 10million tourists in 3 years to come ni lazima tuwekeze kwenye matangazo. Pay millions of $ and get much more.
We can even sponsor some basketball teams in US halafu tuone outcomes.
 
Huenda hata Kigwangala hajawaza unachowaza. Anasubiri luckily Jay Z aje tu, au labda Chris Wizzy ashirikiane na Diamond halafu amlete yeye apitie kitonga.
Ndugu yangu, inawezekana Mh. Kigwangalla hajawaza ninachokiwaza kwa maana na yeye pia mwanadamu na ana majukumu mengi ndio maana tunakumbushana kama hivi kupitia social media platforms
 
Asante kwa mchango wako pia
 
"Hata beyonce, Jay z, Chriss brown, Rihanna na Dj khaleed walituomba tuingie nao mikataba lakini kama wizara bado tunaendelea kutafakari"
 
Asante kwa kuchangia
 
Wakitangaze kiswahili na wawakabidhi kile kitabu cha kijani wanachobeba wazalendo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…