Wasanii waitwe wachafuzi wa jamii na sio vioo vya jamii

Wasanii waitwe wachafuzi wa jamii na sio vioo vya jamii

MIDFIELD

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2013
Posts
1,944
Reaction score
702
Habari za jpili bandugu, wanajukwaa. Kuna kitu mimi huwa kinanipa shida sana kukubaliana nacho. Tutafakari kwa pamoja suala hili.

Kwa muda mrefu sana wasanii mbalimbali wwamekuwaa music, maigizo ulimbwende n.k wanapenda kujinasibu kuwa wao ni vioo vya jamii, kwa maana hiyo jamii inapaswa kuwaiga mambo yao. Kiukweli kwa mambo ambayo wanayanya hawa wasanii mengi yao ni machafu kabisa. Mifano michache tu, wao ndo wamekuwa vinara wa madawa ya kulevya, ngono, picha chafu za ngono, uvaaji mbovu kabisa ambao watoto wetu wanaiga na mengine kibao. Kwa mtaji huu nashauri wasanii waitwe wachafuzi wa jamii na siyo kioo cha jamii. Kioo cha jamii ni vema aitwe mwalimu kwani sote tunapitia kwa walimu toka chekechea mpk vyuo vikuu.
Nawasilisha
 
Habari za jpili bandugu, wanajukwaa. Kuna kitu mimi huwa kinanipa shida sana kukubaliana nacho. Tutafakari kwa pamoja suala hili.

Kwa muda mrefu sana wasanii mbalimbali wwamekuwaa music, maigizo ulimbwende n.k wanapenda kujinasibu kuwa wao ni vioo vya jamii, kwa maana hiyo jamii inapaswa kuwaiga mambo yao. Kiukweli kwa mambo ambayo wanayanya hawa wasanii mengi yao ni machafu kabisa. Mifano michache tu, wao ndo wamekuwa vinara wa madawa ya kulevya, ngono, picha chafu za ngono, uvaaji mbovu kabisa ambao watoto wetu wanaiga na mengine kibao. Kwa mtaji huu nashauri wasanii waitwe wachafuzi wa jamii na siyo kioo cha jamii. Kioo cha jamii ni vema aitwe mwalimu kwani sote tunapitia kwa walimu toka chekechea mpk vyuo vikuu.
Nawasilisha
Kwaiyo vioo vya jamii ni wanasiasa
 
Ninavyoelewa mimi waliposema kioo ni kumaanisha utavutiwa na kazi zake na atakuinfluence ufuate nyayo za hiyo kazi.

Mfano wachekeshaji wengi hua wanasema Majuto ndiyo kioo chao.

Hii maana ya kimaadili sijui nani kaileta. Halafu mtu awe hasi au chanya ni atakupa somo tu, ukiona mlevi anapata shida utajifunza kua usiwe mlevi n.k.
 
Nadhani mkuu kuna kitu ambacho hujakielewa kuhusiana na huo msemo kuwa 'wasanii ni kioo cha jamii'

Msanii anatumia sanaa yake (kuimba au kuigiza n.k) kuonyesha kitu fulani kilichopo kwenye jamii kiuhalisia au kugikirika. Kioo maana yake taswira (ni kama unapojitazama kwenye kioo, utachokiona ndivyo ulivyo) ndio maana wanasema wasanii ni vioo sababu hata wafanye uchafu kiasi gani mtaani kuna uchafu zaidi ya wanaoufanya wao.
 
Hayo wanayoyafanya yapo katika jamii....Amini kuwa hayo wanayofanya yanafanywa na wengi katika jamii ila kwa kuwa hawana majina hayachukui sura kama yanayochukua yakifanywa na wasanii
 
Hayo wanayoyafanya yapo katika jamii....Amini kuwa hayo wanayofanya yanafanywa na wengi katika jamii ila kwa kuwa hawana majina hayachukui sura kama yanayochukua yakifanywa na wasanii
Ok inawezekana pia lakini kinachonipa shida, ni asilimia kubwa sana yao wanajihusisha na hayo mambo
 
Nadhani mkuu kuna kitu ambacho hujakielewa kuhusiana na huo msemo kuwa 'wasanii ni kioo cha jamii'

Msanii anatumia sanaa yake (kuimba au kuigiza n.k) kuonyesha kitu fulani kilichopo kwenye jamii kiuhalisia au kugikirika. Kioo maana yake taswira (ni kama unapojitazama kwenye kioo, utachokiona ndivyo ulivyo) ndio maana wanasema wasanii ni vioo sababu hata wafanye uchafu kiasi gani mtaani kuna uchafu zaidi ya wanaoufanya wao.
Nakubaliana na wewe mkuu kwamba mtaani wanafanya ya hovyo zaidi, lakini wao (wasanii) walipaswa kufanya mazuri basi ili kweli waielimishe jamii iachane na hayo ya hovyo na hapo wangestahili kuitwa kioo cha jamii. Na ikiwa tafsiri ya kioo cha jamii ni ile taswira anayoiona mtu jinsi alivy katika kioo, basi wasanii wapo sahihi kwa maana kwamba wanaonesha jinsi jamii yetu tulivyo na mambo ya hovyo
 
Hivi kweli ni msanii yupi unaweza sema ni kioo cha jamii kwa mavazi yao, maisha ya kimahusiano(mafuska wa waziwazi), wengi wanatumia madawa ya kulevya, ni washirikina na mbaya zaidi hawajali familia ( hawana?) na ndugu zao. Wao ni maisha ya starehe bila kumcha Mungu.
Halafu useme kioo cha jamii? Jamii ipi?
 
Wasanii wa Tanzania huwa nawaona kama Vichaa.
Ni kweli kabisa mkuu. Lakini katika utafiti wangu mdogo nakuja kugundua kwamba asilimia kubwa upeo wao hasa kielimu (formal education) ni mdogo sana. Sasa namna pekee ya wao pia kuonekana ktk jamii na kujipatia kipato ni kufanya hayo yasiyostahili
 
Hivi kweli ni msanii yupi unaweza sema ni kioo cha jamii kwa mavazi yao, maisha ya kimahusiano(mafuska wa waziwazi), wengi wanatumia madawa ya kulevya, ni washirikina na mbaya zaidi hawajali familia ( hawana?) na ndugu zao. Wao ni maisha ya starehe bila kumcha Mungu.
Halafu useme kioo cha jamii? Jamii ipi?
Well said
 
Sawa mwalimu, sh'kamoo
Marahaba screpa.
ila jamani majina ya jamii forum ni mazuri sana. maana jina tu pekee linakuchekesha kabla hujasoma hata comment yake. Wakitulazimisha kutumia majina halisi watatukimbiza humu kwa kweli. Maana watakuwa wanatuweka katika target watulipue
 
Ninavyoelewa mimi waliposema kioo ni kumaanisha utavutiwa na kazi zake na atakuinfluence ufuate nyayo za hiyo kazi.

Mfano wachekeshaji wengi hua wanasema Majuto ndiyo kioo chao.

Hii maana ya kimaadili sijui nani kaileta. Halafu mtu awe hasi au chanya ni atakupa somo tu, ukiona mlevi anapata shida utajifunza kua usiwe mlevi n.k.
Ni kweli kabisa mkuu. Ndiyo uzuri wa hili jukwaa. Tunapanuana mawazo na uelewa wa mambo
 
Back
Top Bottom