Cha msingi ni kukaza tu,Diamond ngoma yake aliyoitoa na Mabovu na Ngwair(rip) Jisachi kabla mfuko haujatoboka full msimbazi kama adili wa choka haikukamata mpaka alivyotoa Kamwambie ikabamba hajakaa sawa akatoa Mbagala ikabamba zaidi na jamaa akawa anatumia teqnik ya kutafuta kiki kwenye media ndio akazidi kuchana.
Diamond anajua kufanya timing, tumpe sifa yeye ni msanii ambaye anajua muziki ni biashara, na huwezi ukapiga muziki mzuri then ukaula ukashiba, ni lazima uuze kwa wanaoutaka muziki wako, yeye huwa anajitahidi kutoka wakati game iko wazi, hakuna mrundikano wa nyimbo nyingi zilizotoka.
Hao wanamuziki walioorodheswa hapo wanalingana sana kiuwezo na Diamond, na wengine wamempita uwezo ila Diamond anajua kutengeneza kiki za media kabla ya kuachia ngoma. Kabla ya kutoa Number 1 kulikuwa na mgogoro wa Wema na Penny, baada ya Wema kupiga simu usiku na kupokewa na Penny.
Wakati inatoka Mawazo kulikuwa na mgogoro wa Wema na Jokate, na wakati wa kutoka Number 1 (Remix) Diamond alikuwa na watoto wa Madrasa, pia wakati anatoa Mdogomdogo alikuwa na msaada wa kusomesha watoto. Na mwezi huu au ujao anatoa ngoma mpya, kiki yake ndio hiyo Morano na BMW.
Diamond anajua kuitangaza biashara yake, na inawezekana anaweza kuwa mwanamuziki wa Bongo anayeandikwa zaidi kwa mambo yasiyohusiana na muziki kabisa. Kwenye birthday party yake kulikuwa na bahasha za khaki kwa blog maarufu na magazeti, redio na TV.
OSATA -Othman suka SAid Fela Na TAle Babu ndio wanaoua mziki wa Tanzania
Ni kweli kabisa OSATA ndio wnawanaua muziki, coz msanii akitoka wakati mmoja na msanii aliye chini ya OSATA ni lazima apotezwe, hata kama alikuwa na ngoma kali namna gani. Ndio maana unaona leo hii msanii kama Snura anabamba na kuonekana mkali kwa sababu yuko chini ya OSATA, lakini msanii kama Mo-Music wa Basi Nenda hajabamba kihivyo.
Ova