Wasanii wanaodaiwa kutumia madawa ya kulevya, ni yupi anayekusikitisha?

Dah! Mtinko kwetu mkuu ...vp na ww mwenyeji nn huko?
Hapana tulikwenda kikazi kukusanya data za hali ya maisha ya mkoa wa singida.ndo nikapangwa kata ya mtinko,kijiji cha malolo,dah! nyie wakarimu sana mkuu nifurahi kuwa pale.
 
Nimekuwa najiuliza sana inakuwaje wasanii wengi wa muziki au filamu wanapenda kutumia madawa ya kulevya (unga) ?

Iwe kwa mastaa wa nje na hapa Tz wengi wanajiingiza kwenye ubwiaji wa unga, au bangi

hebu tujadili chanzo huwa ni nini hasa? Huwa inakuwaje kuwaje hadi msanii anaamua kutumia madawa ya kulevya??

Je, kuna faida zipi wanapata wakitumia?? maana naona hasara zake zinajulikana!
 
Mtu anakuwa kashatumia kila kilevi na kimemzoea kwa extent ambayo hakuna kinachompa "stimu" za haraka kama atakavyo. Kwa kuwa vijisent vinakuwepo anaanza kutumia unga ambao huwa na burudani ya aina yake pale unapoanza kwa mujibu wa mateja wastaafu.
 
Mtu anakuwa kashatumia kila kilevi na kimemzoea kwa extent ambayo hakuna kinachompa "stimu" za haraka kama atakavyo. Kwa kuwa vijisent vinakuwepo anaanza kutumia unga ambao huwa na burudani ya aina yake pale unapoanza kwa mujibu wa mateja wastaafu.
daah hatari sana
 
Mkuu,kwa wenzetu wanatambua kuishi km star ni mtihani mkubwa kuliko kuwa star ndo mana star anakuwa na management team inayomuongoza nn afanye ktk wakat gan na wap.
Tatizo kubwa la mastar hasa wa hapa nyumbani,hawajaandaliwa kuuishi ustar,hivo mtu kutoka kula mlo mmoja hadi kumiliki mamilioni,kutoka kuishi uswaz had uzunguni inawachanganya sn vijana wetu na ile tabia ya kuigiza umagharibi basi ni tatizo.
 
Ukianza kuwa punda utakula na majani.. ..kma ndo wabebaji bas kutumia n jamb ambalo halikwepi
 
Aina ya marafiki wanaowapata baada ya kuwa maarifa... mara nyingi hawaanzagi kununua, wanapewa kama offer... yakiwakolea sasa ndiyo waanza kutumia pesa zao kusaka na kutumia...
 
Madawa yaliyozoeleka bongo yanakufanya uwe chizi kabisa, ni Yale ambayo kwa wenzetu huko america labda mtu apigike ndo anatumia, haya madawa ni kama methamphetamine na crack cocaine(cocaine kiduchu inachanganywa na fuko Zima la baking powder), iwaje usiwe kichaa, about ile kitu pure ya cocaine ambayo ni 150,000 kwa gram kibongobongo haipo sana, safest way kwa hawa wasanii wetu wapige ganja natural tu hayo madawa ni shida
 
makundi tu bila kujali ni wasanii au la....mana kuna wasanii wanakitambua nakujielewa hivo hivo kwa ma engineer doctorswatu engine wanajitambua tu ila makundi mabaya ...kuwa msanii sio kwamba ndio una tabianjema au makundimazurihumo humomajanga pia...so akili yako tu
 

SABABU WAUZA MADAWA WANAPENDA KUWATUMIA Wasanii.
 
Alafu wakishaathirika wanaikimbilia jamii eti oooh nahitaji msaada niachane na haya madawa mara oooh nipo kwenye wakati mgumu ,wateja watu wa ajabu sana tuache kushughulikia mambo ya muhimu kama watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu alafu tushughulishwe na mateja mtusameee,kwanza na imani katika vipato vyao hakuna anayewakumbuka hawa watoto yatima wengi wanatumia pesa zao kwa starehe tu.
 
Umenivunja mbavu fuko zima la
Bakin powder
 
Nahisi ni ushamba flani wasanii wetu wanao. Wakishapata vihela na umaarufu basi wanajiona wako juu ya dunia.

Kufanya kitu ili mradi umefanya/hawana future na matokeo yake hata hela wapatazo zinakua ni kama hazina kazi ya maana na kwa ulimbukeni wanaamua kujiingiza kwenye madawa hayo wakidhani ni sifa...

Ifike mahali wasanii wetu wajitambue,wapi wametoka na wanalenga kufika wapi? Ni vizuri kua na nidhamu ya maisha yako
 
Nature ya kazi zao inawagharimu pakubwa.

Tofauti na kada zingine, msanii anaweza kutengeneza mamilioni ya pesa kwa kazi iliyomchukua mwezi mmoja au hata chini ya hapo kuandaa.....hivyo pesa nyingi ukijumlisha na muda mrefu wa kukaa idle ni rahisi sana kuingia mtegoni.

Na hata Wauzaji huwa na mikakati maalum ya kuwalenga kundi hilo kwani wakishapata pesa na hawana kazi zinazowabana, wanatumia muda mwingi sehemu za starehe ambako ndipo Wauzaji/Washawishi huweka mitego yao.

Mfanya biashara au Mtu aliyeajiriwa anakuwa ndani ya "ulingo"...yaani anaongozwa na ratiba ambayo humlazimu kuingia kazini asubuhi na kutoka jioni...na muda kidogo anaopata sanasana ataishia kunywa bia mbili tatu bar, na hakuna Washawishi wanaowazengea.

Pia kumbuka asilimia kubwa ya wasanii sio Wafanyabiashara (hawana asili/akili ya kuendeleza mapato).....pia wengi wao wanatokea kwenye jamii zilizokosa fursa rasmi kama Elimu n.k.....hivyo kupata kwao pesa nyingi ndani ya muda mfupi inawachanganya sana akili...tofauti na yule mwenye asili/akili ya kibiashara ambaye kila shilingi anayoipata kwake ina thamani na hayupo tayari kuipoteza.....

Usishangae kumkuta Mzee Mengi ametulia tuli...ukamuuliza kulikoni Mzee...akakwambia alikuwa na elfu mfukoni sasa anashangaa haioni, hivyo anajaribu kukumbuka aliitumia saa ngapi......lakini Wasanii wengi wala hawaoni uchungu kutumia pesa aliyoingiza kwa muda mfupi.
 

This is very true. Niliona kwenye ile movie ya Get Rich or Die Trying.

Walikua wakimix the solution wit baking powder making a cheaper drug in the market na walipiga hela balaaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…