Wasanii wote wa Wasafi Festival wapigwa ban Clouds

clouds ni redio binafsi waacheni wafanye kulingana na biashara yao, acheni kulialia ililieni Tbccm ipige izo nyimbo zenu.
 
Nitashangaa msanii akilia wakati kuna redio kibao,plus Youtube,Insta,Fb,Boomplay,Sportfy nk cha msingi hakikisha kila nyimbo unayotoa ni jiwe,mbona watakufuata wenyewe na wakikufuata wewe ndiye unawapa terms zako basi.
 
Ndo maana mtu kama country boy,mchizi moni sikuhizi hawawapi tena promo.
 
waache kutegemea redio na televisions, waweke nguvu zao kwenye social networks kama YouTube ,Instagram na Facebook.

Waige mfano kwa wasanii wa comedy wanaoanza kufanya comedy Instagram hadi wanatafuta na media na kusikika,base fun wanaanza kuifanya kwenye social network then media inafuata,sio unaanza kwenye media unakuja social networks.

Hakuna anayesikiliza redio na kusoma magazeti siku hizi.
 
Juma Nature kafanya Wasafi na atakuwepo kwenye tigo fiesta 22
 
Ndo maana mimi naikubali wcb media. Wazee WA chombo kwa hewa
 
Mbona mimi masongi yangu yanapigwa kama kawaida clouds, na nilishiriki wasafi festival.
 
Kosa walilolifanya wasafi kuja kutaka upinzani na CMG...EFM ilivyoanza walikuja na style hiyo kiko wapi...Diamond "wapambe" wako wakina Tale wanàkupotosha...ungekuja kimya kimya bila ya beef na MTU...mfano CMG walivyoanza walikuta Radio one ya Mengi ikiwa moto..walichofanya wao kuwa na vipindi bora sio kuwatukana wala kuleta beef nao...mpaka leo Clouds FM iko juu ya Radio one...tafuta vichwa hao jamaa zako wakubebee mabegi ukisafiri tu...
 
Wakati huko majuu kuupiga wimbo wa msanii bila kumlipa ni kosa la jinai, huku kwetu wanalilia nyimbo zao zipigwe bure kwenye media.
Masikini kujikwamua ni muujiza na sii haki wala stahiki yake.
 
Watu wanaroho mbaya sana.

 
Wasanii wanakosa gani? Wasanii ni service providers kwa haya matamasha, kosa lao silioni.
 
Watu wanaroho mbaya sana.

Dogo kahustle sana,fikiria tu mfano THT iliyo chini ya wanyonyaji wakubwa wa clouds walimwambia hawezi kuimba wakamkatalia kuingia huko,dogo akatumia njia anazozijua akaja kutusua tena kinoma noma,sasa hv wanamwonea wivu,wanaona hawana mchango ktk kumfanya awe hivyo alivyo ndio inakuwa nongwa kwa kuwa hawataweza kumwendesha kama rimoti

Dogo kaanzisha festival yake kidogo tu walionza kabla yake wanajambajamba tu,katoa misaada kwa jamii balaa,hao walioanzisha fiesta sijawahi kuona mchango wao hata mmoja kwa jamii.

Amini usiamini dogo yupo pamoja na Mungu ingawaje ana mapungufu kama mwanadamu,lakini ana mazuri mengi sana kuliko wengine,dogo kwa,kweli ameonewa,hata justice to be held haikufanyika,tena hadi na vyombo vya serikali,ilikuwa,apigwe fine kubwa kidogo ili ajutie lakini sio kumharibia career yake.

Wana roho mbaya mno na hawataweza
 
Kabisa Mkuu halafu anakuja mburula anataka kumzibia riziki yake kwa kumzuia kuperform hata nje ya nchi ambako hakuna anayejua basata ni mdudu gani.

 
Kabisa Mkuu halafu anakuja mburula anataka kumzibia riziki yake kwa kumzuia kuperform hata nje ya nchi ambako hakuna anayejua basata ni mdudu gani.

Inauma sana mkuu
 
Ujinga hauondoki kwa kumchukia mwelevu waambie clouds media
 
Hahaha, mi sijui hata ka kuna kitu kinaitwa radio
Wabadilike aisee, wafanye bifu za kiutuuzima. Sahv watu wanashindana viewers YouTube baada ya kutoa ngoma wao wanapigiana zongo redioni, bado wapo gizani aisee.
 
Ok nakupa homework ndani ya miezi hii miwili ukisikia nyimbo za msanii yoyote aliyeimba kwenye wasafi njoo unisute.
JF ya siku hizi bana,
Sasa ukisutwa utaathirika vipi? Na msutaji atafaidika vipi? By the way neno kusutana limekaa ki dada dada hivi. We sema labda tumuweke Mod mmoja shahidi ikitokea nyimbo zimepigwa ulambwe Ban
 
Maigizo tu haya,
CMG na WCB zote za Kusaga in one way or another.
 
Kwan kabla zilikua zinapigwa? Si ni kina dudu baya, kina juma nature, stereo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…