Evelyn Salt
JF-Expert Member
- Jan 5, 2012
- 70,916
- 141,437
Kwanza hongereni kwa michango yenu ya kujenga, huwezi kupita jukwaa hili usipate kitu kipya.
Ila pia kwa upande mwingine baadhi ya washauri, wachangiaji ni wakatishaji tamaa sana.
Mtu anaomba kujua biashara flani labda mtaji anasema ana million 1 majibu yake sasa, milioni si kitu, hiyo biashara huiwezi kwa hela hiyo andaa million kumi chaaa!!! Jamani hivi humu tuna assume kila mtu ana mtaji wa mamilioni?
Nlikua nacheki threads za biashara ya salon za kiume nmechoka na michango, kwamba kiti cha salon andaa million mbili, poda na mashine laki tano, mara kiti cha scrub laki tano yani unapewa hesabu za million kumi,hadi hapo tu nguvu zinaisha. Hakuna options kulingana na mtaji? mwenye mil 1 afanye cha mil 1, mwenye mil 10 afanye cha mil 10. Mfano mtu mwenye salon mitaa ya chuo au uswazi anategemea wateja wa hali ya kawaida tu hayo ya scrub sidhani kama ni ishu.
Kuna salon moja nlikua naenda yani hako kachumba mkiingia watano mmejaa, kana mashine moja, viti vya plastic viwili, vioo viwili na radio, kiti kimoja kunyoa kingine kutengeneza dreads kwa mwonekano utadhani stoo ila wateja sasa, gari zinazopaki hapo ni shida,mtu anakuja kuweka foleni then anaenda kazini atarudi, kila kichwa cha dread ni elf 10 kunyoa elf mbili jamaa wapo busy hadi usiku na hakuna cha mbwembwe za makochi wala nini wengine tunasubiri nje kwenye matofali.
Wadau mnaotaka kuanza biashara msikatishwe tamaa, jikune mkono unapofika, hicho kidogo ulichonacho anza nacho, mchina mwenyewe bidhaa zake zipo kulingana na hali ya kila mtu ukihitaji cha garama utapata na mwenye hela ndogo atapata hicho hicho ila chenye quality sawa na hela yake.
Msitukatishe tamaa wenye mitaji ya kuunga unga, ni hayo tu.
Ila pia kwa upande mwingine baadhi ya washauri, wachangiaji ni wakatishaji tamaa sana.
Mtu anaomba kujua biashara flani labda mtaji anasema ana million 1 majibu yake sasa, milioni si kitu, hiyo biashara huiwezi kwa hela hiyo andaa million kumi chaaa!!! Jamani hivi humu tuna assume kila mtu ana mtaji wa mamilioni?
Nlikua nacheki threads za biashara ya salon za kiume nmechoka na michango, kwamba kiti cha salon andaa million mbili, poda na mashine laki tano, mara kiti cha scrub laki tano yani unapewa hesabu za million kumi,hadi hapo tu nguvu zinaisha. Hakuna options kulingana na mtaji? mwenye mil 1 afanye cha mil 1, mwenye mil 10 afanye cha mil 10. Mfano mtu mwenye salon mitaa ya chuo au uswazi anategemea wateja wa hali ya kawaida tu hayo ya scrub sidhani kama ni ishu.
Kuna salon moja nlikua naenda yani hako kachumba mkiingia watano mmejaa, kana mashine moja, viti vya plastic viwili, vioo viwili na radio, kiti kimoja kunyoa kingine kutengeneza dreads kwa mwonekano utadhani stoo ila wateja sasa, gari zinazopaki hapo ni shida,mtu anakuja kuweka foleni then anaenda kazini atarudi, kila kichwa cha dread ni elf 10 kunyoa elf mbili jamaa wapo busy hadi usiku na hakuna cha mbwembwe za makochi wala nini wengine tunasubiri nje kwenye matofali.
Wadau mnaotaka kuanza biashara msikatishwe tamaa, jikune mkono unapofika, hicho kidogo ulichonacho anza nacho, mchina mwenyewe bidhaa zake zipo kulingana na hali ya kila mtu ukihitaji cha garama utapata na mwenye hela ndogo atapata hicho hicho ila chenye quality sawa na hela yake.
Msitukatishe tamaa wenye mitaji ya kuunga unga, ni hayo tu.