the mkerewe
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 232
- 14
Nina madem wanne kwa pamoja ila hawajuani, watatu wanajulikana sana kwa marafiki zangu ni wa hadhi ya juu (wanatoka famila za wafanya biashara.Wa nne anatoka mabibo loyola kwao naamini hawataweza kumudu kulipa bei mpya ya umeme uchumi hoi.kati ya wote WA MABIBO ananidatisha haitaji mitoko mikubwa,kila nguo nikimnunulia inamfaa,hana makuu, ngozi na sauti yake vinaakisi upole alionao,haongea kimashauzi,hukataa jambo kwa hoja sio kwa hulka, huvaa nguo za kumfunika,hupenda kuzibana nywele kwa nyuma, yaani she is natural nikimwona uchovu wa kazi na hasira za mabosi na watawala hiniishuka haraka ila yeye halijui na staki ajue manake atajiskia.Natamani nikampangie chumba ila halikubaliki.NATAKA NIWAACHE HAO WATATU ILA MABESTI ZANGU WANAMKATAA WA MABIBO kisa kwao na siyo aina yetu.UKWELI NIMECHOKA maisha ya kujiachia nataka demu wa kumjali anijali,wa kunizalia na kunilelea na wamabibo ndiye mwenye hiyo sifa hata kama familia yao itajakuwa mzigo kwangu.HAWA MABESTI ZANGU NAFANYA NAO MRADI unaonipa kiburi ya kuishi na kufanya fujo wikiend huku mipango ikisogea