Wasi Wasi wa Udini

Status
Not open for further replies.
Wazanzibar wanataka kucheza UPATU na hiyo OIC.... wapewe uhuru huo, hiyo ni haki ya mke ndani ya ndoa -MUUNGANO. Bara hatuna haja kabisa ya kujiunga na OIC isipokuwa madai ya Zanzibar sasa hvi kutaka kujiunga na EAC kama nchi, hii inaleta kidogo Mushekeri....
Kuuvunja MUUNGANO yaani ndoa, huu utakuwa utaratibu mwingine kabisa nje ya OIC.... na kama kweli wamepania mimi naomba tu ifanyike referendum Zanzibar!... Tuwaache wananchi wenyewe waaamue baada ya kujua faida na hasara za kuvunja muungano. Nina hakika ya asilimia zaidi ya 50 watasema - HAPANA!...
 
muungano hauhitaji referenda kuuvunja

issue iliopo kila mmoja hautaki kilichobaki ni kutoa taarifa tu bas

wabara nao hawauhita ji na kilichobaki ni kukubali uvunjwe kisha tuendeleee na mabalaa yetu ya kutafuta wachawi

no big deal -HAUKUWEPO,UKAWEPO ,UNAWEZA USIWEPO TENA
 
Mimi nna swali:

Katika mashindano ya Kombe la Challenge, Zanzibar hushiriki kivyake na bara kivyake ... kana kwamba ni nchi tofauti. Lile hufanyika kwa misingi gani? Je misingi hiyo yaweza tumika kuiruhusu Zanzibar kujiunga na OIC?
 
kulikoni,
ZNZ walijaribu kujiunga na FIFA kwa misingi hiyo hiyo ya uanachama wa CECAFA, lakini wakakataliwa kwasababu hawatambuliki kama nchi. FIFA inaitambua Tanzania. kwa msingi huo huo, ZNZ haiwezi kujiunga na vyombo vingine vya kimataifa kama UN, OAU, EA,SADC,COMESA, etc.

Mapendekezo yangu ni kwamba Tanzania ijiunge na OIC. kama kuna misaada au miradi yoyote tutakayopata kutokana na uanachama wetu, basi ielekezwe kule ambako inahitajika.
 



Mjomba you are missing the point

agreement ya watu ni kuwa hatutaki muungano sasa ya nini kujiunga na OIC for the sake of Zanzibar?

watu wana move on na wao wamove on bas

sasa cha kujadili ni namna ya KUUVUNJA huo muungano
 
Bara nzima yenye wananchi 34,000,000 hatuwezi kuvutwa kama gari bovu na wananchi 950,000 wa Visiwani, kwenda kuingia hiyo kitu mbovu,

Referrendum? Ya nini kwani ulipoanzishwa ilifanywa? Sasa Why Now? Unless kama kwenye hii forum kuna wanaoelewa sababu za kimsingi za kuendeleza huu Muungano, faida yake so far toka uwepo maana wote tunajua hasara zake tayari,

Jamani wazee wanaofahamu faida zake waziweke hapa zijadiliwe, maana hasara zake tayari tunazifahamu?
 

faida na hasara zilishakuwa discussed zaidi ya miaka 30 iliopita hivyo hatuna haja ya kujadili kitu hichi...na hii leo 2006 naona ni hasara tuuu hivyo basi dawa ni kuuvunja tuuu hivi wewe unaona bora tuu watu wa bara wawalipie bili za Umemem watu wa Zanzibar? wao wanaishi kwa INCOME SUPPORT ZA WABARA at the same time wao wanaona kuwa tunaungangania muungano na hatuwaruhusu kuwa na marafiki sasa whats the point?

hoja za kuzungumza ni NAMNA YA KUUVUINJA MUUNGANO bwana ES
 
Jamani bandugu tusifanye hasira tukasahau kuwa swala hili ni zito sana. Mkidai sababu ya kwamba Muungano ulifanywa na baadhi ya watu ni sawa kabisa na kusema tunaweza kuamua kuua hata UHURU wetu kwa sababu walioamua tupate UHURU ni baadhi ya watu.
Faida zake zipo millioni na kama unaamini kuwa UNITY is Strength!... Together we can make different.. hayo ni machache tu yenye maana nzito.
Kuwapa Umeme Zanzibar bure hii ni habari tunaitunga sisi. Navyoamini mimi hizo Hydro power zimejengwa baada ya Muungano... Kwa hiyo kujengwa bara haina maana Zanzibar wako nje ila walichangia kwa hali na mali kama wakazi wa Mwanza,Bukoba, Songea n.k. Kumbukeni tu mali yote iliyopatikana ndani ya ndoa ni ya familia.. MUME na MKE!
Kisha utaratibu wa kisheria siku zote huondoa mzozo na mfano mzuri ni huo wa CCM. Kila kukicha utasikia matusi na maneno mengi kuikashifu lakini inapofikia Uchaguzi mshikaji CCM siku zote mbele!..INASHINDA!
Sintashauri kama infringing on the autonomy of the Zanzibar revolution Government is the way to go!....Isipokuwa referendum itasema - PEOPLE have spoken!
 
Mimi sidhani kama kuna haja ya kuregeza kamba katika hili..uzi ni ule ule, hata hao Georgia na Uzbekistan waliona bora wawe huku kuliko kuwa ndani ya Urusi sasa UMOJA NI NGUVU ndani ya ukandamizi wapi na wapi?

wananchi hawalitaki hili ni hili linaonekana kuwa ni pet oproject ya wakubwa sasa ninitena kurudi nyuma

?
 
Dr. WHO,

Hiyo njaa iliyoko Georgia na Uzbekistan mshikaji haisemeki tena wenzetu wanakila kitu - Utajiri wa mali na elimu, leo sisi tukijatengana na hio Uzi usiokuwa na mwanzo mbona tutakuja kulana wenyewe!... hawa wasomi wetu wafuga ng'ombe wa kizungu unafikiri watatufikisha popote!
Usiambiwe na mtu wananchi wa nchi hizi wote wanajuta kuvunjika ktk USSR na sio tu wamepoteza Superpower, wanalaani SIASA. Russia ndio kwanza wanazidi kuyoyoma mbele.
 
hiyo haiondoi sababu ya kuvunja muungano wa Tanganyika na Zanzibar

maana hakuna anayekubali la mwenzie sasa whats the point?
 
Dr. WHO,
Navyoamini mimi, Bara na Zanzibar sio kwamba hatukubaliani isipokuwa hakuna mawasiliano mazuri na hasa toka Bara. Bara hapendi kabisa kusikia na kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya Zanzibar.
Nafikiri Uchaguzi wa JK kuwa rais wa Jamhuri yetu ulitoa ishara kwamba Muungano hauna matatizo isipokuwa utekelezaji mbaya ya matatizo ya Zanzibar.
Sherehe za Muungano mwaka huu zilifana sana sehemu zote duniani. Ilinikumbusha enzi za Nyerere. Wazanzibar kwa Wabara walikutana kila kona kusherehekea wakitumai mkombozi katokea kuondoka kwa matatizo hasa ya Zanzibar.
Nothing happened hadi sasa... mke bado kafungiwa ndani hana ruhusa ya kutoka nje!....Mshikaji, mbinde hapa!
Bara bob tunajijeuri fulani cha kutaka ku - control Muungano. na kibaya zaidi sijui kwa nini lazima YES itoke BARA ndipo swala linalohusu Zanzibar likubalike!...
JK aliahidi bunge kuwa kufkia August mwaka huu kutakuwepo na mabadiliko makubwa, jambo ambalo hakulifanya na Zanzibar wana kila haki ya kulalamika. Bara tunaukataa Muungano kwa sababu wengi wetu hatujayatazama matatizo ya ndani ya Zanzibar. Tunatumia UBWANA na ku-control nyumba hali muda mwingi tunacheza bao tu na kulaani sana Umalaya wa mwanamke. Kisha basi sisi wenyewe vifagio! tunazidisha U -PLAYER nje mara utasikia Wasouth, Malaysia, Richmond -USA, Thailand na kwingineko!
 
Ndugu yangu Mkandara,
Unajua kinachonisikitisha juu ya maoni ya watu kama dakta Who ni kwamba kama huu mwungano ungetengenezwa na Waingereza, mathalan, leo kusingekuwa na malalamiko. Lakini kwa kuwa Wabantu wawili, Nyerere na Karume, walidiriki kufanya ambayo Wabantu hawakutarajiwa kufanya, kuna kuhoji, kukebehi, kulalamika, ad infinitum, juu ya huu mwungano. Unajua nini? Marekani walivamia Hawaii. Wakamwua mfalme wao, wakawaingiza kwa nguvu katika mwungano. Texas na Mexico zilichukuliwa kwa mtutu wa bunduki. Do I need to say more?
 



Kuna ubaya gani kuhoji? mfano juzi juzi Ikulu ya Zanzibar iliungana na aliyewahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Bw. Wolfgang Dourado, kudai kwamba marekebisho ya katiba ya 11 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yalikiuka makubaliano ya muungano kwa kumnyang'anya umakamu wa rais wa Jamhuri ya muungano, na wakashangaa ni vipi ja,mbo hili halijahojiwa na hao wabunge wa muungano amabo sasa wanaipigia kelele Zanzibar kuizuia isbadilishe katiba yake bila ridhaa ya serikali ya muungano

sasa ndio maana nikasema kwa nini tusiuvunje muungano?


maana kama kila kitu ni TOP SECRET inkuwa ngumu hata kufanya hayo marekebisho ya katiba na hili la ku question mambo ndio watawala wetu hawatotuonyesha hiyo mikataba ya MADINI,IPTL,TANESCO,na mengineyo kwa sababu tunafanya dhambi
 
Dr. WHO,
Vipi tena sii wewe uliyepinga mpango wa Vote?...Quebec huko Canada wanataka watambuliwe kama nchi ndani ya nchi na inaonyesha safari hii itapita kwa sababu vote zinaonyesha kuwa wananchi wengi wa Quebec wanapendelea mgawanyika wa aina hiyo. Miaka Mitano iliyopita walishindwa kuifanya Quebec nchi nje ya Canada baada ya kura za kukataa kuzidi kwa asilimia ndogo sana. Walikubali kushindwa hawakutumia nguvu wala hila za kusema wanajitenga.
Hawakukata tamaa wamelirudisha tena swala hili kwa lugha tofauti na vote pekee ndio demokrasia ya kweli. Who knows wanaweza kufanikisha safari hii.
 
hiyo referendum wapige wazanzibari. watanganyika hawana hata habari kama huu muungano upo. tutawapotezea muda tu.
 
sure joka we dont give a damn kama hawa jamaa wapo AU la afterall zanzibar ni kama wilaya tu so if they want to stay we can just keep on subsdise them but if they want to part its upon them ,but i feeel sorry for there unity ,and rasilimali especially unguja hamna chanzo zaidi ya utalii na uvuvi at least pemba kuna karafuu,uvuvi na mafuta sasa muungano ukifa leo na zanzibar inameguka sasa its up to them to decide,wangemsikiliza jk waunde serikali ya pilau at least kuwe na usawa kiutawala
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…