Wasi Wasi wa Udini

Wasi Wasi wa Udini

Status
Not open for further replies.
Dr. WHO,
Ndugu yangu umesema mengi sana mazuri na hata umeweza kutoa dhana zako binafsi kwa kuwahukumu watu wa upande huu lakini ajabu umekataa kabisa hukumu za upande huu. nadhani hoja ni muhimu zaidi ya kunyoosha vidole hali hakuna mtu Dito hapa ukumbini.
Unaposema kukamatwa kwa masheikh baada ya Uhuru hapa bado sijakuelewa!.. una maana uhuru wa Bara au Zanzibar?..
Kisha kifungu cha kwanza cha makamu wa rais na rais wa Zanzibar hapo pia sijaweza kuelewa vizuri. Je, hapa unazungumzia kuwepo kwa Karume na Shein ni uvunjaji wa kanuni?
Kisha umeendelea kusema:-
Katika mkutano, Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi uliofanyika Dodoma, chama kilipitsha azimio kwamba suala la Urais wa Zanzibar na katiba likajadiliwe katika vikao vya Chama Cha Mapinduzi Zanzibar. Je unajua kuwa wananchi walihoji ni lini Kadinali na wanasheria wa Chuo Kikuu na Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi wa Tanganyika walipewa mamlaka ya kutengua maamuzi ya mkutano mkuu wa Chama Cha Mapinduzi na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
Hapa pia nimekwama kwa sababu sioni uhusiano uliotolea mfano wa hoja - Uhusiano kati ya vikao vya Chama cha Mapinduzi Zanzibar na huyo Kadinali ama wanasheria wabunge n.k
Inawezekana kabisa labda nimeingia katikati ya hoja hii ndio maana sielewi kinachoendelea lakini kinachonishinda zaidi ni kuwa hawahawa Wazanzibar wanaomkataa Karume kama rais wa Zanzibar na kumwita kila majina ya Usaliti... leo hii tena amekuwa mtume!..Where do U guys stand?
 
labda ungesoma hiyo ilipita kabla hiyo ulio quote then ungeelewa from where i was coming from

usiku umekuwa mwingi

tutaendelea tena kesho panapo majaliwa
 
Dr. Who,
Nimesoma toka hiyo ya nyuma lakini sikuona huo Uhuru unaozungumzia kuwa walikamatwa masheikh! navyojua mimi wakati wa mapinduzi kuna watu walikamatwa. Well, kwanza hapa lazima tuelewe nini maana ya neno MAPINDUZI!.. hili halina kheri kabisa kwa nchi yeyote ile.
Swala la tanganyika kuimeza zanzibar sijui linaweza kuelezeka vipi tofauti kwani hata kama rais akitoka Zanzibar bara wataweka madai kuwa wanamezwa na Kisiwani. Tatizo hapa sii muungano isipokuwa sisi bado tumeweka tofauti baina yetu. Yaani kuna Mume na mke hapa!... Hiyo Sovereign Republic ni maandishi tu ndani ya katiba lakini watu wenyewe hatuyatambui zaidi ya haki ya kuwepo a sovereign state - Zanzibar!.
Kwa hiyo Dr. kama tukiondoa hizi hisia zetu za kutengana sidhani kama tunaweza kubishana hata hili swala la OIC na mengineyo mengi tu. Mbona Marekani sijawasikia wakidai kuwa rais katoka Texas kwa hiyo states nyingine zote zinatawaliwa?...
Kisha habari ya Muungano huifahamu na hata hao wanaohadithia hawaifahamu kwa sababu wengi wao walikuwa wanachama wa Hizbu. Na ndio hawahawa wanaodai leo hii kutaka kuona huo mkataba wa Muungano kwa sababu hawakushirikishwa... wamesahau kabisa kuwa wao walikuwa wamepinduliwa serikali yao na baadaye kurudishwa ndani na kuunda chama kimoja. They were not part of Mapinduzi na nakuhakikishia wote hawa hawapenmdi kabisa kusikia baraza la mapinduzi! Lazima tukubali kwamba uhasama kati yao bado upo hadi kesho na bara au CCM ni kisingizio tu.Hizi ni cheche za mgawanyo toka kwao na haiwezekani bila kulimenya chungwa (Tanzania) zima ili upate vipande vyake.
Muungano wa Zanzibar ulipangwa kama yalivyopangwa mapinduzi! Plan ilikuwa moja na wahusika wakuu wa mapinduzi ndio waliokuwepo ktk muungano. Kwa hiyo huo muda wa miezi ni wewe una uona sio wanamapinduzi wenyewe. Hizo habari za CIA na mengineyo yote vichombezo tu kwani Okello hakutokea Marekani na pia unafahamu vizuri marekani wakitaka kitu hufanya nini. Tuliyaona Congo kwa Patric Lumumba, Nuriega na hivi sasa Saadam. Lazima marekani apandikize mtu wanayemtaka na Nyerere asingewashinda kwani walijua vizuri kuwa ni Mjamaa.... Hotuba zake za mwanzo kupinga Kutawaliwa na uchumi kumilikiwa na wageni ni ushahidi tosha kwa Marekani kuelewa Nyerere alikuwa kundi gani.
Hata hivyo, binafsi swala la OIC naamini ni haki yenu kuamua mnavyotaka kwani Zanzibar ni mke mwenye imani yake ya kidini. Hiyo katiba inasema Tanzania hakuna dini lakini ukweli utabaki kuwa - Zanzibar kuna DINI....
Kwa mantiki hiyo mimi naamini kuwa nyumba (Tanzania) inaweza kabisa kutokuwa na dini lakini mume na mke wakawa na imani zao tofauti, yet maintain relationship bila kuingiza maswala ya dini kwa nia mbaya. Yes, kila mmoja wao anaweza kutokuwa na imani na dini ya mwenziwe lakini swala hapa ni uhusiano wao ndio muhimu. Na nyumba zote zinazoweza kudumu ktk ndoa ya dini tofauti huwa zinaliweka swala hili kama swala la mtu pekee!..
Kwa hiyo Zanzibar kama wanataka kucheza Upatu na OIC wacheze but not on our expense!..
 
Mkandara said:
Dr. Who,
Nimesoma toka hiyo ya nyuma lakini sikuona huo Uhuru unaozungumzia kuwa walikamatwa masheikh! navyojua mimi wakati wa mapinduzi kuna watu walikamatwa. Well, kwanza hapa lazima tuelewe nini maana ya neno MAPINDUZI!.. hili halina kheri kabisa kwa nchi yeyote ile.


Nadhani hukunielewa nilikuwa namuongelea Nyerere aliyewakamata hao ma sheikh na sikuzungumzia masheikh waliokamatwa zanzibar...Sijui uelewa wako wa hili suala zima la mapinduzi likoje lakini ningependa kukufahamisha kuwa si mapinduzi yote lazima DAMU IMWAGIKE kwa sababu Georgia kulikuwa na velvet revolution na hivi juzi kulikuwa na revolution nyingine THAILAND ambako bwana Thaksin liondolewa bila damu na wananchi wameliridhia hiyo sasa hebu rekebisha hilo...revolution si lazima damu imwagike


Swala la tanganyika kuimeza zanzibar sijui linaweza kuelezeka vipi tofauti kwani hata kama rais akitoka Zanzibar bara wataweka madai kuwa wanamezwa na Kisiwani. Tatizo hapa sii muungano isipokuwa sisi bado tumeweka tofauti baina yetu. Yaani kuna Mume na mke hapa!... Hiyo Sovereign Republic ni maandishi tu ndani ya katiba lakini watu wenyewe hatuyatambui zaidi ya haki ya kuwepo a sovereign state - Zanzibar!.
Kwa hiyo Dr. kama tukiondoa hizi hisia zetu za kutengana sidhani kama tunaweza kubishana hata hili swala la OIC na mengineyo mengi tu. Mbona Marekani sijawasikia wakidai kuwa rais katoka Texas kwa hiyo states nyingine zote zinatawaliwa?...



Well..waasisi wa muungano huu wamekuwa wakieleza kuwa waliamua kuziunganisha nchi mbili hizi, kutokana na sababu za kihistoria. Wanasema wananchi wa nchi mbili hizi wana asili moja na uhusiano wa karibu. Ni kweli Watanganyika na Wazanzibar wote ni Waafrika. Hilo halina ubishi. Na wala Zanzibar kuwa ni kisiwa hakuwezi kuwa ndiyo sababu ya kuvitenganisha visiwa hivyo vya Zanzibar na Bara la Afrika.Kwa vile wahenga wamesema "umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu",Lakini muungano wa nchi ni maridhiano baina ya wananchi wa zile nchi zinazohusika. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar umekuwa na migogoro mingi tokea ulipoundwa. Nini kilichosababisha migogoro hiyo? Au kwa vile wananchi hawakushirikishwa? na kwa nini huoni umuhimu wa kurudia katika contract kuangalia kuna mamabo gani yamekiukwa na ikishindikana GET OUT CLAUSE inasemaje?






Kisha habari ya Muungano huifahamu na hata hao wanaohadithia hawaifahamu kwa sababu wengi wao walikuwa wanachama wa Hizbu. Na ndio hawahawa wanaodai leo hii kutaka kuona huo mkataba wa Muungano kwa sababu hawakushirikishwa... wamesahau kabisa kuwa wao walikuwa wamepinduliwa serikali yao na baadaye kurudishwa ndani na kuunda chama kimoja. They were not part of Mapinduzi na nakuhakikishia wote hawa hawapenmdi kabisa kusikia baraza la mapinduzi! Lazima tukubali kwamba uhasama kati yao bado upo hadi kesho na bara au CCM ni kisingizio tu.Hizi ni cheche za mgawanyo toka kwao na haiwezekani bila kulimenya chungwa (Tanzania) zima ili upate vipande vyake.


Huhitaji kuwa mwanachama wa HIZBU kuona CONTRACTS za muungao after all hili linawagusa wananchi milioni 40 sasa iweje mikataba muhimu kama hii iwe siri? hivi leo hii 2006 uko moto juu kuhusu mkataba wa RICHMOND lakini hutaki kusikia kuhusu mkataba wa muungano hii haingii akilini sasa watoto wetu mashuleni wanafundishwa nini...uozo au propaganda? kwa nini wasifundishwe kuhusu katiba yao au mambo ya muungano na mojawapo ni hiyo contract? labda kwa kukupa ushauri wa bure nadhani ungeanza na kuangalia huo muungano waliufikia vipi kwa kusoma kitabu kilichoandikwa na Amrit Wilson kiitwacho "Uhasidi wa Marekani kwa Mapinduzi ya Zanzibar"

Muungano wa Zanzibar ulipangwa kama yalivyopangwa mapinduzi! Plan ilikuwa moja na wahusika wakuu wa mapinduzi ndio waliokuwepo ktk muungano. Kwa hiyo huo muda wa miezi ni wewe una uona sio wanamapinduzi wenyewe. Hizo habari za CIA na mengineyo yote vichombezo tu kwani Okello hakutokea Marekani na pia unafahamu vizuri marekani wakitaka kitu hufanya nini. Tuliyaona Congo kwa Patric Lumumba, Nuriega na hivi sasa Saadam. Lazima marekani apandikize mtu wanayemtaka na Nyerere asingewashinda kwani walijua vizuri kuwa ni Mjamaa.... Hotuba zake za mwanzo kupinga Kutawaliwa na uchumi kumilikiwa na wageni ni ushahidi tosha kwa Marekani kuelewa Nyerere alikuwa kundi gani.


Mzee Mkandara unazidi kujionyesha jinsi gani suala hili linavyokuchanganya kwa sababu kama akina marehemu ABDUL RAHMAN BABU kutaka kuthibitisha kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulitokana na mpango wa Marekani wa kutaka kulinda maslahi yake dhidi ya nchi za Kikoministi BABU alimquote mwandishi wa Kitabu hicho hapo juu , Bibi Amrit Wilson anaeleza, "siku ya tarehe 5 Machi (1964), Dean Rusk (Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani, katika kipindi hicho) alituma simu kwenye ofisi za ubalozi wa Marekani Dar es Salaam, Nairobi na Kampala, kuwaagiza maafisa wa Marekani kuwasihi Nyerere, Kenyatta na Obote wamfahamishe Karume kuhusu hatari ya chama cha ASP kumtegemea BABU na hatari anayoleta Babu..... kwa usalama wa Zanzibar na Afrika Mashariki kwa jumla....." soma ukurasa 51.

Simu hiyo ya Dean Rusk ililenga katika kuwashawishi viongozi wa nchi za Afrika Mashariki wawatanabahishe Nyerere na Karume juu ya hatari iliyokuwa inaweza kuletwa na Babu na makomredi wenziwe katika nchi zao. Kwa mujibu wa maelezo yaliyomo ndani ya simu hiyo inaonesha Marekani ilikuwa ikimwona Kenyatta kuwa alikuwa akiuelewa vyema ubaya wa Babu. Ndiyo Marekani ilipoona jitihada zake za kuwataka Nyerere aiunganishe Tanganyika na Zanzibar zimegonga mwamba ikaona imwombe Kenyatta awashawishi Nyerere na Karume juu ya kuziunganisha nchi zao, kwa usalama wao wenyewe.

Simu hiyo iliendelea kusema, "Haitakuwa jambo la busara kuifufua tena kwa Nyerere, mbali ya kukataa kwake kwa awali, fikra ya shirikisho la Zanzibar -Tanganyika kama njia mojawapo ya kumpa nguvu Karume na kupunguza mamlaka ya Babu? Hatua kama hiyo kwa wakati huu itasaidia pia kuimarisha nafasi yake mwenyewe Nyerere.

Siku hiyo ikamalizia kwa kusema, "vinginevyo, ukichukulia mwenendo wa Kenyatta kwa Babu, itakuwa vizuri kujaribu kwanza kumshawishi yeye atoe ushauri kwa Nyerere juu ya manufaa ya shirikisho la Zanzibar na Tanganyika, kama hatua ya kwanza kuelekea kwenye shirikisho kubwa la Afrika Mashariki naamini kuwa UKO UNITED STATES na hivyo kama unahitaji information zaidi basi angalia documents zilizokuwa declassified na jamaa wa STATE DEPARTMENT kuhusu huu muungano wa Tanganyika na Zanzibar utapata nyeti zaidi kisha utaelewa kilitokea nini





Hata hivyo, binafsi swala la OIC naamini ni haki yenu kuamua mnavyotaka kwani Zanzibar ni mke mwenye imani yake ya kidini. Hiyo katiba inasema Tanzania hakuna dini lakini ukweli utabaki kuwa - Zanzibar kuna DINI....
Kwa mantiki hiyo mimi naamini kuwa nyumba (Tanzania) inaweza kabisa kutokuwa na dini lakini mume na mke wakawa na imani zao tofauti, yet maintain relationship bila kuingiza maswala ya dini kwa nia mbaya. Yes, kila mmoja wao anaweza kutokuwa na imani na dini ya mwenziwe lakini swala hapa ni uhusiano wao ndio muhimu. Na nyumba zote zinazoweza kudumu ktk ndoa ya dini tofauti huwa zinaliweka swala hili kama swala la mtu pekee!..
Kwa hiyo Zanzibar kama wanataka kucheza Upatu na OIC wacheze but not on our expense!..


Our expense itakuja pale tutakapo jua pale hii mikataba itakapo wekwa wazi sasa tunakuwa kama wendawazimu tunakuwa tunanegotiate kitu ambacho wengi hawakijui kwani ni TOP SECRET!!!! The bottomline ni kuwa mgogoro mkubwa, ambao umekuwa ukijitokeza, mara kwa mara, ni ule wa kila upande, katika pande mbili za Muungano, yaani Tanganyika na Zanzibar, kudai kuwa unapunjwa na upande wa pili. Wakati Wazanzibari wanadai kuwa Tanzania Bara inataka kuimeza Zanzibar, na Watanganyika wanadai kwa nini Zanzibar iwe na serikali yake ndani ya Muungano wakati ile ya Tanganyika imeuawa?

Hapo ndipo inapochipuka ile hoja ya kuwa na shirikisho la serikali tatu - serikali ya Tanganyika na serikali ya Muungano; jambo ambalo Marehem Mwalimu Nyerere, katika uhai wake, alilivalia njuga kwa kulipinga kwa nguvu zake zote. Na aliyejitokeza kutetea serikali tatu alimnyamazisha kwa gharama yo yote ile MAFANO: Kitendo cha Rais Mstaafu wa Zanzibar, wa Awamu ya Pili, Mheshimiwa Aboud Jumbe, kumwandikia barua Nyerere kumweleza kuwa kwa mujibu wa waraka wa makubaliano ya Muungano ya 1974, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ulikusudiwa uwe ni wa shirikisho lenye serikali tatu, na siyo mbili, au moja, kama inavyodaiwa na CCM -Bara, kilimsababishia Jumbe ajiuzulu nyadhifa zake zote, katika chama na serikali.

Na lile kundi la Wabunge 55 wa Bara, G55, walipotaka iwepo serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano, Nyerere wakati huo akiwa amekwisha ng'atuka Urais wa Tanzania na uenyekiti wa CCM, alisimama kidete kuwapinga wabunge hao na kulisambaratisha kundi lao. Aliandika na kitabu kuwasema na kuwakosoa aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamo Mwenyekiti wa CCM, Mzee Malecela na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Hayati Kolimba, kwa kile alichodai, kumshauri vibaya Rais Mstaafu, wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi.

Lakini hilo halijaweza kuinyamazisha ile hoja ya kuwa na muungano wenye mfumo wa serikali tatu. Kama Mwalimu Nyerere alistahiki kupewa pongezi kwa kufanikisha kuziunganisha Tanganyika na Zanzibar, basi pia, anastahili kulaumiwa kwa kuweka mfumo wa muungano wenye kero nyingi? Na usiokubalika!

Sasa namalizia kwa kuuliza jamani what ever hapened with SOCIAL CONTRACT TANZANIA? mana noana tunapelekwa tuuu huku tunaambiwa hilo siri, hilo halifai kuuliza,hilo dhambi sasa tunalea jamaiii ya namna gani?
 
Dr. WHO,
umesema mengi sana lakini nitajaribu kukujibu kwa ufupi sanaa.
Nimesema mapindizi huja na mengi ikiwa ni KUKAMATWA kwa hao masheikh sidhani kama tulikuwa tukizungumzia MAUAJI...usichanganye vitu brother!
Pili, hakuna mtu anayeweza kutangazia wananchi wote kuwa kesho tutapindua serikali... Kwa hiyo kama Muungano ulipangwa wakati wakipanga mapinduzi sidhani kama hili ni swala la wananchi wote ila ni kwa faida ya wananchi wote. Mnachotaka kufahamu hapa ni kipi hasa!
Tatu, Kwa nini mnataka kuona hizo ulizoziita contract za Muungano?...nambie nchi gani zilizoungana, eti wananchi wake wameelezwa contract za muungano huo.
Marekani imeunganisha states 50 na kuna watu 400/m hakuna kati yao unayejua contact za muungano wao wala haja ya kuziona. Mimi sielewi kabisa sababu ya kutaka kuziona.. mkiziona kisha?... lazima mnatafuta kitu na sio kuziona contracts za hapa na pale.
Basi ombeni hata contract za UHURU wetu toka kwa Muingereza!.. Hii ni dhahiri inaonyesha kuwa mnatafuta vijisababu vya kipuuzi... ni sawa na mtoto anayetaka kujua contract za baba na mama yake kitandani!..

Kosa kubwa lililofanywa na CCM ni kuwakaribisha Hizbu ndani na ndio hawa wanaoleta matatizo yote ya ku-question muungano. Muungano una matatizo? that's another topic lakini kumshitaki Nyerere kuwa ali-force muungano hali mkijua kuwa mapinduzi yalikuwa lazima toka kwa walowezi na mapinduzi yalihitaji kuwa protected..Nyerere alihusika sana na mapinduzi hiyo haina ubishi na hivyo haina ubishi kuwa alihusika na kuwepo kwa muungano. Usalama wa Zanzibar ni usalama wa bara. Angekuwa mjinga kama hakufahamu hili! Looh Hizbu hawa wamekaribishwa ndani sasa wanadai hata mke wapewe!
Sina haja ya kusoma kitabu kilichojaa udhanifu!... Simu imepigwa ktk ubalozi wa Marekani kuwasihi Nyerere, Kenyatta na Obote... mara simu hiyo hiyo inaonyesha kukataliwa na kuendelea kumsihi Nyerere kuhusu Muungano... Huyu Dean Rusk alikuwa akiongea na nani ktk simu hiyo? those years hatukuwa na three way phone! how come simu hiyo hiyo inaeleza tena kuongea na Kenyatta!... Na huyu mtu aliweza vipi kuipata nakala ya simu hiyo?... Just asking... maanake hainiingii akilini kabisa simu ya Ubalozini ikashikwe na mlalahoi asiyekuwa na simu.
Na kama tishio alikuwa BABU why not kill him badala yake washauri muungano hali wakimwacha mbaya wao hai?... Zaidi ilikuwaje wote vigogo unaowasema walichukuliwa na Nyerere na kupewa wadhifa wa juu Bara hali watu hawa walikuwa tishio kwa power ya Nyerere!
Ndugu yangu hizi ni POLITICS ambazo hazina mpango ktk maendeleo ya Zanzibar...Zanzibar imepoteza culture zake na leo hii Uislaam nchini hapo ni kitendawili. Kuna kila laana ambazo hata bara hakuna hali viongozi wanaoendesha maendeleo ya Zanzibar ni Wazanzibar na waislaam. OIC imeshindwa kuwasaidia Somalia, Sudan, Msumbiji na kwingineko zaidi ya kujenga chuo kimoja na kutoa misaada ya chakula basi!.. Wao wenyewe hawana technology zaidi ya kutegemea Marekani..as a fact kila nchi inajitegemea zaidi kuliko mfuko wa OIC. Hiyo OIC ni sawa kabisa na World vision hawana lolote bora hata wajiite NGO tujue moja tutawapa.
 
OIC means "Organization of Islamic Countries". We are not an Islamic country. If you answer, as some are wont to do, that some non-Islamic countries have joined, then may I inform you that there is a principle of logic that says that "two wrongs don't make a right?". We should not copy mistakes.

We are not an Islamic country, and so, we may not join an organization that is meant for Islamic countries. As for Zanzibar, it is not a country. It does not qualify to join an organization of countries, Islamic or otherwise.

Augustine Moshi
 
mkandara nitakujibu kesho panapo majaliwa tukiamka salama usiku mwingi tena saa hizi
 
Dr. WHO,
umesema mengi sana lakini nitajaribu kukujibu kwa ufupi sanaa.
Nimesema mapindizi huja na mengi ikiwa ni KUKAMATWA kwa hao masheikh sidhani kama tulikuwa tukizungumzia MAUAJI...usichanganye vitu brother!




Babaaa vipi ? japo unasema kuwa ulisoma nilichokiandika lakini naona hukutaka kunifahamu niliposema hi:

Quote:
Originally Posted by Mkandara
Dr. Who,
Nimesoma toka hiyo ya nyuma lakini sikuona huo Uhuru unaozungumzia kuwa walikamatwa masheikh! navyojua mimi wakati wa mapinduzi kuna watu walikamatwa. Well, kwanza hapa lazima tuelewe nini maana ya neno MAPINDUZI!.. hili halina kheri kabisa kwa nchi yeyote ile.
Pili, hakuna mtu anayeweza kutangazia wananchi wote kuwa kesho tutapindua serikali... Kwa hiyo kama Muungano ulipangwa wakati wakipanga mapinduzi sidhani kama hili ni swala la wananchi wote ila ni kwa faida ya wananchi wote. Mnachotaka kufahamu hapa ni kipi hasa!


sijakuelewa point yako tafadhali hebu ifafanue kidogo nipate kukuelewa


Tatu, Kwa nini mnataka kuona hizo ulizoziita contract za Muungano?...nambie nchi gani zilizoungana, eti wananchi wake wameelezwa contract za muungano huo.Marekani imeunganisha states 50 na kuna watu 400/m hakuna kati yao unayejua contact za muungano wao wala haja ya kuziona. Mimi sielewi kabisa sababu ya kutaka kuziona.. mkiziona kisha?... lazima mnatafuta kitu na sio kuziona contracts za hapa na pale. Basi ombeni hata contract za UHURU wetu toka kwa Muingereza!.. Hii ni dhahiri inaonyesha kuwa mnatafuta vijisababu vya kipuuzi... ni sawa na mtoto anayetaka kujua contract za baba na mama yake kitandani!..


Unajua pamoja na USOMI wako nakushangaa uanweza ukaja na statement ya namna hii..hivi ushawahi kusikia kitu kinachoitwa SOCIAL CONTRACT? vile vile nakubaliana nawe kuwa si kila mtu ana interest ya kuona contract za muungano lakini at the same time huwezi kuziweka SIRI kwa sababu wananchi wanayo right ya kujua wanatawaliwa based on what? Maneno yako ni sawa na kusema kuwa wananchi HAWAHITAJI KUJUA KATIKA sasa hii ni hatari kwa sababu ina constitute to DICTATORSHIP na matokeo yake siku zote huwa si mazuri

Mfano wako wa AMERICA ni mzuri zaidi kwa sababu kila contract iliyosainiwa na serikali yao iko katika PUBLIC DOMAIN sasa kama kweli serikali yetu tukufu haina cha kificha kwa nini hizi documents ziwe siri? haingii akilini sasa tazamahapa chini uone jinsi jamaa walivyoweka kila kitu open na hata debate zinazoendela leo in the states kwa kiwango kikubwa yanahusu yaliyomo katika CONSTITUTION YAO na hata EUROPE wananchi wanajadili EUROPEAN CONSTITYTION sasa iweje sie tupelekwe tuu na tukitaka kujadili tuaambiwa KOSHER!

hebu tazama mfano wa seerikali inyoongoza

watu:http://www.archives.gov/historical-docs/


Kosa kubwa lililofanywa na CCM ni kuwakaribisha Hizbu ndani na ndio hawa wanaoleta matatizo yote ya ku-question muungano. Muungano una matatizo? that's another topic lakini kumshitaki Nyerere kuwa ali-force muungano hali mkijua kuwa mapinduzi yalikuwa lazima toka kwa walowezi na mapinduzi yalihitaji kuwa protected..Nyerere alihusika sana na mapinduzi hiyo haina ubishi na hivyo haina ubishi kuwa alihusika na kuwepo kwa muungano.
Usalama wa Zanzibar ni usalama wa bara. Angekuwa mjinga kama hakufahamu hili! Looh Hizbu hawa wamekaribishwa ndani sasa wanadai hata mke wapewe!
Sina haja ya kusoma kitabu kilichojaa udhanifu!... Simu imepigwa ktk ubalozi wa Marekani kuwasihi Nyerere, Kenyatta na Obote... mara simu hiyo hiyo inaonyesha kukataliwa na kuendelea kumsihi Nyerere kuhusu Muungano... Huyu Dean Rusk alikuwa akiongea na nani ktk simu hiyo? those years hatukuwa na three way phone! how come simu hiyo hiyo inaeleza tena kuongea na Kenyatta!... Na huyu mtu aliweza vipi kuipata nakala ya simu hiyo?... Just asking... maanake hainiingii akilini kabisa simu ya Ubalozini ikashikwe na mlalahoi asiyekuwa na simu.



Unashangaza kweli wewe unasema in 1960's Americans walikuwa hawana simu za 3 way...duh! wewe kiboko nadhani nazungumza na mtoto wa jana ambaye haangaliii facts zake kabla ya kuziweka bayana...jibu la hilo ndi ndogo zsasa angalia picha zilizopigwa wakati wa CUBAN missle criisis utaona kuwa hawa jamaa walikuwa na technology ambayo ni ya mbali sana...yaani wapeleke binadamu mwezini halafu washindwe kuwa na 3 way phones!

anyways nitakusamehe kwa hilo na nitarudi katika mada yetu....sijui unauelwa gani wa politics za Zanzibar lakini ukweli usiopingika ni kuwa migogoro ndani ya muungano, katika huu mfumo wa serikali mbili haitakoma. Kila itakapochomoza itatumiwa mizengwe kuinyamazisha. Lakini hiyo si dawa! Njia pekee ya kumaliza migogoro hiyo ni kwa pande mbili kwa kutafuta mfumo, utakaokubalika na pande zote mbili. Kudai kuwa muungano huu ni wa serikali mbili kuendea serikali moja, ndiyo sera ya CCM nindoto ya mchana! Ikawa CCM-Bara inaota hivyo, ijue kuwa CCM-Visiwani, haitakubali, hata siku moja, kuiua na kuizika serikali ya Zanzibar kwa mikono yake yenyewe. Labda ilazimishwe kwa mkong'oto! Kwa taarifa yako CCM-Visiwani, inakubali mfumo wa serikali mbili, kwa sababu mfumo huo unadhamini kuwapo ile serikali ya Zanzibar; lakini kama mfumo huu utataka kubadilishwa na kuwekwa mfumo wa serikali moja tu; basi CCM-Zanzibar itakuwa tayari kuukubali mfumo wa serikali tatu, unaotakiwa na wapinzani Zanaibar, kuliko kukubali mfumo wa serikali moja. Kwa sababu mfumo wa Serikali tatu utaiwezesha serikali ya Zanzibar kuendelea kuwapo.

Ndugu yangu hizi ni POLITICS ambazo hazina mpango ktk maendeleo ya Zanzibar...Zanzibar imepoteza culture zake na leo hii Uislaam nchini hapo ni kitendawili. Kuna kila laana ambazo hata bara hakuna hali viongozi wanaoendesha maendeleo ya Zanzibar ni Wazanzibar na waislaam. OIC imeshindwa kuwasaidia Somalia, Sudan, Msumbiji na kwingineko zaidi ya kujenga chuo kimoja na kutoa misaada ya chakula basi!.. Wao wenyewe hawana technology zaidi ya kutegemea Marekani..as a fact kila nchi inajitegemea zaidi kuliko mfuko wa OIC. Hiyo OIC ni sawa kabisa na World vision hawana lolote bora hata wajiite NGO tujue moja tutawapa.


Hija yako ni hafifu kwa sababu huzungumziii hali ya mgogoro wa muungani ambao Jana LOWASA anajaribu kuutafutia ufumbuzi. kumbuka kuwa katika huu mfumo wa vyama vingi, mfumo ya serikali mbili utaendelea kuwapo, katika ule muda ambapo chama cha CCM kitaendelea kuwapo katika madaraka; lakini jee kama CUF Zanzibar wangashinda katika uchaguzi mkuu uliopita wangekubali kuendelea na mfumo wa serikali mbili? Itakuwa kila serikali inayoingia madarakani ibadilishe muundo wa muungano? Kwa nini hatuweki mfumo unaokubalika na wote, ili upate kuheshimiwa na wote?

je una habari kwamba kunakipindi wafanyabiashara wa Zanzibar waligoma kupeleka bidhaa Bara, kwa sababu ya kutozwa ushuru mara mbili, wakiingiza bidhaa Zanzibar kutoka nje wanatozwa ushuru na wanapozipeleka Bara, kwa ajili ya kutafuta soko, hutozwa ushuru mara ya pili?Swali hili si la leo. Ni la siku nyingi sana. Basi kwa nini halitafutiwi njia mwafaka ya kulitatua? Au sera ya muungano huu ni kuendeleza migogoro?


na kama tunaona tunashindwa kuishi pamoja kwani lazima tuwe ndani ya muungano? twaweza kuuvunja na kila mmoja akangalia lwake kwa sababu muungano ulikuwa haupo ,then ukawepo then unaweza ukawa usiwepo ni fact of life kama ndoa vile ..ikishindikana ya nini kungangania kuishi maisha ya kulumbana kila siku? same kama tulivyiokuwa ndani ya EAC tujkatoka..tumerudi twaweza kutoka vile vile no big deal
 
OIC means “Organization of Islamic Countries”. We are not an Islamic country. If you answer, as some are wont to do, that some non-Islamic countries have joined, then may I inform you that there is a principle of logic that says that “two wrongs don’t make a right?”. We should not copy mistakes.

We are not an Islamic country, and so, we may not join an organization that is meant for Islamic countries. As for Zanzibar, it is not a country. It does not qualify to join an organization of countries, Islamic or otherwise.

Augustine Moshi



But how can we discuss the OIC without even knowing what was in the Union memorandum?

how about thinking beyond government led propaganda?
 
Dr. WHO,

Looh wewe kiboko bob!.. ulisema mwanzo kuwa Masheikh walikamatwa siku ya UHURU.. nikakuuliza UHURU wa wapi Bara au Visiwani? Hakutoa jibu kabisa hadi sasa. Nikasema kama ni wakati wa Mapinduzi unajua tena mengi huja na Mapinduzi... wewe umedai tena Mapinduzi gani hayo ya KUUA. Well, tumetoka ktk swali la UHURU na kuwa Mapinduzi kisha ukaongea madai kuwa mapinduzi sii lazima yawe ya KUUA. Damn!...wewe kiboko maanake umekosa tu kumuuliza Kimathi kuwa hata UHURU sio lazima watu wauane....
Pili, Hizo links ulizotoa zinaonyesha Bills of act au Katiba hazihusiani kabisa na contract za MUUNGANO wa states za Marekani...Kwani katiba ya Muungano pia huipati mshikaji?..
Anyway, DR. WHO, Contract za MUUNGANO ni sawa na WILL yaani huwezi kuziona hadi hapo mweka WILL atakapo kufa!.... kwa hiyo vunja Muungano utapata kuziona zaidi ya hapo madai ya hawa Wazenji hayana msingi... makubaliano ya kupindua Utawala wa Sultan na kuulinda kwa Muungano ulifanywa na baadhi ya watu na sio lazima kabisa wewe uone hayo makubaliano.
Haya ndiyo matatizo yanayowapata hata Wakenya ambao kabla ya Uhuru wao walimwita Kimathi na Maumau kuwa mashetani wala nyama za watu, watu wasiokuwa na dini na mengine mengi kuwapaka Wakikuyu... Haya huyohuyo Maumau kawaletea UHURU wakaanza kupindua na kudai kuwa Wakikuyu wanajipendelea.... Hali ni haohao Wakikuyu walikuwa wakiitwa mashetani wala watu... je, kweli ni akili leo hii Wakenya kutaka kuona mikataba ya Kimathi na MAUMAU ilikuwa vipi ktk kupigania UHURU badala ya kutafuta haki zao kulingana na hali ya LEO!...tena kibaya zaidi mtu huyu anayetafuta hizo nakala ni kutaka kuhakikisha kuwa Kimathi kweli alikuwa akila watu. Damn!
Dr. WHO nipo mitaa hii karibu miaka ishirini na 3 way line ni new technology brother, 1960 haikuwepo. Hiyo kwenda mwezini haihusiani kabisa na simu kwani haohao wazungu walivumbua magari na treni kabla hata ya simu. Kwa hiyo ukubwa wa kitu sii lazima kiwe kinachelewa na kidogo kuwahi. Kisha ktk maelezo ya huyo mwandishi inaonyesha conference yenyewe ilikuwa ya pande nne. 1. CIA 2. Ubalozi wa Marekani Kenya 3. Kenyatta na 4. Nyerere. Besides, How CIA can they be so stupid! kueneza habari za siri kwa watu wazi hivyo bila kufahamu kama mmoja wao atapinga na pengine kutoa siri?

hakuna aliyesema MUUNGANO hauna matatizo!.. sote tunaelewa kuna matatizo lakini kosa lenu mnaifanya ISSUE kuwa WATU na sio MUUNGANO. Hapa mnatumia MUUNGANO kama chambo tu lakini matatizo yenu ni WATU tena wale wanaotoka BARA na wakristu.. Hii ndio sababu tatizo la Muungano linashindwa kabisa kutatuliwa kwa sababu mnapoteza muda mwingi kujadili WATU badala ya Muungano wenyewe.
Dr. WHo unajua sometimes nafikiri majibu ya mkato kama alivyosema Augustine Moshi ndio dawa pekee. Ukiwa hutaki mkeo awe na urafiki na mtu fulani basi usitake kueleza sababu kwani utazua maswali zaidi. NISIKUONE na MWATUMU... period. Maelezo mengi hayayewezi ku-solve problem ya mtu ambaye kajichimbia ktk kabati na hataki kuona nje yake.

Nitamalizia kwa kukupa msimamo wangu wa maswala haya....
Nitakupa mfano mmoja mzuri sana na sijui kama umewahi kuufikiria.
Unajua kuhusu swala la mavazi majuzi Holland wameweka sheria kuzuia wanawake wa kiislaam wasivae Hijab..
Well, kwa washabiki wanaotazama WATU kama ndio problem WATAKUBALIANA na sheria hiyo na Upande wa pili wale pia wanatazama bado WATU kama problem WATAPINGA sheria hiyo... Je, mimi nitasema nini?..Nitasema WOTE wajinga na labda kwa msemo wa Mzee ES, hii ni NONSENSE!
Hapa wote hawa wanatazama rangi za watu kutoa hukumu zao na wala sii haki ya binadamu. Huyo mzungu Mhollanzi anataka Hijab iwe baned ni huyo huyo atakaye taka kuvaa nusu Uchi akiwa Arabuni na kudai haki ya kujichagulia kuvaa. Na Mwarabu ambaye atapinga sheria hii ya Holland kwa madai ya haki za binadamu ni huyohuyo anayeweka sheria Arabuni wazungu wasivae nguo fupi!...
nadhani umenipata point yangu!
 
unajua wewe uko states na sasa hivi huko mchana usiku ushakuwa mwingi hapa babu
 
Wa-Zanzibari waruhusiwe kuingia hilo shirika bila ya kusumbuliwa, na sisi wa Bara tuache tabia za kizamani za kukataa tu vitu bila ya kuelewa, na kwa sababu Mwalimu alisema, Uganda ni mwana chama wa shirika hilo na bado ni rafiki mkubwa wa the West, if that is the case,

Muungano umeshindwa kuwasaidia ndugu zetu matatizo yao, kama hiyo ilikuwa i moja ya sababu za kuungana, sasa Bara hatuwezi kuendelea kuwa blackmailed na hawa wavisiwani kila wakati kwa kisingizio cha kuwanyima kuingia shirika hilo,

tuwaruhusu na tupunguze misaada ya kuwapa umeme bure, na mishahara ya serikali kila wanapokwama, enough is enough, waende huko bila conditions tena now!
 
Wa-Zanzibari waruhusiwe kuingia hilo shirika bila ya kusumbuliwa, na sisi wa Bara tuache tabia za kizamani za kukataa tu vitu bila ya kuelewa, na kwa sababu Mwalimu alisema, Uganda ni mwana chama wa shirika hilo na bado ni rafiki mkubwa wa the West, if that is the case,

Muungano umeshindwa kuwasaidia ndugu zetu matatizo yao, kama hiyo ilikuwa i moja ya sababu za kuungana, sasa Bara hatuwezi kuendelea kuwa blackmailed na hawa wavisiwani kila wakati kwa kisingizio cha kuwanyima kuingia shirika hilo,

tuwaruhusu na tupunguze misaada ya kuwapa umeme bure, na mishahara ya serikali kila wanapokwama, enough is enough, waende huko bila conditions tena now!





MZEE ES

Kwa mara ya kwanza nakiri kukubaliana na wewe by 100% katika majibu yako ya hapo juuu

unajua ni kama ndoa ikishindikana basi kila mmoja aangalie ustarabu wake sasa sisi tunangangania nini?

Vile vile wao wanaishi kwa subsidies za Bara...kama Umeme na kadhalika sasa sijui kwa nini wanasiasa especially wa CCM bara wanangangania huu muungano ambao kwa uapnde wangu uko ONE SIDED na pili hakuna anayetaka kueleza mkataba wake ukoje na tatu watu hawaruhusiwi kuulizia sasa huu ni kufanyana wapumbavu
 
Halafu tusijifanye kuwa sisi tu ndio tuna Muuungano, maana hata US ni muungano wa states, nchi kama Hawaii, Perto-Rico si nazo zilikuwa nchi kamili lakini zikaungana na US na hakuna mang'ana, sasa sisi bongo ni nini hiki ambacho basii imekuwa taabu tuuuu, yaani muuungano umekuwa muuungano tuuuu, hakuna lolote la maana!

Sasa tumefikia hata kuwapa kazi watu wasiokuwa na uwezo kwenye mabalozi yetu nje, eti mradi tu ionekane kuna mchanganyiko wa watu wa muungano, NONESENSE!

jamani enough! hawa wavisiwani waruhusiwe kuamua maamuzi muhimu kwa uchumi wao ambayo serikali ya muuungano imeshindwa kuyakabili, haiwezekani kisiwa chenye wananchi wasiozidi millioni moja wahanagaike tuuu kwa sababu ya muuungano, eti mpaka tuna waziri wa muungano, kazi yake ni nini? maana kama kweli angekuwa na kazi muhimu haya mambo tusingeyasikia kwenye media yangemaliziwa huko kwenye wizara au vikao vya siasa vya muuungano kama vipo, the fact kwamba tunasikia makelele ina maana havipo!

Wa-Zanzibari waruhusiwe kuingia sio hao jamaa tu hata na wengine kama wapo, ambao watawasaidia kiuchumi, maana sisi Bara tumeshindwa kuwasaidia, kama ni lazima basi tuendelee tu na muuungano wa siasa, lakini sio kiuchumi, tuwaache watafute mbinu zao za kuhimili uchumi badala ya kuitegemea serikali ya Bara, ambayo imejaaa wezi watupu na wahuni kazi kucheza mazingaombwe!
 
nadhani sasa inabidi tuzungumzie kuuvunja muungano

kwa sababu hakuna anyeutaka zaidi ya wanasiasa
 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ijiunge na OIC. Zanzibar haina mamlaka ya kikatiba kujiunga na chombo hicho.

Misaada ya OIC ipelekwe kwa watanzania wote kwa kuzingatia mahitaji--bara na visiwani, waislamu,wakristo, pamoja na wasio na dini yoyote.
 
Wa-Zanzibari waruhusiwe kuingia hilo shirika bila ya kusumbuliwa, na sisi wa Bara tuache tabia za kizamani za kukataa tu vitu bila ya kuelewa, na kwa sababu Mwalimu alisema, Uganda ni mwana chama wa shirika hilo na bado ni rafiki mkubwa wa the West, if that is the case,

Muungano umeshindwa kuwasaidia ndugu zetu matatizo yao, kama hiyo ilikuwa i moja ya sababu za kuungana, sasa Bara hatuwezi kuendelea kuwa blackmailed na hawa wavisiwani kila wakati kwa kisingizio cha kuwanyima kuingia shirika hilo,

tuwaruhusu na tupunguze misaada ya kuwapa umeme bure, na mishahara ya serikali kila wanapokwama, enough is enough, waende huko bila conditions tena now!

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ijiunge na OIC. Zanzibar haina mamlaka ya kikatiba kujiunga na chombo hicho.

Misaada ya OIC ipelekwe kwa watanzania wote kwa kuzingatia mahitaji--bara na visiwani, waislamu,wakristo, pamoja na wasio na dini yoyote.






Bwana Joka Kuu

sasa hivi tena ishu siyo OIC bali namna ya kuuvunja huo muungano kisha kila mmoja achukue chake
 
DrWHO,
Binafsi naunga mkono kuvunjwa kwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Kama Wazanzibari hawataki serikali moja, basi sioni sababu ya kuendelea na Muungano. Siamini kama watanganyika watatendewa haki ikiwa kutakuwa na serikali tatu.
 
well

Actually its not kuwa Wazanzibari hawautaki muungano...the same applies na wabara ambao wamekuwa wakiwalipia almost kila kitu wazanzibari hivyo kila mtu kachoka..wa bara na wa visiwani na kilichobaki ni kuguess ni muda gani itachukua mpaka huo muungano uvunjike
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom