Wasichana huchagua wenza wao mapema

Wasichana huchagua wenza wao mapema

Nchi Kavu

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2010
Posts
4,290
Reaction score
2,468
Habari za Eid pili wandugu

Kama kawaida yangu ninapitulia ndipo jambo hunijia kama hivi halafu natafuta pakukitolea.

Nimekumbuka tu mbali kidogo miaka hiyo ya ubarubaru. Kipindi ambacho kwa bahati mbaya vijana wa kiume hukitumia ndivyo sivyo, pengine ni kwa kukosa misingi thabiti toka kwa jamii inayowazunguka.

Miaka ya 27 hadi 32 kwa vijana wa kike na wa kiume. Katika umri huu ni vijana wa kike ndio aghalabu huwa na focus ya maisha. Pengine huwa wamepevuka zaidi kuliko wa kiume.

Ni kipindi hiki ambapo vijana wa kike (wasichana) huchagua wanaume wa ndoto zao kwa maana ya kujenga maisha na familia. Huwa haitokei bahati mbaya ila wao kwa muda wao hufanya chunguzi zao na muda ukifika wewe kijana wa kiume uliyetunukiwa chaguo hilo utaona baadhi ya dalili na ishara.

Hapa naomba niweke bayana. Naongelea zaidi vijana wale ambao 'umande' kwao ulikuwa rafiki. Wale wengine hata miaka 18, 22 poa tu.

Dalili na ishara hizi hawa wanaume huziona bayana, tatizo linakuja, aidha hajamalizana na viruka njia au anaona huyo binti sio sahihi kwake. Tatizo la tatu huwa ni kipato. Hili la kipato likae pending kwanza.

Nasema haya kwa kuwa nimepita huko. Kama kuna makosa vijana wa kiume hufanya, ni kipindi hiki. Mwanamke aliyekuchagua kati ya wengi ndiye alipaswa kuwa mke wako. Bahati mbaya huwa tunawapuuzia na kwenda kuwatafuta wale wa vigezo vyetu.

Nawaasa vijana wa kiume. Mwanamke anayekuchagua kati ya wengi huyo mpe nafasi
 
Wanawake wa kipind hiki,
Wako tayar kumtunuku kiumbe yeyote penzi ili mradi tu awe nazo PESA.

Ikifika miaka 35,
wanakuja jf kutafuta mwanaume anayepumua tu.

Hii yote inachangiwa na ugumu wa maisha na upungufu wa maadili kwenye jamii zetu
 
Wanawake wa kipind hiki,
Wako tayar kumtunuku kiumbe yeyote penzi ili mradi tu awe nazo PESA.

Ikifika miaka 35,
wanakuja jf kutafuta mwanaume anayepumua tu.

Hii yote inachangiwa na ugumu wa maisha na upungufu wa maadili kwenye jamii zetu
Inawezekana kweli kwa kizazi hiki maana dunia inaenda kasi
 
Nakubaliana na wewe
kua mwanamke anayo nafas kubwa ya kumchagua mwenza wake KIMAPENZI na ikawa kweli akafanikiwa.

Hii yote inachangiwa na huruma kubwa walionao wanaume wengi kwa wanawake, pindi mwanamke anapokua na hitaji lake kwa mwanamke.

Ila NAKUHAKIKISHIA
Ila linapokuja suala la MWENZI WA MAISHA NA KUJENGA FAMILIA, mwanaume ndio mwamuzi No.1

Na hapa ndipo wanawake wanapofeli ktk kuzichanga karata zao vema .
 
Huu uamuzi wa mwanaume nakubaliana nawe asilimia zote. Laiti kama uamuzi huu ungekuwa hauna hitilafu huko mbeleni tungeweza kusema ni sahihi. Hitilafu kwa maana ya kuhitilafiana, migogoro, n.k.

Pengine angempa nafasi yule mwanamke aliyeonyesha kumhitaji labda maisha yangenyooka siku zote
 
Ni kweli, wakati we bado unashangaza shangaa kuna binti anakuchagua siriaz kabisa
 
Nakubaliana na wewe
kua mwanamke anayo nafas kubwa ya kumchagua mwenza wake KIMAPENZI na ikawa kweli akafanikiwa.

Hii yote inachangiwa na huruma kubwa walionao wanaume wengi kwa wanawake, pindi mwanamke anapokua na hitaji lake kwa mwanamke.

Ila NAKUHAKIKISHIA
Ila linapokuja suala la MWENZI WA MAISHA NA KUJENGA FAMILIA, mwanaume ndio mwamuzi No.1

Na hapa ndipo wanawake wanapofeli ktk kuzichanga karata zao vema .
Ndoa ya wawili ama ya mmoja?.
Kama hujapendwa utakubaliwaje?
Ama ni sawa tu kupendewa pochi?
 
Sichaguliwi, nachagua.

Kama I have to sleep with only one woman for the rest of my life and forsake all others, it better be on my terms
 
Sichaguliwi, nachagua.

Kama I have to sleep with only one woman for the rest of my life and forsake all others, it better be on my terms
Muda si mrefu nimesoma hapa jukwaani stori ya jamaa aliyelipiza kisasi kisa kusalitiwa. Kuwa na terms zako haizuii kuchapiwa ikibidi
 
Mtoa mada upo sawa kabisa ..

Dc mstaafu Ole sabaya!! Akupaswa kuishi katika cheo hiki!!

Jaman hii simu inatype nin tena:[emoji850]

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wanawake wa kipind hiki,
Wako tayar kumtunuku kiumbe yeyote penzi ili mradi tu awe nazo PESA.

Ikifika miaka 35,
wanakuja jf kutafuta mwanaume anayepumua tu.

Hii yote inachangiwa na ugumu wa maisha na upungufu wa maadili kwenye jamii zetu
Wanakuja JF au wanajazana kwa mwamposa au nabii Enock pale Tangibovu tena jana nilipanda daladala walikuwa wengi wametoka kwa mwamposa
 
Wanakuja JF au wanajazana kwa mwamposa au nabii Enock pale Tangibovu tena jana nilipanda daladala walikuwa wengi wametoka kwa mwamposa
Changamoto saNa,
sema mi naona wanajifanyia mazingaombwe (ILLusION) wenyewe.

Ni kwamba,
Wanaume wanaoenda kuwatafuta uko makinisani,
Ndo hao hao wanaume walionao uko mitaani, wanaowasimamisha kuwaomba namba wanawalingia na kuwakataa.

Sema tu Uko makanisani,
wanatafuta justification tu za kiroho kwa kuzidanganya nafsi zao kua hao Ni wanaume bora waliotoka kwa bwana.
 
Back
Top Bottom